Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g94 12/8 kur. 10-13
  • Je, Wewe Ni Msikilizaji Mwenye Hisia-Mwenzi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe Ni Msikilizaji Mwenye Hisia-Mwenzi?
  • Amkeni!—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Nywea Katika Yasemwayo
  • Onyesha Uelewevu
  • Wasikilizaji Wema Huongea Pia!
  • Ustadi wa Kusikiliza kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Mwige Mfanya-wanafunzi Mkuu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Sikiliza Ili Ujifunze
    Amkeni!—2002
  • Nifanyeje Mtu Akinieleza Matatizo Yake?
    Amkeni!—2005
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1994
g94 12/8 kur. 10-13

Je, Wewe Ni Msikilizaji Mwenye Hisia-Mwenzi?

WAZIA kama ungekuwa na mali za kumpa kila mtu maishani mwako zawadi ghali. Lo, wangefurahi na kuthamini kama nini! Kwa kweli, wewe waweza kuwapa wengine zawadi maalumu, kitu fulani wahitajicho kikweli. Hakitakugharimu hata senti moja. Ni nini hicho? Uangalifu wako. Watu walio wengi hutaka uangalifu nao huitikia kwa uthamini waupokeapo. Hata hivyo, ili uwape uangalifu bora ni lazima uwe msikilizaji mwenye hisia-mwenzi.

Ikiwa wewe ni mzazi au mwajiri au watumikia katika cheo chochote ambacho watu hukujia kupata ushauri na mwelekezo, wahitaji kusikiliza kwa hisia-mwenzi. Usipofanya hivyo, watu watagundua ukosefu wako wa hisia-mwenzi, na kuaminika kwako kutaathiriwa.

Hata ikiwa wewe huombwi shauri mara nyingi, bado wahitaji kusikiliza watu kwa hisia-mwenzi, kama wakati rafiki akujiapo umfariji. Kama vile mithali ya Biblia itaarifuvyo, kukosa kusikiliza kabla ya kusema kwaweza kutokeza aibu. (Mithali 18:13) Basi, ni baadhi ya njia gani ambazo waweza kujionyesha kuwa msikilizaji mwenye hisia-mwenzi?

Nywea Katika Yasemwayo

Msikilizaji mwenye hisia-moyo ni nini? Webster’s New Collegiate Dictionary hufasili “hisia-mwenzi” hivi: “Uwezo wa kushiriki katika hisia au mawazo ya mwingine.” Kamusi hiyohiyo hufasili “sikiliza” hivi: “Kusikia kwa uangalifu wenye makini.” Kwa hiyo msikilizaji mwenye hisia-mwenzi hufanya zaidi ya kusikia tu yale mtu asemayo. Yeye hutoa uangalifu na kushiriki katika fikira na hisia za mtu huyo.

Hii hutaka kunywea katika yale unayosikia, bila kuruhusu akili yako itangetange. Hata kufikiria jinsi utakavyojibu hukengeusha kusikiliza. Jitie nidhamu ukae umekaza fikira juu ya yale anayosema mtu mwingine.

Mtazame moja kwa moja mtu anayesema nawe. Macho yako yakitangatanga, utaonekana kama usiyependezwa. Chunguza ishara zake na lugha ya mwili. Je, anatabasamu au anakunja uso? Je, macho yake yaonyesha ucheshi, huzuni, au hangaiko? Je, yale ayaachayo bila kuyasema yana maana? Usiwe na wasiwasi juu ya jibu lako; litaibuka kutokana na usikizi wako uliokazwa mahali pamoja.

Unaposikiliza, yaelekea utaitikia kwa kichwa na kutumia vionyesho vya kukubali, kama ‘naona’ na ‘naelewa.’ Hii yaweza kuonyesha kwamba unafuatana naye. Hata hivyo, usifikiri kwamba kuitikia kwa kichwa na kukubali-kubali kutafanya watu wafikiri kwamba unasikiliza na kumbe hufanyi hivyo kwa kweli. Hakika, kuitikia kwa kichwa kwa uendelevu kwaweza kufichua kwamba huna subira. Ni kama kwamba unasema, ‘Fanya haraka. Fanya upesi. Malizia.’

Vyovyote vile, hupaswi kuhangaika kupita kiasi juu ya mbinu zenyewe. Ebu sikiliza kikweli tu, na maitikio yako yataonyesha weupe wako wa moyo.

Maswali mazuri pia huonyesha kwamba umenywea katika yanayosemwa na unafuata. Hayo huonyesha wapendezwa. Omba uelewesho wa mambo yasiyosemwa au yasiyo wazi. Uliza maswali yaalikayo huyo mtu mwingine afafanue na kujieleza zaidi. Usiwe na wasiwasi kwamba huenda ukatize pindi kwa pindi, lakini usifanye hivyo kupita kiasi. Kuelewa mambo ni sehemu ya utaratibu wa kusikiliza. Ikiwa ukatizi haufanywi kupita kiasi, huyo mtu mwingine atathamini kwamba una tamaa ya kufahamu kikamili yote anayosema.

Onyesha Uelewevu

Hii yaweza kuwa ndiyo sehemu iliyo ngumu zaidi, hata ikiwa wamhurumia kikweli mtu anayeongea nawe. Wakati mtu mwenye msononeko akujiapo, je, wewe hujidukiza mbio-mbio ukiwa na madokezo na matatuzi ya kutazamia mema? Je, wewe huonyesha haraka kwamba hali si mbaya sana ilinganishwapo na kutaabika kwa mtu mwingineye? Hili lingeweza kuonekana kama lenye msaada, lakini laweza kuwa na tokeo hasi.

Kuna sababu kadhaa kwa nini ungeweza kuelekea kuacha kusikiliza na kuanza kutatua. Ungeweza kufikiri kwamba madokezo yako yenye idili ndiyo yahitajiwayo hasa kumchangamsha roho mtaabikaji. Au ungeweza kuhisi kwamba ni wajibu wako ‘kutengeneza’ chochote kile ‘chenye kasoro’ na kwamba usipofanya hivyo, husaidii wala “hufanyi kazi yako.”

Hata hivyo, kwa kawaida miminiko la mapema la masuluhisho humpa mtu ujumbe mbalimbali wenye kuvunja moyo, kama vile, ‘Nahisi tatizo lako likiwa sahili kuliko vile udaivyo.’ Au, ‘Napendezwa zaidi na sifa yangu mwenyewe ya kuwa mtatua-matatizo kuliko nipendezwavyo na hali-njema yako.’ Au, labda, ‘Sielewi kitu—wala sitaki kuelewa.’ Kulinganisha tatizo la mtaabikaji na yale ya wengine kwa kawaida huwasilisha habari hii, ‘Wapaswa kuaibika kwa kuhisi ukifadhaika hali watu wengine wanataabika kuliko wewe.’

Ikiwa bila kujua unatoa ujumbe mbalimbali huo wenye kuvunja moyo, rafiki yako atahisi kwamba hukumsikia kikweli, kwamba hawasilishi ujumbe wake. Huenda hata akakata shauri kwamba wewe wafikiri una cheo kikubwa kuliko yeye. Wakati ule mwingine, atageukia mtu mwingine kufarijiwa.—Wafilipi 2:3, 4.

Namna gani ikiwa rafiki yako afadhaika isivyohitajika? Kwa kielelezo, huenda akahisi hatia bila sababu ifaayo. Je, wapaswa uharakishe kumwambia kwamba sababu yake haifai ili aanze kuhisi vema? Sivyo, kwa sababu ikiwa hujamsikiliza kwanza, mahakikishio yako hayatafariji sana. Badala ya yeye kuhisi amepunguziwa mzigo, atahisi kwamba bado hajajiondolea mzigo huo, kwamba bado aibeba hatia yake. Kama vile mwanafalsafa wa karne ya 19 Henry David Thoreau alivyotamka, “huhitaji watu wawili kusema kweli: mmoja wa kuisema na mwingine wa kuisikia.”

Wafaa kama nini mwelekezo wa Biblia: ‘Mwe wepesi wa kusikia, bali si wepesi wa kusema.’ (Yakobo 1:19) Na pia ni jambo la maana sana kusikiliza kwa hisia-mwenzi! Shiriki katika hisia za anayekueleza usiri. Kubali ugumu wa tatizo lake, kina cha msononeko wake. Usidunishe tatizo lake kwa taarifa kama, ‘Aaa, ni leo tu mambo yamekuwia magumu’ au, ‘Mambo si mabaya hivyo.’ Kwa tokeo kinyume, udunishaji huo huenda hata ukazidisha hisia zake zilizofadhaika. Atavurugika hisia kwa sababu huchukui ujumbe wake kwa uzito. Kwa hiyo acha maitikio yako yaonyeshe kwamba wasikia lisemwalo na kwamba wakubali kwamba hivi ndivyo ahisivyo kwa sasa.

Usikizi wenye hisia-mwenzi haukutaki ukubaliane na mtu anayekutolea usiri wake. Huenda ukaamini kwamba mtu huyo hana haki ya kupandisha sauti hivi, “Naichukia kazi yangu!” Lakini ukiitikia kwa kutokubali (‘Hupaswi kuhisi hivyo’) au kwa kukanusha (‘Hakika hivyo sivyo wamaanisha’), atakata shauri kwamba huelewi. Maelezo yako yapasa yaonyeshe uelewevu wako. Kwa mtu achukiaye kazi yake, ungeweza kusema, ‘Lazima iwe yakupa mikazo.’ Halafu omba maelezo ya kuelewesha. Hivyo hukubaliani naye isivyohitajika kwamba apaswa kuchukia kazi yake bali unakiri tu kwamba hivi ndivyo ahisivyo kwa wakati uliopo. Kwa njia hiyo wampa uradhi wa kuwa amesikiwa, wa kuwa amewasilisha kikamili hisia zake. Mara nyingi, kushiriki tatizo hilo huenda kukalipunguza.

Vivyo hivyo, mtu asemaye, “Mke wangu anachunguzwa na daktari leo,” angeweza kuwa akimaanisha, “Nina wasiwasi.” Acha jibu lako lionyeshe watambua jambo hili. Yaonyesha kwamba uliisikiliza maana iliyokusudiwa na maneno hayo, na hiyo inafariji kuliko kama ungepuuza maana yake, kuikanusha, au kujaribu kumrekebisha kwa kumwambia kwamba hapaswi kuwa na wasiwasi.—Warumi 12:15.

Wasikilizaji Wema Huongea Pia!

The Art of Conversation chataja wale wasikilizao lakini wasemao machache sana, “wakifikiri kwamba hiyo huwapa haiba ya unyamavu wenye fahari.” Hii hushurutisha huyo mtu mwingine abebe mzigo wote wa maongezi, na huko ni kukosa adabu. Kwa upande ule mwingine, ni kukosa adabu pia, tena inachosha sana, ikiwa mtu unayemsikiliza aendelea kudondosha maneno bila kukuruhusu ujieleze. Kwa hiyo, ingawa wahitaji kuwa msikilizaji mwema, huenda ukataka pia kujulisha huyo mtu mwingine ajue kwamba una neno lenye msaada.

Ungeweza kusema nini? Ukiisha kusikiliza kwa staha maelezo ya rafiki yako, je, wapaswa sasa kutoa ushauri? Labda ndivyo, ikiwa una sifa za kukustahilisha kuutoa. Ikiwa una utatuzi kwa tatizo la rafiki yako, kwa vyovyote mwonyeshe. Maneno yako yatakuwa na uzito fulani, kwa kuwa ulitumia wakati ukisikiliza kwanza. Ikiwa huna sifa za ustahiki zihitajikazo kumpa rafiki yako aina ya mwelekezo au msaada ahitajio, jaribu kumsaidia apashane habari na mtu aliye katika cheo cha kuutoa.

Hata hivyo, katika visa fulani ushauri hauhitajiwi wala hauombwi. Kwa hiyo jihadhari usidhoofishe tokeo jema la kusikiliza kwako kwa kuongeza maneno mengi. Huenda rafiki yako akalazimika kuvumilia tu hali isiyodhibitika au atumie wakati aje kuzimudu hisia zake hasi. Yeye alikujia wewe ili ushiriki taabu yake. Wewe ulisikiliza. Ulishiriki hisia zake, ukamhakikishia kwamba wahangaika na kwamba wewe utamtia katika fikira na sala zako. Mwache ajue kwamba ana uhuru wa kukujia tena na kwamba utastahi usiri wa matatizo yake. Huenda akawa hasa ahitaji faraja hiyo kuliko kukuacha ujaribu kutengeneza tatizo lake.—Mithali 10:19; 17:17; 1 Wathesalonike 5:14.

Iwe kusikiliza kwaandamana na ushauri au sivyo, kwanufaisha wahusika wote wawili. Mwenye kusema ana uradhi wa kusikiwa na kuelewa. Afarijiwa kujua mtu fulani ajali vya kutosha kuyasikia yake yote. Msikilizaji athawabishwa pia. Wengine wathamini hangaiko lake. Akitoa ushauri, huo ndio wenye kustahiki hata zaidi kwa sababu hasemi mpaka awe ameifahamu kikamili hali aliyoletewa. Ni kweli kwamba usikizi wenye hisia-mwenzi huchukua wakati. Lakini lo, ni akiba yenye faida kama nini! Kwa kweli, kwa kuwapa watu uangalifu wako wenye makini, wawapa zawadi maalumu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki