Matangazo
◼Toleo la mwezi wa Novemba: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidini sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Kitabu Ujuzi kinaweza kutolewa kwa ajili ya usomaji wa kibinafsi. Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ikiwa watu wanasema kwamba wana watoto, watoleeni kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Januari: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa tayari wenye nyumba wana kitabu hicho, wahubiri wanaweza kuwatolea kitabu chochote cha kurasa 192 chenye karatasi zinazobadilika rangi, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1992. Februari: Toeni kitabu kimoja kati ya vitabu vifuatavyo ikiwa vinapatikana, Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Je, Kuna Muumba Anayekujali?, au Siri ya Kupata Furaha ya Familia.
◼ Wahubiri wote wanahimizwa wajaze kadi ya mamlaka ya kudumu ya uwakilishi (DPA), au kadi ya mwelekezo wa mapema kuhusu tiba/ondoleo la hatia (AMD), ikiwa hawajafanya hivyo. Kadi hiyo ya DPA, au ya AMD, inalinda haki yako ya kukataa kutiwa damu. Wazee watamsaidia mtu mmoja-mmoja kulingana na uhitaji.—Ona nyongeza katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 2006.
◼ Kuanzia Januari 1, 2009, jina “mwangalizi msimamizi” halitatumiwa tena. Sasa mwangalizi msimamizi ataitwa “mratibu wa baraza la wazee.”
◼ Vitabu na magazeti yote yaliyopo yahesabiwe Desemba 31, 2008, au haraka iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Hesabu hiyo ni kama ile inayofanywa kila mwezi na mratibu wa vitabu. Jumla zote ziandikwe kwenye fomu ya Orodha ya Vitabu (S-18). Jumla ya idadi ya magazeti yaliyopo inaweza kupatikana kutoka kwa mtumishi (au watumishi) wa magazeti. Mwandishi wa kutaniko linaloratibu anapaswa kusimamia kazi hiyo. Mwandishi na mwangalizi-msimamizi wa kutaniko linaloratibu watie sahihi fomu hiyo. Kila kutaniko linaloratibu litapokea nakala tatu za fomu ya Orodha ya Vitabu (S-18). Tafadhali tumeni nakala ya kwanza kwenye ofisi ya tawi kabla ya Januari 6. Wekeni nakala ya pili kwenye faili zenu. Nakala ya tatu inaweza kutumiwa kufanyia hesabu.