Habari Kuu za Utumishi
Sudan: Ripoti ya kila mwaka ya mwaka wa 2012 ilikuwa yenye kutia moyo kwa kuwa ilionyesha kwamba kulikuwa na wahubiri 511 nchini humo, watu 1,569 walihudhuria Ukumbusho na 19 walibatizwa.
Sudan Kusini: Ripoti ya kila mwaka ya mwaka wa 2012 ilionyesha kwamba kulikuwa na jumla ya wahubiri 1,174 na watu 4,678 walihudhuria Ukumbusho na 66 walibatizwa mwaka huo. Kwa kweli hiyo ni ripoti nzuri sana kutoka Sudan Kusini.
Uganda: Katika mwezi wa Novemba jumla ya wahubiri 5,606 waliongoza mafunzo ya Biblia 15,144. Hilo ni ongezeko la asilimia 8 la wahubiri na ongezeko la asilimia 10 zaidi ya mafunzo ya Biblia ikilinganishwa na mwezi uo huo mwaka uliotangulia. Kwa kweli, watu wa Yehova wana shughuli nyingi sana katika kazi hii ya kufundisha inayookoa uhai!—1 Tim. 4:16.