Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb15 uku. 162-uku. 163 fu. 2
  • “Watu Ishirini na Wawili Waliliacha Kanisa”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Watu Ishirini na Wawili Waliliacha Kanisa”
  • 2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb15 uku. 162-uku. 163 fu. 2
Picha katika ukurasa wa 162

JAMHURI YA DOMINIKA

Watu Ishirini na Wawili Waliliacha Kanisa

GERMAN GOMERA alikuwa mtoto wa kumi kati ya watoto 11. Baada ya baba na dada zake wawili kufa, mama yake, Luisa, alihamia mjini pamoja na familia. Wakiwa huko, walijiunga na Kanisa la Wameno, ambalo kaka wawili wa Luisa na familia zao walikuwa waumini.

“Mwaka wa 1962, wenzi wa ndoa mapainia wa pekee walihamia katika mji wetu,” anasimulia German. “Ilisemwa kwamba walikuwa wakiwapotosha wakazi wa mji kwa ‘mafundisho ya kishetani.’ Hata hivyo, wenzi hao wa ndoa walipoitembelea familia ya Piña, walikaribishwa. Familia ya Piña ilikuwa kubwa. Walivutiwa na upole na urafiki wa mapainia hao, hivyo wakasikiliza kwa makini ujumbe wao. Matokeo ya ziara hiyo ni kwamba familia ya Piña na dada zangu watatu wakubwa walianza kujifunza.”

German anaendelea kusimulia hivi: “Siku moja, mapainia hao walipoitembelea familia ya Piña, Mama alialikwa pia. Walisoma maandiko ya Biblia yanayokazia tumaini la kuishi milele duniani. Mama akauliza, ‘Kwa nini basi, kanisani kwetu tunafundishwa kwamba tutaenda mbinguni?’ Baada ya ndugu kumjibu kwa kutumia Biblia na kumfafanulia kile ambacho Maandiko yanaeleza kuhusu tumaini la ufufuo duniani, Mama aliitikia vizuri na akaanza kuwaeleza wengine mambo aliyokuwa amejifunza.

“Makasisi wa Kanisa la Wameno walipojua kwamba baadhi ya waumini wao wanajifunza na Mashahidi wa Yehova, walijitahidi kuwashawishi waache kujifunza. Lakini walifanya hivyo kwa ukali na vitisho. Maximina, mama katika familia ya Piña, aliwaambia makasisi hivi, ‘Nisikilizeni! Mimi ni mtu mzima na nina uhuru wa kujifanyia uamuzi.’

“Hatimaye,” anasema German, “watu 22 waliliacha Kanisa la Wameno na kuanza kuhudhuria mikutano ya kutaniko katika nyumba ya kukodi. Mama alibatizwa mwaka wa 1965, nami nikabatizwa mwaka wa 1969, miaka minne baadaye, nikiwa na umri wa miaka 13.”

Picha katika ukurasa wa 163

German na dada zake leo. Wote wanamtumikia Yehova kwa uaminifu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki