Matangazo
◼ Toleo la Januari 2007: Kitabu chochote cha kurasa 192 chenye karatasi inayochujuka, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1991, kinaweza kutolewa. Kitabu Ujuzi au broshua Endeleeni Kukesha! inaweza kutolewa pia. Februari: Tutatoa kitabu Mkaribie Yehova na kitabu Ujuzi. Machi: Tutatoa kitabu Biblia Inafundisha na tutajitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tunapowarudia watu waliopendezwa tutajitahidi kuwatolea kitabu Biblia Inafundisha, tukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Kuanzia Februari, na kabla ya Machi 4, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa, “Ni Nani Atakayestahili Kuingia Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu?”
◼ Video, Young People Ask—What Will I Do With My Life? itazungumziwa katika mkutano wa Utumishi mwezi wa Aprili. Ikihitajika, video hiyo inaweza kuombwa kupitia kutaniko haraka iwezekanavyo.
◼ Vichapo vyetu vinachapishwa kwa Kichina cha aina mbili. Watu kutoka Hong Kong na Taiwan wanasoma Kichina cha kiasili, ambacho tumekipa alama “Kichina” (CH). Idadi kubwa ya Wachina wengine husoma Kichina kilichorahisishwa kinachoitwa “Kichina Sahili” (CHS). Kwa kuwa Kichina ambacho mtu anasoma ni tofauti hata iwe anazungumza Kikantoni, Kimandarini, au lahaja nyingine, ni vizuri kujua anapendelea Kichina gani hasa. Ili kujua mtu anapendelea Kichina kipi, unaweza kutumia kijitabu Good News for People of All Nations, ukurasa wa 19-20. Kwa njia hiyo, vichapo vitaombwa kulingana na lugha inayohitajiwa.
◼ Makutaniko yanapaswa kufanya mipango inayofaa ya kuadhimisha Ukumbusho wa mwaka huu siku ya Jumatatu, Aprili 2, baada ya jua kushuka. Ingawa hotuba inaweza kuanza mapema, mkate na divai havipaswi kupitishwa kabla ya jua kushuka. Chunguzeni wakati ambapo jua litashuka katika eneo lenu siku hiyo. Ni afadhali kila kutaniko liadhimishe Ukumbusho likiwa peke yake. Hata hivyo, huenda hilo lisiwezekane. Mahali ambapo kwa kawaida makutaniko kadhaa hutumia Jumba moja la Ufalme, kutaniko moja linaweza kutumia Jumba la Ufalme na yale mengine yanaweza kukutanika mahali pengine jioni hiyo. Ikiwa makutaniko kadhaa yatatumia Jumba moja, ikiwezekana tunapendekeza kuwe na muda wa angalau dakika 40 kati ya programu ili wote wafaidike kikamili na ushirika baada ya Ukumbusho. Hakikisheni kuwa hakuna msongamano wa magari. Pia hakikisheni kuna mahali pa kuegesha magari na pa kushusha na kubeba abiria. Mabaraza ya wazee yanapaswa kufanya mipango inayofaa.
◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuhakikisha kwamba wana barua ya kuwekwa rasmi kwa painia (S-202) ya kila painia wa kawaida kutanikoni. Ikiwa hawana wanapaswa kuiandikia ofisi ya tawi.