Habari Kuu za Utumishi
Uganda: Kilele kipya cha wahubiri kilifikiwa katika mwezi wa Julai wahubiri 5,859 walipotoa ripoti zao za utumishi wa shambani. Hilo ni ongezeko lenye kutia moyo la asilimia 10 ikilinganishwa na mwezi wa Julai mwaka uliotangulia. Hiki ni kilele kipya cha nne cha wahubiri kilichofikiwa katika mwaka huo wa utumishi. Pia, kulikuwa na kilele kipya cha magazeti 100,991 yaliyotolewa katika utumishi wa shambani. Kwa wastani kila mhubiri wa kutaniko alihubiri saa 14.1 mwezi wa Julai.