Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/07 uku. 1
  • “Anampa Nguvu Mtu Aliyechoka”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Anampa Nguvu Mtu Aliyechoka”
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Humpa Nguvu Aliyechoka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Yehova Humpa Nguvu Mwenye Kuchoka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Kupata Nguvu Mpya, Si Kuchoka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • “Yeye Humpa Nguvu Mtu Aliyechoka”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 5/07 uku. 1

“Anampa Nguvu Mtu Aliyechoka”

1 Sisi sote huchoka. Huenda tukachoka kwa sababu ya kazi au shughuli nyingine, au hata kwa sababu ya matatizo tunayokabili katika “nyakati [hizi] za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” (2 Tim. 3:1) Tukiwa watumishi wa Yehova, sisi hupataje nguvu za kiroho tunazohitaji ili tusipunguze bidii katika huduma yetu? Sisi hupata nguvu hizo kwa kumtegemea yule aliye “hodari katika nguvu,” Yehova. (Isa. 40:26) Anajua mahitaji yetu na kwa kweli anataka kutusaidia.—1 Pet. 5:7.

2 Maandalizi ya Yehova: Yehova hutupa nguvu kupitia roho yake takatifu, nguvu zilezile alizotumia kuumba ulimwengu wote. Tunapochoka, roho ya Mungu hutusaidia ‘kupata nguvu mpya.’ (Isa. 40:31) Jiulize hivi, ‘Ni lini mara ya mwisho niliposali kihususa kwa ajili ya roho takatifu ili inipe nguvu za kutimiza wajibu wangu wa Kikristo?’—Luka 11:11-13.

3 Kila siku tukisoma na kutafakari Neno la Mungu lililoandikwa kwa mwongozo wa roho na tukijengwa kiroho kwa kujifunza vichapo vya Kikristo kwa ukawaida, tutakuwa kama “mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao hutoa matunda yake katika majira yake na ambao majani yake hayanyauki.”—Zab. 1:2, 3.

4 Pia, Yehova huwatumia waamini wenzetu, ambao wanaweza kuwa ‘msaada wenye kututia nguvu.’ (Kol. 4:10, 11) Wanatutia nguvu katika mikutano ya kutaniko kupitia mazungumzo, maelezo, na hotuba zao zenye kujenga. (Mdo. 15:32) Wazee Wakristo hasa hutusaidia kiroho, hututia moyo, na kutuburudisha.—Isa. 32:1, 2.

5 Huduma: Ukihisi kwamba unaanza kuchoka, usiache kuhubiri! Tofauti na shughuli nyingine ambazo hutuchosha, kushiriki kwa ukawaida katika huduma hutuburudisha. (Mt. 11:28-30) Kuhubiri habari njema hutusaidia kukazia fikira Ufalme wa Mungu na kutazamia kwa hamu wakati ujao wa milele na baraka zake.

6 Kuna mengi ya kufanya kabla mfumo huu mbovu haujaharibiwa. Tuna sababu nzuri za kubaki imara katika utumishi wetu, ‘tukitegemea nguvu ambazo Mungu hutoa.’ (1 Pet. 4:11) Kwa msaada wa Yehova tutamaliza kazi yetu, kwa kuwa “anampa nguvu mtu aliyechoka.”—Isa. 40:29.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki