DOKEZO LA KUJIFUNZA
Tayarisha Moyo Wako
Tunapojifunza Biblia, tunataka mawazo ya Yehova yaguse moyo wetu au utu wetu wa ndani. Ezra aliweka mfano mzuri kuhusu jambo hilo, ‘alipoutayarisha moyo wake kuichunguza Sheria ya Yehova.’ (Ezra 7:10) Tunawezaje kuutayarisha moyo wetu?
Sali. Anza kila kipindi cha kujifunza kwa sala. Mwombe Yehova akusaidie uelewe na kutumia mambo unayojifunza.—Zab. 119:18, 34.
Uwe mnyenyekevu. Mungu huwaficha kweli watu wenye kiburi na wanaofikiri kwamba hawahitaji msaada wake ili kuielewa Biblia. (Luka 10:21) Tunapofanya utafiti, kusudi letu si kuwaonyesha wengine kwamba tunajua mambo mengi. Kwa unyenyekevu, badili njia yako ya kufikiri ikiwa haipatani na njia ya Mungu ya kufikiri.
Sikiliza wimbo wa Ufalme. Muziki una nguvu za kugusa moyo wetu, unatutayarisha kwa ajili ya ibada. Kusikiliza wimbo wa Ufalme kabla ya kuanza kipindi cha kujifunza huenda kukakusaidia kutayarisha moyo wako.