Novemba 2-8
KUTOKA 39-40
Wimbo 89 na Sala
Utangulizi (Dak. 1)
HAZINA ZA NENO LA MUNGU
“Musa Alifuata Maagizo kwa Makini”: (Dak. 10)
Kut 39:32—Musa alifuata kwa makini maagizo ya Yehova kuhusu ujenzi wa hema la ibada (w11 9/15 27 ¶13)a
Kut 39:43—Musa mwenyewe alikagua hema la ibada ujenzi ulipokamilika
Kut 40:1, 2, 16—Musa alisimamisha hema la ibada kulingana na maagizo aliyopewa na Yehova (w05 7/15 27 ¶3)
Kutafuta Hazina za Kiroho: (Dak. 10)
Kut 39:34—Waisraeli walifauluje kupata ngozi za sili kwa ajili ya ujenzi wa hema la mkutano? (it-2 884 ¶3, 4)
Kut 40:34—Ni nini kilichomaanishwa na tendo la wingu kuanza kufunika hema la mkutano? (w15 7/15 21 ¶1)
Umepata hazina gani za kiroho katika usomaji wa Biblia wa juma hili kumhusu Yehova Mungu, au ambazo ungependa kutumia katika utumishi wa shambani, au jambo lingine?
Usomaji wa Biblia: (Usizidi dak. 4) Kut 39:1-21 (th somo la 5)
BORESHA HUDUMA YAKO
Video ya Ziara ya Kwanza: (Dak. 4) Mazungumzo. Onyesha video. Simamisha video kila mara kunapokuwa na kituo, kisha uwaulize wasikilizaji maswali yanayojitokeza kwenye video. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi tunavyoweza kuepuka kuunga mkono upande wowote mwenye-nyumba anapotaka kuzungumzia mambo ya kisiasa au masuala yenye utata katika jamii.
Ziara ya Kwanza: (Isizidi dak. 3) Tumia pendekezo la kuanzisha mazungumzo. Jibu swali la mwenye-nyumba anayeuliza maoni yako kuhusu mgombeaji fulani wa kisiasa au suala fulani la kisiasa. (th somo la 12)
Hotuba: (Isizidi dak. 5) w16.04 29 ¶8-10—Kichwa: Tunaweza Kuepukaje Kuunga Mkono Upande Wowote Katika Mazungumzo na Katika Akili Zetu? (th somo la 14)
MAISHA YA MKRISTO
Sikiliza kwa Uelewaji (Mt 13:16): (Dak. 15) Onyesha video. Kisha uliza maswali yafuatayo: Kwa nini tunahitaji kusikiliza kwa uelewaji? Ni nini maana ya Marko 4:23, 24? Tunaweza kutoa mfano gani ili kuelewa Waebrania 2:1? Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunasikiliza kwa uelewaji?
Funzo la Biblia la Kutaniko: (Lisizidi dak. 30) jy sura ya 139
Umalizio (Usizidi dak. 3)
Wimbo 139 na Sala
a Ufupisho wa Machapisho: wp = Mnara wa Mlinzi—Toleo la Watu Wote; bhs = Biblia Inatufundisha Nini?; w = Mnara wa Mlinzi; it = Insight On the Scriptures; jy = Yesu—Njia, Kweli, na Uzima; lvs = Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu; rr = Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!; si = “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”