Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/07 uku. 3
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma ya Ufalme—2007
Huduma ya Ufalme—2007
km 3/07 uku. 3

Matangazo

◼ Toleo la Machi: Tutatoa kitabu Biblia Inafundisha na tutajitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tunapowarudia watu waliopendezwa, kutia ndani wale ambao huhudhuria Ukumbusho na/au mikutano mingine ya pekee ya kitheokrasi lakini hawashirikiani sana na kutaniko, tutajitahidi kuwatolea kitabu Biblia Inafundisha, tukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia. Juni: Tutatoa kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? au Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Pia kitabu Ujuzi kinaweza kutolewa.

◼ Wahubiri wanapaswa kupewa matoleo mapya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! mara tu yafikapo. Hilo litawawezesha kufahamu habari zilizomo kabla ya kuyatoa magazeti hayo katika utumishi wa shambani.

◼ Mwangalizi-msimamizi au ndugu fulani aliyeteuliwa naye anapaswa kukagua hesabu za kutaniko za miezi ya Desemba, Januari, na Februari. Ukaguzi ukikamilishwa, kutaniko linapaswa kutangaziwa ripoti ya ukaguzi pamoja na ripoti ya hesabu itakayofuata.—Ona Maagizo ya Kufanyia Hesabu za Kutaniko (S-27).

◼ Mwandishi wa kila kutaniko ambalo lina Jumba la Ufalme anapaswa kuhakikisha kwamba wameondolewa wajibu wa kulipa ushuru au kodi kwa ajili ya Jumba la Ufalme. Barua zozote zinazoondoa wajibu wa kulipa ushuru na kodi zinapaswa kuwekwa katika faili ya kudumu. Hakikisheni kwamba ofisi ya tawi ina nakala ya barua hizo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki