MAISHA YA MKRISTO
Njia Tatu za Kumtegemea Yehova
Daudi alimshinda Goliathi kwa sababu alimtegemea Yehova. (1Sa 17:45) Yehova anataka kudhihirisha nguvu zake kwa niaba ya watumishi wake wote. (2Nya 16:9) Tunaweza kutegemeaje msaada ambao Yehova anatoa badala ya kutegemea uzoefu na uwezo wetu wenyewe? Zifuatazo ni njia tatu:
Sali mara nyingi. Usisali tu ili usamehewe baada ya kufanya kosa, bali pia sali upate nguvu unapokabili jaribu. (Mt 6:12, 13) Usisali tu kwamba Yehova abariki maamuzi ambayo tayari umefanya, bali pia sali upate mwongozo na hekima kabla ya kufanya maamuzi.—Yak 1:5
Uwe na ratiba ya kusoma na kujifunza Biblia. Soma Biblia kila siku. (Zb 1:2) Tafakari mifano ya Biblia, na utumie mambo uliyojifunza. (Yak 1:23-25) Jitayarishe kwa ajili ya huduma badala ya kutegemea uzoefu wako. Jifunze mapema habari itakayozungumziwa katika mikutano ya kutaniko ili unufaike kikamili
Shirikiana na tengenezo la Yehova. Jifahamishe na miongozo ya karibuni zaidi ya tengenezo, kisha utende haraka kupatana nayo. (Hes 9:17) Wasikilize wazee wanapotoa mashauri na maagizo.—Ebr 13:17.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA HATUHITAJI KUOGOPA MATESO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
• Ni mambo gani yenye kuogopesha ambayo ndugu na dada walikabili?
• Ni nini kilichowasaidia kushinda woga wao?