Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb23 Septemba uku. 7
  • Wachungaji Wanaowanufaisha Watu wa Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wachungaji Wanaowanufaisha Watu wa Yehova
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2023
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kuwaonyesha Watenda Dhambi Upendo na Rehema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
  • Akina Ndugu—Je, Mnajitahidi Kustahili Kutumikia Mkiwa Wazee wa Kutaniko?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
  • Maamuzi Yanayoonyesha Unamtegemea Yehova
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2023
  • Kumbuka Kwamba Yehova Ndiye “Mungu Aliye Hai”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2023
mwb23 Septemba uku. 7

MAISHA YA MKRISTO

Wachungaji Wanaowanufaisha Watu wa Yehova

Watu wengi wana maoni yasiyofaa kuhusu watu wenye mamlaka. Inaeleweka kwa nini wana maoni hayo. Kwa muda mrefu wanadamu wametumia mamlaka yao kwa njia mbaya ili kujinufaisha wenyewe. (Mik 7:3) Tunashukuru sana kwamba wazee katika kutaniko wamezoezwa kutumia mamlaka yao kuwanufaisha watu wa Yehova.—Est 10:3; Mt 20:​25, 26.

Tofauti na watu wenye mamlaka katika ulimwengu huu, wazee hujitahidi kufikia mapendeleo kwa sababu wanampenda Yehova na watu wake. (Yoh 21:16; 1Pe 5:​1-3) Chini ya mwongozo wa Yesu, wachungaji hao wanawasaidia wahubiri wote kuhisi wao ni sehemu ya familia ya Yehova na kuendelea kukaa karibu na Yehova. Wanatenda upesi ili kutoa msaada wa kiroho kwa kondoo wa Yehova na kusaidia kunapokuwa na dharura ya kitiba au janga linapotokea. Ikiwa unahitaji msaada, kwa nini usichukue hatua ya kwanza kuwasiliana na mzee katika kutaniko lako?—Yak 5:14.

Picha kutoka kwenye video “Wachungaji Wanaotunza Kundi.” Mzee akimkumbatia Elias kwa furaha wanaposalimiana.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA WACHUNGAJI WANAOTUNZA KUNDI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Mariana alinufaikaje kutokana na msaada aliopata kutoka kwa wazee?

  • Elias alinufaikaje kutokana na msaada aliopata kutoka kwa wazee?

  • Masimulizi uliyotazama yanakufanya uhisije kuhusu kazi ya wazee?

Chukua hatua ya kwanza kuwasiliana na mzee . . .

  • ikiwa umebadili namba ya simu au anwani

  • ikiwa unakabiliana na jaribu gumu

  • ikiwa utasafiri kwa muda mrefu

  • ikiwa unakabili tatizo la afya au utalazwa hospitalini

  • ikiwa umetenda dhambi nzito

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki