MACHI 4-10
ZABURI 16-17
Wimbo 111 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
1. “Yehova, Chanzo Changu cha Wema”
(Dak. 10)
Tukichagua marafiki wanaomtumikia Yehova tutakuwa na furaha (Zb 16:2, 3; w18.12 26 ¶11)
Tunapata uradhi tunapojua tuna uhusiano mzuri pamoja na Yehova (Zb 16:5, 6; w14 2/15 29 ¶4)
Yehova anatulinda kiroho na hilo linatufanya tuhisi tukiwa salama (Zb 16:8, 9; w08 2/15 3 ¶2-3)
Tuna maisha yenye kusudi kama aliyokuwa nayo Daudi kwa sababu jambo kuu maishani mwetu ni kumwabudu Yehova, Chanzo chetu cha wema.
JIULIZE, ‘Nimepata faida gani maishani baada ya kujifunza kweli?’
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Zb 17:1-15 (th somo la 5)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 1) NYUMBA KWA NYUMBA. Toa mwaliko wa Ukumbusho. (th somo la 11)
5. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Toa mwaliko wa Ukumbusho. Mtu anapoonyesha upendezi, toa utangulizi wa video Kumbuka Kifo cha Yesu kisha mzungumze kuihusu. (th somo la 9)
6. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 2) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Toa mwaliko wa Ukumbusho. (th somo la 2)
7. Kufanya Wanafunzi
Wimbo 20
8. Tunaweza Kufanya Nini Ili Kujitayarisha kwa Ajili ya Ukumbusho?
(Dak. 15) Mazungumzo.
Yesu alituamuru tukumbuke kifo chake. Kwa hiyo, Jumapili, Machi 24, tutaadhimisha kifo cha Yesu, ambacho kilihusisha maonyesho mawili makuu ya upendo katika historia. (Lu 22:19; Yoh 3:16; 15:13) Unaweza kufanya nini ili kujitayarisha kwa ajili ya tukio hilo muhimu?
Shiriki kwa bidii katika kampeni ya kuwaalika watu kwenye hotuba ya pekee na Ukumbusho. Andika orodha ya watu ambao ungependa kuwaalika na uwaalike. Ikiwa baadhi ya watu hao hawaishi katika eneo lenu, angalia mapema kwenye jw.org muda na mahali ambapo mikutano inafanywa katika eneo lao
Jitahidi kuongeza utumishi wako katika mwezi wa Machi na Aprili. Unaweza kuwa painia msaidizi na kuchagua takwa la saa 15 au 30
Usomaji wa Biblia wa juma la mwisho la maisha ya Yesu duniani utaanza Machi 18, basi tunakuhimiza kuanza usomaji huo siku hiyohiyo. Unaweza kuamua kiasi cha habari utakachosoma kila siku ukifuata “Ratiba ya Usomaji wa Biblia wa Ukumbusho wa 2024” kwenye ukurasa wa 6-7
Siku ya Ukumbusho, tazama Ibada ya Asubuhi ya Ukumbusho inayopatikana kwenye jw.org
Kabla na baada ya programu ya Ukumbusho, wakaribishe kwa uchangamfu wageni na pia ndugu na dada wasiotenda. Waambie kwamba uko tayari kujibu maswali yoyote waliyo nayo. Fanya mipango ya kuwatembelea wale waliohudhuria ili kuendeleza mazungumzo
Tafakari kuhusu fidia kabla na pia baada ya Ukumbusho
Onyesha VIDEO Kumbuka Kifo cha Yesu. Kisha waulize wasikilizaji:
Tunaweza kuitumiaje video hii katika kampeni ya Ukumbusho?
9. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) bt sura ya 6 ¶18-24, sanduku uk. 48