Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Septemba: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kitatumiwa. Fanya jitihada ya pekee ya kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Ikiwa tayari wenye nyumba wana kitabu hicho, waeleze jinsi wanavyoweza kufaidika kwa kuwaonyesha kwa ufupi jinsi wanavyoweza kujifunza Biblia. Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ikiwa mtu anapendezwa, mwonyeshe trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? na uizungumzie ukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia. Novemba: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Unaweza pia kuwaachia watu kitabu Ujuzi ili wajisomee. Desemba: Kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Watu wakisema kwamba wana watoto, waachie kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu.
◼ Kwa kuwa mwezi wa Novemba una Jumamosi tano na Jumapili tano, utakuwa mwezi mzuri wa kufanya upainia msaidizi.
◼ Hotuba ya pekee ya watu wote ya majira ya Ukumbusho ya 2009 itatolewa juma la Aprili 20, 2009. Kichwa cha hotuba hiyo kitatangazwa baadaye. Makutaniko ambayo yatakuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko au kusanyiko mwishoni mwa juma hilo yatakuwa na hotuba ya pekee juma linalofuata. Hakuna kutaniko linalopaswa kuwa na hotuba ya pekee kabla ya Aprili 20.
◼ Katika ombi linalofuata la vitabu, makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza mabuku yaliyojalidiwa ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ya 2008, Fahirisi ya 2008, na Watchtower Library−2008 Edition kwenye CD-ROM. Orodha ya lugha ambazo vifaa hivyo vitapatikana itaonyeshwa katika “Tangazo kwa Makutaniko Yote,” linalotumwa kila mwezi. Tafadhali kumbukeni kwamba Watchtower Library−2008 Edition inatayarishwa kwa ajili tu ya wahubiri ambao wamebatizwa na wahubiri wa kutaniko ambao hawajabatizwa na inaweza kuagizwa tu kupitia kutaniko. Wahubiri ambao wanatumia sana Watchtower Library na hawatumii tena mabuku yaliyojalidiwa wanapaswa kufikiria ikiwa kuna haja ya kuagiza mabuku hayo.
◼ Ndugu fulani aliyeteuliwa na mwangalizi-msimamizi anapaswa kukagua hesabu za kutaniko za miezi ya Juni, Julai, na Agosti. Mtu yuleyule asitumiwe kufanya ukaguzi unaofuatana. Ukaguzi ukikamilishwa, kutaniko linapaswa kutangaziwa ripoti ya ukaguzi baada ya ripoti ya hesabu itakayofuata kusomwa.—Ona Maagizo ya Kufanyia Hesabu za Kutaniko (S-27).