HAZINA ZA NENO LA MUNGU | METHALI 7-11
“Moyo Wako Usikengeuke”
Viwango vya Yehova vinaweza kutulinda. Hata hivyo, ili tufaidike navyo, ni lazima tuvithamini na kuviingiza mioyoni mwetu. (Met 7:3) Mtumishi wa Yehova anaporuhusu moyo wake ukengeushwe, anaweza kunaswa kwa urahisi na mbinu zenye ujanja na zenye udanganyifu za Shetani. Methali sura ya 7 inaeleza kuhusu kijana ambaye aliruhusu moyo wake umkengeushe. Tunaweza kujifunza nini kutokana na makosa yake?
Shetani hutushawishi tufanye dhambi kwa kutumia hisi zetu tano akijaribu kutuondoa kwa Yehova
Hekima na uelewaji utatusaidia kutambua madhara ya kufanya dhambi na kuepuka kujihatarisha kiroho