Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Septemba na Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapofanya ziara za kurudia, tumia kitabu Biblia Inafundisha au ikitegemea hali, mojawapo ya broshua, Msikilize Mungu au Msikilize Mungu Uishi Milele, na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Novemba na Desemba: Wahubiri wanaweza kutoa mojawapo ya trakti zifuatazo: Je, Una Roho Isiyoweza Kufa?, Je! Ulimwengu Huu Utaokoka?, Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa?, Kuteseka Kote Kutaisha Karibuni!, Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini?, Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani, na Yehova—Yeye Ni Nani? Ikiwa kuna upendezi, onyesha jinsi funzo la Biblia linavyofanywa ukitumia kitabu Biblia Inafundisha au mojawapo ya broshua Msikilize Mungu au Msikilize Mungu Uishi Milele.
◼ Hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho ya mwaka wa 2013 itatolewa katika juma la Aprili 1. Kichwa cha hotuba hiyo kitatangazwa baadaye. Makutaniko yaliyo na ziara ya mwangalizi wa mzunguko au kusanyiko mwishoni mwa juma hilo, yatakuwa na hotuba ya pekee juma linalofuata. Hotuba hiyo haipaswi kutolewa katika kutaniko lolote kabla ya Aprili 1.