Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Aprili 28, 2008. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Machi 3 hadi Aprili 28, 2008.
SIFA ZA USEMI
1. Kwa nini ni muhimu kutoa hotuba tukitegemea habari ambazo tumepewa, na tunaweza kufanyaje hivyo? [be uku. 234 fu. 1–uku. 235 fu. 1]
2. Kwa nini maswali ni muhimu tunapofundisha? [be uku. 236 fu. 1-5]
3. Maswali yanawezaje kuwasaidia wasikilizaji wetu wasababu juu ya habari fulani? [be uku. 237 fu. 3–uku. 238 fu. 1]
4. Tunapofundisha, kwa nini ni muhimu kutumia maswali kwa ustadi ili kutambua hisia za moyoni za wasikilizaji? (Met. 20:5; Mt. 16:13-16; Yoh. 11:26) [be uku. 238 fu. 3-5]
5. Kuna faida gani za kutumia tashbihi tunapofundisha? (Mwa. 22:17; Yer. 13:11) [be uku. 240 fu. 1-3]
HOTUBA NA. 1
6. Kitabu cha Marko kinakazia kanuni gani zenye kuongoza ambazo zitatusaidia kupata uhai chini ya Ufalme wa Mungu? [si uku. 186 fu. 32]
7. Roho takatifu inawasaidiaje watumishi wa Mungu leo? (Yoh. 14:25, 26) [be uku. 19 fu. 2-3]
8. Ni faida gani kubwa zaidi tunayopata kwa kusoma? [be uku. 21 fu. 3]
9. Kujifunza kunatia ndani nini? [be uku. 27 fu. 3–uku. 28 fu. 1]
10. Injili ya Luka inajengaje uhakika kwamba Maandiko ya Kiebrania yamepuliziwa na Mungu? [si uku. 192 fu. 30-31]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
11. Kwa nini Yesu alimsahihisha mtu fulani aliyemwita “Mwalimu Mwema”? (Marko 10:17, 18) [w08 2/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Kitabu cha Marko”]
12. Yesu alitumia mtini kuonyesha nini kuhusu taifa la Israeli? (Marko 11:12-14, 20, 21) [w03 5/15 uku. 26 fu. 2-3]
13. Malaika Gabrieli alimaanisha nini aliposema kwamba Maria ‘atachukua mimba katika tumbo lake la uzazi’ wakati roho takatifu itakapokuja juu yake na nguvu za Mungu kumfunika? (Luka 1:30, 31, 34, 35) [w08 3/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Kitabu cha Luka”; it-2 uku. 56 fu. 2]
14. Je, wanafunzi wa Yesu walikuwa wakifanya “jambo lisilo halali katika siku ya Sabato”? (Luka 6:1, 2) [gt 31]
15. Tunaweza kupata somo gani kutokana na shauri la Yesu kwa Martha? (Luka 10:40-42) [w99 9/1 uku. 31]