Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g91 12/8 kur. 24-25
  • Kifo cha Mtoto—Kwa Nini Mungu Hukiruhusu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kifo cha Mtoto—Kwa Nini Mungu Hukiruhusu?
  • Amkeni!—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Muumba Akuhurumia
  • Wakati Kifo Kilipoanza
  • Suala la Ulimwengu Wote Mzima Lahusika
  • Tukifa tunaenda wapi?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Adui wa Mwisho, Kifo, Aangamizwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Wafu Wako Wapi?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Yesu Huokoa—Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1991
g91 12/8 kur. 24-25

Maoni ya Biblia

Kifo cha Mtoto—Kwa Nini Mungu Hukiruhusu?

WAZAZI wengi waliofiwa hufarijika kujua kwamba Mungu hakuchukua mtoto wao kwa kifo, kama dini nyinginezo zinavyofundisha.a Hata hivyo, uhakika huu wenye uzito wa makini wabaki: Mungu ana uwezo wa kuzuia kifo. Na bado, hukiruhusu kiendelee.

Kwa hiyo mtoto anapokufa, huenda wazazi wakalia kwa uchungu, “Mbona Mungu aliruhusu tukio hilo litendeke?” Kifo, kiwe kimetokana na aksidenti, na maradhi, au na jeuri, karibu nyakati zote huonekana kuwa tendo la ukatili lisilo la haki. Kifo cha mtoto huonekana hivyo hata zaidi. Katika mojayapo ya makaburi, alama kwenye kaburi moja la mtoto, imeandikwa teto hili la kuhuzunisha: “Mchanga mno, kapendeza mno, [kafa] haraka mno.”

Muumba Akuhurumia

Mungu angeruhusuje uchungu kama huo? Ikiwa umepoteza mtoto katika kifo hivi karibuni, hakuna elezo lolote hata liwe lenye hoja kivipi, utakaotokomeza uchungu wa kifo hicho. Katika nyakati za Biblia, hata watu wenye imani yenye nguvu sana waliugua kwa ajili ya misiba ya maisha isiyo ya haki wakamwuliza Mungu kwa nini aliruhusu mambo kama hayo. (Linganisha Habakuki 1:1-3.) Lakini kuna majibu katika Biblia ambayo kwa wakati yaweza kutufariji.

Kwanza ujue kwamba Mungu hakutaka mtoto wako afe. Mungu hafurahii hata uangamizi wa waovu, licha ya kifo cha mtoto. (Linganisha 2 Petro 3:9.) Kwa hakika, yeye hupata uchungu mno mtoto anapokufa. Kwa vyovyote vile, tunahisi msiba wa kifo kwa sababu tu ya kwamba tuna uwezo wa kupenda, kuhurumia wanaopatwa nacho. Na tuna uwezo wa kupenda kwa sababu tu tumeumbwa kwa mfano wa Mungu. Sisi huonyesha uwezo mkamilifu wa Mungu wa kupenda, ingawa upeo wetu wa kufanya hivyo ni kwa uhafifu. (Mwanzo 1:26; 1 Yohana 4:8) Biblia yatuhakikishia ya kwamba Mungu husoma maono yetu ya moyoni yaliyo ndani kabisa, amehesabu nywele zenyewe za vichwa vyetu, ajua hata shomoro aangukapo kutoka kwenye mti. Hivyo, yeye aitwa “Baba wa rehema.”—2 Wakorintho 1:3; Mathayo 10:29-31.

Kwa wazi basi, Mungu hataki yeyote wa viumbe vyake wenye akili wafe. Akusudia kukomesha kifo, akikimaliza milele. (Isaya 25:8) Lakini iwapo hivyo ndivyo Yeye ahisi, mbona anaruhusu kifo wakati huu, hasa cha watoto?

Wakati Kifo Kilipoanza

Mungu huruhusu watoto wafe kwa sababu ile ile ambayo yeye huruhusu watu wazima wafe. Kifo kilikuwa chaguo la Adamu, si la Mungu. Hata kabla ya Adamu na Hawa kuasi dhidi ya Muumba wao katika Edeni, wote wawili walijua kwa ukamili kwamba Mungu alikuwa ameweka adhabu ya kifo kwa ajili ya dhambi. Ikiwa hawangechagua kutokutii Mungu, bado wangekuwa hai leo. Lakini kwa upumbavu walitupa ule urithi wenye thamani zaidi ambao wangalipitishia wazao wao—haki ya kupata uhai mkamilifu, wa milele duniani. Mara tu walipotenda dhambi, walipoteza ukamilifu. Wangeweza kuwapitishia wazao wao dhambi na kifo pekee.—Mwanzo 3:1-7; Warumi 5:12.

Lakini huenda ukastaajabu: ‘Kwa vile bei ilikuwa juu sana, mbona Mungu aliruhusu Adamu na Hawa watende dhambi? Au kwa nini hakuharibu uasi wao kabla ya hao kupitisha kifo na huzuni kwa watoto wao—na watoto wetu?’

Suala la Ulimwengu Wote Mzima Lahusika

Mungu aliruhusu wazazi wetu wa kwanza wakose kutii kwa sababu hakukusudia kamwe kuumba ulimwengu wa watu wafanyao mambo bila kufikiri wala kutumia akili, watu wanaomtumikia Mungu kwa sababu tu wamepangwa kufanya hivyo. Kama vile na mzazi yeyote, Mungu alitaka watoto wake wa kibinadamu wamtii kwa sababu ya hisia za tumaini na upendo, lakini siyo kwa kulazimishwa. Aliwapa Adamu na Hawa sababu za kutosha ili wamtumaini na kumpenda, lakini hata hivyo walikosa kutii wakakataa utawala wake.—Mwanzo 1:28, 29; 2:15-17.

Mbona Mungu hakuwaua waasi hao papo hapo? Mungu alikuwa tayari ameeleza kusudi lake kwamba siku moja dunia ingekaliwa kikamilifu na wazao wa Adamu na Hawa. Yeye hashindwi kamwe kutimiza makusudi yake. (Isaya 55:10, 11) Lakini jambo lililo la muhimu zaidi, swali la maana zaidi lilitokezwa katika Edeni. Je! Mungu ana haki ya kutawala juu ya mwanadamu, na je, njia Yake ndiyo iliyo bora zaidi, au mwanadamu aweza kujitawala mwenyewe vizuri zaidi?

Njia moja tu ya haki ya kujibu swali hilo mara moja tu kwa wakati wote ilikuwa kwa kuruhusu mwanadamu ajitawale mwenyewe. Historia imejibu swali hilo kwa njia ya kutia hofu. Matokeo ya kuhuzunisha ya utawala wa kibinadamu yaonekana kila mahali—ulimwengu ambamo kifo cha watoto wasio na hatia ni jambo la kawaida, ambalo karibu lipotelee katika wingi wa maovu mengine. Iwapo hakuna jambo jingine lolote ambalo limethibitishwa na utawala wa kibinadamu wa miaka elfu sita, hili limethibitishwa: Wazo la kwamba mwanadamu aweza kujitawala mwenyewe pasipo Mungu ni baya kuliko udanganyifu wa kuhuzunisha; ni uwongo mbaya sana. Maadamu mwanadamu aendelea kutawala pasipo Mungu, mwanadamu ataishi na kufa kwa uchungu.

Yehova, Mungu mwadilifu, mwenye upendo, amechagua njia yenye hekima zaidi. Kwa jinsi ile mzazi angeruhusu mtoto wake mpendwa afanyiwe upasuaji wenye uchungu kwa ajili ya wakati ujao wenye furaha na afya njema wa mtoto huyo, Mungu ameruhusu mwanadamu apitie uchungu wa kujitawala mwenyewe kwa ajili ya wakati ujao wa milele wa mwanadamu. Na kama vile uchungu wa upasuaji haubaki milele, utawala wa mwanadamu na matendo yao yasiyo haki yatakoma hivi karibuni.

Ufalme wa Mungu utakapotawala juu ya dunia bila upinzani, mamilioni ya watoto watafufuliwa na kukaribishwa kutoka kwa wafu. Kama wazazi ambao watoto wao walifufuliwa na Yesu wakarudi kwenye uhai tena katika karne ya kwanza W.K., wengi wakati huo ‘watashangaa mshangao mkuu.’ (Marko 5:42; Luka 8:56; Yohana 5:28, 29) Na ainabinadamu yote irudishwapo kwenye hali ya ukamilifu ambayo Adamu na Hawa walipoteza, basi hakuna yeyote atakayekufa tena kamwe—kutia na watoto!—Ufunuo 21:3, 4.

[Maelezo ya Chini]

a Ona “Maoni ya Biblia—‘Kwa Nini Mungu Alichukua Mtoto Wangu?’” katika toleo la Amkeni! la Oktoba 8, 1991.

[Blabu katika ukurasa wa 25]

Mamilioni ya watoto watafufuliwa na kukaribishwa kutoka kwa wafu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki