Matangazo
◼ Toleo la machapisho la mwezi wa Januari na Februari: Wahubiri wanaweza kutoa yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je, Kweli Mungu Anatujali?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Mungu Anataka Tufanye Nini?, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je Ziko Kweli?, Serikali Itakayoleta Paradiso, Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!, Lasting Peace and Happiness—How to Find Them, au Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? Unapofanya ziara za kurudia, tumia kitabu Biblia Inafundisha au ikitegemea hali za yule unayezungumza naye, mojawapo ya broshua, Msikilize Mungu au Msikilize Mungu Uishi Milele, na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Machi na Aprili: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapofanya ziara za kurudia, tumia kitabu Biblia Inafundisha au ikitegemea hali za yule unayezungumza naye, mojawapo ya broshua, Msikilize Mungu au Msikilize Mungu Uishi Milele, na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Kichwa cha hotuba ya watu wote itakayotolewa na mwangalizi wa mzunguko katika nusu ya pili ya mwaka wa utumishi wa 2013 ni “Habari Njema . . . kwa Kila Taifa na Kabila na Lugha.”