Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb25 Januari kur. 14-15
  • Februari 24–Machi 2

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Februari 24–Machi 2
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2025
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2025
mwb25 Januari kur. 14-15

FEBRUARI 24–MACHI 2

METHALI 2

Wimbo 35 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Kwa Nini Uwe na Hamu kwa Ajili ya Funzo Lako la Kibinafsi?

(Dak. 10)

Ili uonyeshe unaithamini kweli (Met 2:​3, 4; w22.08 18 ¶16)

Ili likusaidie kufanya maamuzi mazuri (Met 2:​5-7; w22.10 19 ¶3-4)

Ili uimarishe imani yako (Met 2:​11, 12; w16.09 23 ¶2-3)

Mwanamume Mwisraeli akitumia sururu ndani ya pango.

JIULIZE, ‘Ninaweza kuboreshaje ratiba yangu ya funzo la kibinafsi?’

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Met 2:7—Ni katika njia gani Yehova ni “ngao kwa wanaotembea kwa utimilifu”? (it-1 1211 ¶4)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Met 2:​1-22 (th somo la 12)

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwonyeshe mwenye nyumba jinsi ya kupata habari kwenye jw.org ambazo zinaweza kuwasaidia wenzi wa ndoa. (lmd somo la 1 jambo kuu la 3)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 3) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mtolee mtu huyo gazeti linalohusu habari ambayo alipendezwa nayo wakati uliopita. (lmd somo la 9 jambo kuu la 3)

6. Hotuba

(Dak. 5) lmd nyongeza A jambo kuu la 8—Kichwa: Mume na mke wanapaswa kuwa waaminifu. (th somo la 13)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 96

7. Je, Wewe Ni Mtafutaji wa Hazina?

(Dak. 15) Mazungumzo.

Vijana, je, wazo la kutafuta hazina linawavutia? Ikiwa ndivyo, Biblia inakualika utafute hazina yenye thamani zaidi ulimwenguni, yaani, ujuzi kumhusu Mungu. (Met 2:​4, 5) Unaweza kupata hazina hiyo kwa kutenga wakati kusoma Biblia kwa ukawaida na kwa kuchimba ndani ya masimulizi unayosoma. Kufanya hivyo kunaweza kufurahisha na kuthawabisha!

  • Unaweza kujiuliza maswali gani unaposoma Biblia? (w24.02 32 ¶2-3)

  • Ni vifaa gani ambavyo unaweza kutumia ili kupata majibu?

Mvulana aliyevalia mavazi kama ya wavumbuzi, akifungua sanduku lililojaa hazina.

Mfululizo wa video wenye kichwa Jifunze Kutoka kwa Rafiki za Yehova unaweza kukusaidia kujifunza jinsi ya kutafakari mambo uliyosoma katika Biblia.

Mvulana akifanya funzo la kibinafsi la Biblia. Broshua “Uhai​—⁠Ulitokana na Muumba? ” iko mezani.

Onyesha VIDEO Jifunze Kutoka kwa Rafiki za Yehova—Abeli.

Soma Mwanzo 4:​2-4 na Waebrania 11:4. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Abeli alionyeshaje kwamba alikuwa rafiki ya Yehova?

  • Abeli alisitawishaje imani yake katika Yehova?

  • Wewe unaweza kufanya nini usitawishe imani yako?

DOKEZO

Unaposoma Biblia, fanya utafiti kuhusu watu, maeneo, na vitu unavyosoma kuvihusu, hata ikiwa unafikiri unafahamu mambo hayo vizuri. Unapojifunza Biblia kwa njia hiyo, mambo unayosoma yanakuwa halisi kwako!

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

(Dak. 30) bt sura ya 23 ¶1-8 na utangulizi wa sehemu ya 8

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 102 na Sala

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki