Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/07 uku. 1
  • Tumekabidhiwa Hazina

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumekabidhiwa Hazina
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Weka Moyo Wako Juu ya Hazina za Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Unaweza “Kumjua Mungu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Thamini Pendeleo Lako la Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Hazina Yetu, Huduma Tukufu ya Ki-Siku-Hizi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 2/07 uku. 1

Tumekabidhiwa Hazina

1 Mtume Paulo alithamini utume wa kuhubiri aliopewa na Mungu naye akaurejezea kuwa “hazina.” (2 Kor. 4:7) Alivumilia hali ngumu na mnyanyaso alipotimiza utume huo. Alimhubiria bila kuchoka mtu yeyote aliyekutana naye. Alifunga safari nyingi ngumu na zenye hatari kwenye nchi kavu na baharini. Tunaweza kumwigaje Paulo na kuonyesha kwamba tunathamini huduma yetu? (Rom. 11:13) Ni nini kinachofanya huduma yetu iwe hazina isiyo na kifani?

2 Hazina Yenye Thamani Zaidi: Mara nyingi hazina za kidunia humletea mtu maumivu ya moyo na manufaa ya muda tu. Kwa upande mwingine, huduma yetu hutuletea sisi na wengine manufaa ya kudumu. (1 Tim. 4:16) Huduma hiyo huwasaidia watu wanyoofu kumjua Yehova, kufanya mabadiliko yanayohitajika maishani, na kupata tumaini halisi la uzima wa milele. (Rom. 10:13-15) Tunapoona huduma yetu kuwa kitu chenye thamani, tunapata kusudi lenye kuridhisha maishani, hisia ya kudumu kwamba tumetimiza jambo muhimu, na tumaini lenye kutia-moyo kwa ajili ya wakati ujao.—1 Kor. 15:58.

3 Onyesha Kwamba Unathamini Hazina Yako: Mara nyingi tunapojidhabihu tunaonyesha tunakithamini kitu kwa kadiri gani. Ni pendeleo kama nini kutumia wakati na nguvu zetu kumsifu Yehova! (Efe. 5:16, 17) Njia ambayo sisi hutumia wakati wetu inapaswa kuonyesha kwamba tunathamini zaidi mambo ya kiroho badala ya mambo ya kimwili. Kwa kuwa tuna kitu chenye thamani sana cha kuwapa wengine, bila shaka tutahubiri kwa uchangamfu na kuwa chonjo kuhubiri habari njema kila tunapopata nafasi.

4 Kwa kawaida, sanaa zenye thamani hazifichwi, bali huwekwa wazi katika majumba ya maonyesho ili kila mtu afurahie kuziona. Tukiona huduma yetu kuwa yenye thamani, itakuwa jambo kuu maishani mwetu. (Mt. 5:14-16) Tukiwa na mioyo iliyojawa uthamini, sikuzote na tumwige mtume Paulo kwa kutumia kila nafasi kuonyesha tunathamini kikweli huduma yetu, na kuiona kuwa hazina.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki