Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb22 Machi uku. 5
  • Njia Tatu za Kumtegemea Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Njia Tatu za Kumtegemea Yehova
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2022
  • Habari Zinazolingana
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Mkaribie Mungu Kupitia Sala
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Ni Nini Kinachokuongoza Unapofanya Maamuzi ya Kibinafsi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Fanya Maamuzi Ambayo Yanamletea Mungu Heshima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2022
mwb22 Machi uku. 5

MAISHA YA MKRISTO

Njia Tatu za Kumtegemea Yehova

Daudi alimshinda Goliathi kwa sababu alimtegemea Yehova. (1Sa 17:45) Yehova anataka kudhihirisha nguvu zake kwa niaba ya watumishi wake wote. (2Nya 16:9) Tunaweza kutegemeaje msaada ambao Yehova anatoa badala ya kutegemea uzoefu na uwezo wetu wenyewe? Zifuatazo ni njia tatu:

  • Sali mara nyingi. Usisali tu ili usamehewe baada ya kufanya kosa, bali pia sali upate nguvu unapokabili jaribu. (Mt 6:12, 13) Usisali tu kwamba Yehova abariki maamuzi ambayo tayari umefanya, bali pia sali upate mwongozo na hekima kabla ya kufanya maamuzi.—Yak 1:5

  • Uwe na ratiba ya kusoma na kujifunza Biblia. Soma Biblia kila siku. (Zb 1:2) Tafakari mifano ya Biblia, na utumie mambo uliyojifunza. (Yak 1:23-25) Jitayarishe kwa ajili ya huduma badala ya kutegemea uzoefu wako. Jifunze mapema habari itakayozungumziwa katika mikutano ya kutaniko ili unufaike kikamili

  • Shirikiana na tengenezo la Yehova. Jifahamishe na miongozo ya karibuni zaidi ya tengenezo, kisha utende haraka kupatana nayo. (Hes 9:17) Wasikilize wazee wanapotoa mashauri na maagizo.​—Ebr 13:17.

Polisi wakimpeleka ndugu kizuizini huku waandishi wa habari na ndugu wengine wakitazama.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA HATUHITAJI KUOGOPA MATESO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

• Ni mambo gani yenye kuogopesha ambayo ndugu na dada walikabili?

• Ni nini kilichowasaidia kushinda woga wao?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki