Matangazo
◼ Toleo la Desemba: Kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Au unaweza kutoa kitabu Mkaribie Yehova au Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 ambacho kina karatasi zinazobadilika rangi, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1991. Makutaniko ambayo hayana vitabu hivyo yanaweza kutoa kitabu Ujuzi au broshua Endeleeni Kukesha! Februari: Kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia au kitabu Ujuzi. Machi: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Ndugu aliyeteuliwa na mwangalizi-msimamizi anapaswa kukagua hesabu ya kutaniko ya miezi ya Septemba, Oktoba, na Novemba. Mtu yuleyule asitumiwe kufanya ukaguzi unaofuatana. Ukaguzi ukikamilishwa, kutaniko linapaswa kutangaziwa ripoti ya ukaguzi baada ya kusoma ripoti ya hesabu itakayofuata.—Ona Maagizo ya Kufanyia Hesabu za Kutaniko (S-27).
◼ Tungependa kuwakumbusha kwamba Ukumbusho wa mwaka wa 2009 utakuwa Alhamisi, Aprili 9, baada ya jua kushuka. Taarifa hii imetolewa mapema ili akina ndugu waweze kufanya mapatano ya kukodi majumba mengine mahali ambapo makutaniko kadhaa yanatumia Jumba moja la Ufalme. Wazee wanapaswa kufanya mapatano na wasimamizi wa jumba watakalokodi ili kuhakikisha kwamba Ukumbusho unaadhimishwa kwa njia ya amani na kwa utaratibu bila kuvurugwa na utendaji mwingine katika jengo hilo.