Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Aprili 27, 2009. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 20 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Machi 2 hadi Aprili 27, 2009.
1. Yosefu alikabilianaje na kishawishi cha kila siku kutoka kwa mtu aliyekuwa karibu? (Mwa. 39:7-12) [lv uku. 105 fu. 18–uku. 106 fu. 20]
2. Biblia ina maoni gani kuhusu sikukuu za kuzaliwa? (Mwa. 40:20-22) [lv uku. 150 fu. 9–uku. 151 fu. 11]
3. Ni katika njia gani Yosefu ni mfano mzuri wa kuwasamehe wale ambao wametenda dhambi dhidi yetu? (Mwa. 45:4, 5) [w99 1/1 uku. 31 fu. 2-3]
4. Maneno ya Yosefu: “Mwichukue mifupa yangu kutoka huku,” yalikuwa na matokeo gani? (Mwa. 50:25) [w07 6/1 uku. 28 fu. 10]
5. Ni nini kinachoweza kutupa uhakika tunapopata mgawo mgumu? (Kut. 4:10, 13) [w04 3/15 uku. 25 fu. 5]
6. Ni mambo gani yaliyotokana na jinsi Yehova alivyoshughulika na Farao, na matukio hayo yanapaswa kuwa na matokeo gani juu yetu? (Kut. 9:13-16) [w05 5/15 uku. 21 fu. 8]
7. Andiko la Kutoka 14:30, 31 lina maana gani kwetu leo? [w04 3/15 uku. 26 fu. 5]
8. Kama andiko la Kutoka 16:1-3 linavyoonyesha, kuna hatari gani za kulalamika? [w93 3/15 uku. 21 fu. 1–3]
9. Kupatana na matakwa ya Agano la Sheria yanayotajwa katika andiko la Kutoka 19:5, 6, ni kwa kadiri gani Israeli la kale lilikuwa “ufalme wa makuhani na taifa takatifu”? [w95 7/1 uku. 16 fu. 8]
10. Ni katika njia gani amri ya kumi kuhusu kutamani ni bora kuliko sheria za wanadamu? (Kut. 20:17) [w06 6/15 uku. 23-24 fu. 16]