Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Julai na Agosti: Tumia broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32: Endeleeni Kukesha!, Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na broshua “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! na broshua nyingine zinazopatikana katika lugha nyinginezo. Septemba: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kitatumiwa. Fanya jitihada za pekee za kuanzisha funzo la Biblia kwenye ziara ya kwanza. Ikiwa tayari wenye nyumba wana kitabu hicho, onyesha jinsi wanavyoweza kufaidika nacho kwa kuwaonyesha kwa ufupi jinsi funzo la Biblia linavyoongozwa. Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mtu akipendezwa, mpe na uzungumzie trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? ukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Kwa kuwa mwezi wa Agosti una Jumamosi tano na Jumapili tano, utakuwa mwezi mzuri wa kufanya upainia msaidizi.
◼ Kuanzia Septemba, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Kutembea Katika Njia ya Utimilifu.”
◼ Ofisi ya tawi haishughulikii maagizo ya vichapo ya mhubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi-msimamizi anapaswa kupanga ili tangazo litolewe kila mwezi kabla ya agizo la kila mwezi la kutaniko kutumwa kwenye ofisi ya tawi ili wote ambao wanataka kuagiza kichapo fulani waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia vichapo. Tafadhali kumbukeni vichapo ambavyo ni vya ombi la pekee.
◼ Kitabu Biblia Inafundisha kinapaswa kutumiwa kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia badala ya broshua Anataka. Broshua Anataka inaweza kuendelea kugawanywa katika huduma ya shambani hadi nakala zote zilizo akibani zitakapokwisha.