Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Septemba: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki na hakubali funzo la Biblia, mhubiri anaweza kumwachia magazeti yoyote ya zamani au broshua yoyote inayomfaa. Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mtu akipendezwa, zungumzia trakti Je, ungependa Kujua Ukweli? na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Novemba: Biblia—Ina Ujumbe Gani? Vilevile, pamoja na broshua hiyo au badala yake, makutaniko yaweza kuamua kutoa yoyote kati ya broshua zilizokuwa toleo la Agosti 2011. Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ikiwa kuna watoto katika familia, kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu au Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia kinaweza kutolewa.
◼ Hotuba ya pekee ya watu wote katika majira ya Ukumbusho mwaka wa 2012 itatolewa juma linaloanza Aprili 2. Kichwa cha hotuba hiyo kitatangazwa baadaye. Hakuna kutaniko linalopaswa kuwa na hotuba ya pekee kabla ya Ukumbusho.
◼ Wahubiri watakaofanya upainia msaidizi mwezi wa Machi 2012 wanaweza kutimiza takwa la saa 30 au 50 mwezi huo. Isitoshe, ikiwa mwangalizi wa mzunguko anatembelea kutaniko mwezi huo, mapainia wasaidizi wote, iwe wanatimiza takwa la saa 30 au 50, wanaalikwa kuhudhuria kipindi chote cha mkutano ambao mwangalizi wa mzunguko atafanya pamoja na mapainia wa kawaida.
◼ Kuanzia mwezi wa Septemba, waangalizi wa mzunguko walianza kutoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Ungana Pamoja na Watu wa Mungu Wenye Furaha.”