Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb20 Aprili uku. 7
  • “Ondoeni Kabisa Miungu ya Kigeni”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Ondoeni Kabisa Miungu ya Kigeni”
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Kuwasiliana na Pepo Kuna Madhara?
    Vijana Huuliza
  • Kubali Msaada wa Yehova wa Kuwapinga Roho Waovu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Kuwasiliana na Pepo?
    Amkeni!—2017
  • Mwabudu Yehova Peke Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
mwb20 Aprili uku. 7
A man throwing away a beaded necklace related to spiritism.

MAISHA YA MKRISTO

“Ondoeni Kabisa Miungu ya Kigeni”

Yakobo alijua kwamba Yehova tu ndiye anayestahili kuabudiwa, hata ingawa Yehova hakuwa ametoa sheria inayopinga ibada ya sanamu. (Kut 20:3-5) Kwa hiyo, baada ya Yehova kumwambia arudi Betheli, Yakobo alimwagiza kila mtu aliyekuwa pamoja naye aondoe kabisa miungu ya kigeni. Kisha Yakobo akatupa sanamu hizo, kutia ndani vipuli, ambavyo huenda vilivaliwa kama hirizi. (Mwa 35:1-4) Bila shaka, Yehova alipendezwa na jambo ambalo Yakobo alifanya.

Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunamwabudu Yehova peke yake? Jambo moja muhimu ni kuepuka chochote kinachohusiana na ibada ya sanamu au kuwasiliana na roho. Huenda hilo likatia ndani kuondoa vitu vyovyote vinavyohusiana na uchawi na kuchunguza burudani yetu kwa makini. Kwa mfano, jiulize: ‘Je, mimi hujiburudisha kwa kusoma vitabu au kutazama sinema zinazoonyesha vitu kama watu wanaonyonya damu, mazimwi, au mambo yanayopita uwezo wa kibinadamu? Je, burudani yangu inaonyesha kwamba mazingaombwe, uchawi, au laana ni vitumbuizo visivyo na madhara?’ Tunapaswa kuepuka kabisa kitu chochote kinachomchukiza Yehova.—Zb 97:10.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA “MPINGENI IBILISI,” KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Mtoto akiwa amelala kitandani, akiwa na hirizi mkononi. Nyuma, mama ya mtoto huyo, ambaye ni funzo la Biblia, anazungumza na wenzi wa ndoa wanaojifunza Biblia pamoja naye.

    Ni tatizo gani lililotokea katika maisha ya mwanafunzi wa Biblia anayeitwa Palesa?

  • Wenzi hao wa ndoa pamoja na mwanafunzi wa Biblia wakikutana na wazee wawili na kupata msaada.

    Kwa nini ni jambo la hekima kutafuta msaada wa wazee katika visa vinavyohusisha kuwasiliana na roho?

  • Mwanafunzi wa Biblia akichoma hirizi ya mtoto jikoni.

    Mpingeni Ibilisi, na umkaribie Mungu.​—Yak 4:7, 8

    Ikiwa tunataka kupata ulinzi wa Yehova, ni mambo gani tunayopaswa kuacha kabisa?

  • Palesa alichukua hatua gani muhimu?

  • Ni njia zipi za kuepuka uvutano wa Ibilisi katika eneo unaloishi?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki