Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatashughulikiwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Desemba 31, 2007. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Novemba 5 hadi Desemba 31, 2007.
SIFA ZA USEMI
1. Ni mambo gani tunayopaswa kukumbuka ili hotuba yetu iwe na umalizio mzuri? [be uku. 221 fu. 1-4]
2. Tunaweza kuhakikishaje kwamba yale tunayosema katika huduma ya shambani ni sahihi? [be uku. 223 fu. 2-4]
3. Tunapotoa hotuba katika mikutano ya kutaniko, tunaweza kuonyeshaje kwamba tunaheshimu sana kutaniko likiwa “nguzo na tegemezo la ile kweli”? (1 Tim. 3:15) [be uku. 224 fu. 1-4]
4. Kwa nini ni muhimu kuchunguza ikiwa habari tunayozungumzia inategemeka, na tunaweza kufanyaje hivyo? [be uku. 225 fu. 1-2]
5. Tunapofundisha, tunaweza kuwasaidiaje wengine waelewe kwa urahisi habari tunayozungumzia? [be uku. 226 fu. 3-uku. 227 fu. 1]
HOTUBA NA. 1
6. Ni nini kinachothibitisha simulizi la Yona kuwa asilia? [si uku. 153 fu. 3]
7. Ni unabii gani wa Mika unaokamatana na utawala wa Ufalme wa Mungu kupitia Kristo Yesu? [si uku. 158 fu. 18]
8. Ni nini kinachothibitisha kitabu cha Habakuki kimepuliziwa na Mungu? [si uku. 161 fu. 4]
9. Kwa nini inaweza kusemwa kwamba kufikia 520 K.W.K. Wayahudi walikuwa bado hawajatimiza kusudi la kurudi kwao kutoka uhamishoni? (Hag. 1:4) [si uku. 166 fu. 3]
10. Kwa kurudia-rudia Zekaria arejezea kwenye siku gani tukufu? [si uku. 172 fu. 26]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
11. Unabii wa Yoeli kuhusu shambulio la wadudu ulitimizwa kwa njia gani katika karne ya kwanza, na unatimizwaje leo? (Yoe. 2:1-10, 28) [w07 10/1 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yoeli na cha Amosi”]
12. “Kikapu cha matunda ya wakati wa kiangazi” kilimaanisha nini? (Amo. 8:1, 2) [w07 10/1 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yoeli na cha Amosi”]
13. Ni katika maana gani kwamba Yehova ‘alijuta juu ya msiba ambao alikuwa amesema ataleta juu ya Waninawi,’ na hilo linatufunza somo gani? (Yona 3:10) [w03 7/15 uku. 17-18]
14. Inamaanisha nini kutembea katika jina la Yehova? (Mika 4:5) [w03 8/15 uku. 17 fu. 19]
15. Katika nyakati za kisasa, Yehova alikuja katika “hekalu” lake wakati gani na jinsi gani? (Mal. 3:1-3) [re uku. 32 sanduku; jd uku. 179 fu. 3–uku. 181 fu. 6]