MATUKIO MUHIMU YA MWAKA ULIOPITA
“Tumeona Maajabu Leo”
Ndugu kipofu abatizwa
SIKU moja Yesu alipomponya mwanamume aliyepooza, watu ‘wote walishangaa sana, wakasifu Mungu, wakajaa woga, wakisema: “Tumeona maajabu leo!”’ (Luka 5:25, 26, Zaire Swahili Bible) Tunapoona mambo ambayo Yehova anatimiza leo kupitia Mwana wake mpendwa, mtumwa mwaminifu na mwenye busara, na waabudu wake waaminifu duniani kote, tuna sababu kubwa ya kusema hivi: “Tumeona maajabu leo.”