Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/08 uku. 7
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 1/08 uku. 7

Matangazo

◼ Toleo la Januari: Kitabu chochote cha kurasa 192 chenye karatasi inayochujuka, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1991, kinaweza kutolewa. Makutaniko ambayo hayana vitabu hivyo yanaweza kutoa kitabu Ujuzi au broshua Endeleeni Kukesha! Februari: Tutatoa kitabu Furaha ya Familia au kitabu Ujuzi. Machi: Tutatoa kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? na tutajitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tujitahidi kuwarudia watu wanaopendezwa ambao walihudhuria Ukumbusho na hotuba ya pekee lakini hawashirikiani sana na kutaniko. Lengo la ziara hizo ni kuanzisha funzo la Biblia na wale ambao hawajaanza kujifunza.

◼ Kwa kuwa mwezi wa Machi una Jumamosi na Jumapili tano, utakuwa mwezi mzuri wa kufanya upainia msaidizi.

◼ Kuanzia Februari, na kabla ya Machi 2, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa, “Unaweza Kupata Wapi Msaada Wakati wa Taabu?”

◼ Makutaniko yanapaswa kufanya mipango inayofaa ya kuadhimisha Ukumbusho wa mwaka huu siku ya Jumamosi, Machi 22, baada ya jua kushuka. Ingawa hotuba inaweza kuanza mapema, mkate na divai havipaswi kupitishwa kabla ya jua kushuka. Chunguzeni wakati ambapo jua litashuka katika eneo lenu siku hiyo. Ni afadhali kila kutaniko liadhimishe Ukumbusho likiwa peke yake. Hata hivyo, huenda hilo lisiwezekane. Mahali ambapo kwa kawaida makutaniko kadhaa hutumia Jumba moja la Ufalme, kutaniko moja linaweza kutumia Jumba la Ufalme na yale mengine yanaweza kukutanika mahali pengine jioni hiyo. Ikiwa makutaniko kadhaa yatatumia Jumba moja, ikiwezekana tunapendekeza kuwe na muda wa angalau dakika 40 kati ya programu ili wote wafaidike kikamili na ushirika baada ya Ukumbusho. Hakikisheni kuwa hakuna msongamano wa magari. Pia hakikisheni kuna mahali pa kuegesha magari na pa kushusha na kubeba abiria. Mabaraza ya wazee yanapaswa kufanya mipango inayofaa.

◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuhakikisha kwamba wana barua ya kuwekwa rasmi kwa painia (S-202) ya kila painia wa kawaida kutanikoni. Ikiwa hawana, wanapaswa kuiandikia ofisi ya tawi.

◼ Kuanzia juma la Agosti 4, 2008, tutajifunza kitabu Izingatie Siku ya Yehova Maishani katika Funzo la Kitabu la Kutaniko.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki