Habari Kuu za Utumishi
Kenya: Katika mwezi wa Julai kulikuwa na kilele kipya cha mafunzo ya Biblia 46,565.
Kwenye Kusanyiko la Eneo lililofanywa Kisumu kwa lugha ya Kijaluo mwezi wa Agosti, Biblia Takatifu Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ilitolewa na Ndugu Stephen Lett wa Baraza Linaloongoza mbele ya wahudhuriaji wenye shangwe 2,400 hivi. Makusanyiko mengine yaliyokuwa yakifanywa wakati huo yaliunganishwa kupitia mfumo wa sauti na kufanya jumla ya wahudhuriaji kuwa zaidi ya 14,000.
Sudan: Ripoti ya mwezi wa Julai ilionyesha ongezeko la asilimia 23 ya idadi ya wahubiri ukilinganisha na wastani wa mwaka uliopita.