Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Mei: Magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! na kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli. Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia la nyumbani kwa kutumia kitabu Mwabudu, hasa pamoja na watu ambao tayari wamejifunza kitabu Biblia Inafundisha na broshua Anataka. Juni: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Julai na Agosti: Tumia broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32: Endeleeni Kukesha!, Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?, Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?, Roho za Wafu—Je, Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je, Ziko Kweli? Serikali Itakayoleta Paradiso, “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” na broshua Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!, na broshua nyingine zozote zinazopatikana katika lugha za kienyeji.
◼ Mabaraza ya wazee yanapaswa kupitia barua ya Julai 6, 2006 kuhusu kujitayarisha kwa ajili ya misiba na wahakikishe kwamba wana anwani na namba za simu za kila mhubiri. Katika maeneo yanayokumbwa na misiba mara kwa mara, wazee wanapaswa kuwa na habari za ziada za jinsi wanavyoweza kuwasiliana na wahubiri wakati wa dharura. Mbali na hali za dharura, ingefaa wahubiri wamjulishe mwangalizi wa Funzo lao la Kitabu la Kutaniko au mzee mwingine ikiwa hawatakuwapo kwa muda mrefu, kwa mfano, wanaposafiri kwenda likizo au safari za kikazi, au ikiwa watalazwa hospitalini, au hali nyingine kama hizo.
◼ Tafadhali zingatieni kwamba hakutakuwa na karatasi za mwaliko kwa ajili ya kusanyiko la wilaya la 2008. Hata hivyo, tunapanga kuwe na kampeni kubwa ulimwenguni pote hivi karibuni. Mtapashwa habari zaidi kuhusu kampeni hiyo baadaye.