Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g92 6/8 kur. 14-16
  • Naweza Kuishije Katika Nyumba Iliyogawanyika Kidini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Naweza Kuishije Katika Nyumba Iliyogawanyika Kidini?
  • Amkeni!—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mitego ya Kuepuka
  • Kufanya Uchaguzi Wako Mwenyewe wa Dini
  • Kuvuta Mzazi Wako Asiyeamini
  • Nishughulikeje na Mzazi Wangu Aliyeondoka Nyumbani?
    Amkeni!—1992
  • Nini Ikiwa Mzazi Wangu ni Mraibu wa Dawa za Kulevya au Pombe?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
  • Ni Kawaida Kuhuzunika Ninavyohuzunika?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
  • Naweza Kumsaidiaje Mzazi Wangu Aliye Peke Yake?
    Amkeni!—1992
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1992
g92 6/8 kur. 14-16

Vijana Wanauliza . . .

Naweza Kuishije Katika Nyumba Iliyogawanyika Kidini?

“Ilikuwa vigumu kwetu wakati wa kukua. Baba yangu alidharau dini yetu. Kulikuwa na mkazo daima nyumbani.”—Terry.

WEWE unaishi katika nyumba iliyogawanyika kidini? Ikiwa ndivyo, unajua jinsi mambo yanavyoweza kuwa yenye matata na magumu. Mama na baba wanaweza labda kuvumilia itikadi za mmoja na mwenzake, lakini kama vile S. Sandmel alivyoonelea katika kitabu chake When a Jew and Christian Marry: “Je! kuvumilia kwa mtu juu ya dini ya mwenzake huendelea hata kwa watoto wanaolelewa katika dini hiyo? Jibu la unyofu katika visa vingi ni la.”

Fikiria, kwa mfano, jambo ambalo lingeweza kutendeka ikiwa mmoja wa wazazi ni Shahidi wa Yehova. Mzazi huyo huhisi wajibu mzito wa kukulea “katika nidhamu ya Yehova na rekebisho la akilini” na huenda akawa na maoni yaliyo imara juu ya kufanya miadi, maadili, kushiriki katika michezo ya shule, utumizi wa wakati wa starehe, na miradi ya maisha. (Waefeso 6:4, NW) Ingawa, mzazi wako asiye Shahidi, anaweza kuwa na maoni yenye kuendekeza sana mambo haya.

Jumapili alasiri huenda mama akataka mwende naye katika mkutano wa Kikristo. Baba huenda akataka ukae nyumbani naye mkitazama mpira kwenye TV. “Kulikuwa na nyakati ambazo nilihisi sikitiko kidogo kwa baba yangu,” akumbuka Doug. “Alikuwa mwuuzaji bidhaa, kwa hivyo hatukumwona katikati ya juma, halafu katika mwisho juma, familia inamwacha wakati inapoenda kwenye mikutano yao. Mara moja-moja ningekosa kuenda mikutano na kubaki nikae naye.”

Yesu alitangulia kuona kwamba hali kama hizo zingetokea. Alisema hivi: “Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu; na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.” (Mathayo 10:35, 36) Si kwamba Yesu alikusudia kugawanya familia, lakini alijua kwamba matatizo yangetokea wakati wengine katika familia wangekubali kweli na wengine wasikubali. Swali ni: Ufanye nini ikiwa umo katika hali hiyo?

Mitego ya Kuepuka

La kwanza zaidi ya yote, tambua kwamba mradi ni kumpendeza, si mmoja wa wazazi wako tu, lakini Mungu mwenyewe! Yeye ndiye anayedai “ibada katika roho na kweli.” (Yohana 4:24) Lakini kufanya hivyo katika nyumba iliyogawanyika kidini, kuna baadhi ya mitego ya kuepuka.

Kuafikiana—Mvulana mmoja tineja ambaye wazazi wake walitalikiana asema kuhusu ziara kwa baba yake asiyeamini: “Anajaribu kunifanya mimi niende kinyume cha kweli na Mungu.” Yeye hufanya hivyo kwa kumkaza mtoto wake ashiriki katika sherehe zisizo za Kikristo. “Hilo lanifanya mimi nihisi mwenye kuhangaishwa sana,” mvulana akubali. Lakini Yesu atukumbusha sisi hivi: “Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili.” (Mathayo 10:37) Kwa hivyo simama imara kwa unaloamini! Ikiwa udhuru wako wenye busara kwa utendaji usiofaa hauridhishi, kwa fadhili lakini kwa imara acha mzazi wako ajue kwamba unakataa kuafikiana. Wakati mzazi wako aonapo nia yako isiyotikisika, huenda mkazo ukapungua polepole.

Kuna uhitaji wa usawaziko hata hivyo. Wafilipi 4:5, NW husema: “Acheni kiasi chenu kijulikane kwa watu wote.” Kiasi hutia ndani kukubali, kubadilikana. Labda unaweza kupanga mambo ili utumie wakati mwingi pamoja na mzazi wako asiyeamini ikiwa yeye anahisi ametupwa. Kumbuka, pia, kwamba una wajibu kwa wazazi wote wawili.—Waefeso 6:1.

Kujifanya ‘Msawazishaji’—Kutokana na fahamu zisizo na mwongozo mzuri, unaweza kushawishiwa kuchukua upande wa mama kwa mambo ya kidini kwa sababu tu ndugu yako amechukua upande wa baba au upande huo mwingine. Lakini je! huo ni msingi thabiti wa kuchagua jinsi ya kumwabudu Mungu? Vipi ikiwa maoni ya mama ya kidini ni ya uongo, yasiyo ya kimaandiko? “Inunue kweli, wala usiiuze,” yashauri Mithali 23:23.

Fuata Kiongozi—Labda unahisi ukaribu zaidi kwa ndugu au dada mkubwa kuliko yeyote wa wazazi. Hivyo huenda ukaelekea kufuata yoyote ya njia ya dini ambayo ndugu au dada yako huyo anachagua kwenda. “Hivyo ndivyo nilivyokuwa nikihisi, nikiwa wa familia kubwa,” asema Roberto. Kwa hivyo alipatwa na umivu la kurudi nyuma kiroho wakati ndugu yake mkubwa alipokataa ibada ya kweli na kuondoka nyumbani kabisa. “Lilikuwa lenye kuvunja moyo sana,” akubali. Bila kujali ni ukaribu wa jinsi gani unaohisi kuelekea ndugu, je! hautakuwa ujinga mtupu kuacha huyo akuongoze kutomtumikia Mungu?

‘Tenga na Ushinde’—“Wakati nilipokuwa karibu na miaka 19, baba yangu alianza kunitia moyo nifanye matembezi pamoja na wasichana,” akumbuka Doug. “Mama, ambaye alikuwa shahidi aliyebatizwa, alikuwa mwenye kupinga kabisa jambo hilo. Kwa ghafula nikajikuta nikimuunga mkono baba, ingawa ndani sana nilijua mama alikuwa sahihi.” Mahali ambapo wazazi wana viwango tofauti vya maadili, kunakuwa na nafasi ya kugonganisha mzazi mmoja dhidi ya mwingine. Inaweza kushawishi kumpenda mzazi anayetoa ruhusa kila mara.

Hata hivyo, kugonganisha mzazi mmoja dhidi ya mwingine, huongezea tu mikazo ya familia. Na kupata ruhusa ya kufanya jambo ambalo unajua si la busara au ni baya halikutolei udhuru machoni pa Mungu. “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hatendi, kwake huyo ni dhambi.” (Yakobo 4:17) Badala ya kutumia kwa werevu mzazi anayekupa wewe uhuru wote, kwa nini usijaribu kusikiliza mzazi yule anayekuongoza kwenye “njia ya uzima”?—Mithali 6:23.

Kufanya Uchaguzi Wako Mwenyewe wa Dini

Walakini, vijana wengine huenda wakavurugika kabisa kuhusu ni mzazi yupi aweza kuwa hivyo. Unaweza kuamuaje? Biblia inatueleza juu ya kijana Timotheo ambaye alikuwa katika nyumba iliyogawanyika kidini. Anaelezwa kuwa “mwana wa mwanamke Myahudi aliyeamini; lakini babaye alikuwa Myunani.” (Matendo 16:1) Wakati mwingine Timotheo lazima awe alihisi kugawanywa katikati ya wazazi wake. Ingawa hivyo, alikuja kushikamana na itikadi za dini ya mama yake na akawa msafiri mwenzi wa mtume Paulo. (Matendo 16:2, 3) Je! hilo lilikuwa ni kwa sababu alimpenda mama yake kuliko baba yake? Hata kidogo.

Mtume Paulo alimwandikia Timotheo: “Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao; na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.” (2 Timotheo 3:14, 15) Kutokana na hilo tunaweza kuona kwamba Timotheo alifanya chaguo lake litegemee kujifunza neno la Mungu kwa uzito! “Alihakikishwa,” akasadikishwa kuliamini.

Badala ya kufanya uchaguzi kwa msingi wa maoni au hisia, chunguza itikadi za wazazi wako katika nuru ya “maandiko matakatifu.”a Mwishowe wewe, si mama au baba, ndiwe mwenye daraka la kufanyia kazi wokovu wako!—Wafilipi 2:12.

Kuvuta Mzazi Wako Asiyeamini

Ukiwa umeazimia kwa moyo wako kufuata dini ya kweli, ni jinsi gani, basi, umwone mzazi wako asiyeamini? Mtume Paulo aliwatia moyo Wakristo kujaribu kuwavuta wenzi wao wasioamini: “Fikiria hili: kama mke huenda ukawa wokovu kwa mume wako; kama mume huenda ukawa wokovu kwa mke wako.” (1 Wakorintho 7:12-16, The New English Bible) Je! hilo haliwezi kutumika, katika kanuni kwa watoto wa wasioamini?

Mwenendo wako safi na heshima yenye kina kirefu kwa mzazi wako yaweza kumfanya yeye awe na uvutio wenye upendezi kwa Ukristo wa kweli. (Linganisha 1 Petro 3:1, 2.) Kumbuka, pia, kwamba kuchukua msimamo katika kweli hakumaanishi uko dhidi ya mzazi asiyeamini. Naam, kwa kuendelea kuwa mwenye kushirikiana, unaweza kumhakikishia huyo upendo wako mwendelevu.

“Kuna wakati wa kunyamaza na wakati wa kunena.” (Mhubiri 3:7) Ikiwa nafasi yatokea ya kuongea na mzazi wako kuhusu itikadi zako, vema, fanya hivyo! “Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao,” Mithali 3:27 yatukumbusha. Lakini uwe mwenye fadhili, na busara. Epuka kunyamazisha mzazi wako kwa sababu tu huenda unajua mengi kuhusu Biblia. Nani ajuaye, labda jitihada zako zitatokeza matunda. “Baba yangu alikuwa mpinzani mkali kwa miaka mingi,” akumbuka Jay. “Ilionekana kana kwamba hangebadilika, lakini mwishowe tulimvuta.” Wakati baba ya Jay alipokufa miaka michache iliyopita, alikuwa akitumikia akiwa mzee Mkristo.

Ikiwa hakuna itikio linalokuja, kumbuka maneno ya Daudi katika Zaburi 27:10: “Baba yangu na mama yangu wameniacha, bali BWANA [Yehova, NW] atanikaribisha kwake.” Wewe pia una marafiki waaminifu wenye kukutegemeza katika kundi la Kikristo, ambao wanaweza ‘kuambatana nawe kuliko ndugu.’ (Mithali 18:24) Kwa msaada wao pamoja na ule wa mzazi anayeamini, unaweza kusimama imara kwa kweli.

[Maelezo ya Chini]

a Ona makala zilizo na vichwa “Kwa Nini Nikubali Dini ya Wazazi Wangu?” na “Je! Biblia ni ya Kweli?” zinazopatikana katika Novemba 22, 1986, na Juni 8, 1987, za Amkeni (Kiingereza)

[Picha katika ukurasa wa 16]

Kugonganisha mzazi mmoja dhidi ya mwingine huenda ukafanya mambo yaende unavyotaka, lakini hatimaye, huongeza mikazo ya familia

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki