HAZINA ZA NENO LA MUNGU | EZRA 6-10
Yehova Hupenda Watumishi Wanaojitolea kwa Hiari
Ezra alifanya matayarisho ya kurudi Yerusalemu
Ezra anaruhusiwa na Mfalme Artashasta kurudi Yerusalemu ili kuendeleza ibada ya Yehova
Mfalme anampa Ezra “maombi yake yote” kwa ajili ya nyumba ya Yehova—dhahabu, fedha, ngano, divai, mafuta, na chumvi, ambavyo kulingana na makadirio ya sasa vyote vingegharimu zaidi ya dola 100,000,000 za Marekani
Ezra aliamini kwamba Yehova atawalinda watumishi Wake
Haingekuwa rahisi kurudi Yerusalemu
Huenda safari ilikuwa na umbali wa kilometa 1,600 na eneo hilo lilikuwa hatari
Walisafiri kwa miezi minne hivi
Wale waliorudi walihitaji imani yenye nguvu, bidii kwa ajili ya ibada ya kweli, na ujasiri
ALIPOSAFIRI EZRA ALIBEBA . . .
Dhahabu na fedha zenye uzito wa talanta 750, uzani unaolingana na uzito wa ndovu watatu hivi wakomavu!
HALI NGUMU WALIZOKABILI WAISRAELI WALIORUDI . . .
Vikundi vya waporaji, jangwa, wanyama-mwitu hatari