Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g97 8/22 kur. 10-11
  • Suluhisho Ni Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Suluhisho Ni Nini?
  • Amkeni!—1997
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Msingi wa Kutazamia Mazuri
  • Atakalofanya Mungu
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Tatizo la Maji Ulimwenguni?
    Habari Zaidi
  • Sehemu Zenye Shida Zaidi
    Amkeni!—1997
  • Maji Halisi na ya Kiroho Ni Muhimu kwa Uhai
    Amkeni!—2001
  • Je, Maji Yanazidi Kupungua Ulimwenguni?
    Amkeni!—2001
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1997
g97 8/22 kur. 10-11

Suluhisho Ni Nini?

WATAALAMU wana mijadala motomoto kuhusu masuluhisho ya matatizo tata ya maji ya wanadamu. Benki ya Ulimwengu yataka dola bilioni 600 zitumiwe kwa usafi wa kutunza afya na mipango ya maji kwa miaka kumi ijayo. Gharama ya kutotumia pesa hizo yaweza kuwa juu hata zaidi. Kwa mfano, nchini Peru, mweneo wa kipindupindu kwa majuma kumi, uliosababishwa na maji machafu, hivi majuzi uligharimu karibu dola bilioni 1—mara tatu ya fedha zilizotumiwa katika ugavi wa maji wa hiyo nchi katika mwongo wote wa miaka ya 1980.

Hata hivyo, japo makusudio mazuri ya wale wanaoiendeleza, miradi ya maji mara nyingi haisaidii sana wale walio maskini zaidi. Ongezeko katika majiji makubwa ya nchi zinazoendelea ni la haraka sana na la kiholela. Maskini huishi katika vibanda hafifu vilivyosongamana kupita kiasi na visivyo na maji au usafi wa kutunza afya. Kwa kuwa hawawezi kufikia huduma za maji zinazotolewa na serikali, ni lazima wanunue maji kwa bei ghali kutoka kwa watu binafsi, mara nyingi maji machafu.

Kwa wazi, shida ya maji tufeni pote ni tata na huhusisha visababishi vinavyohusiana: upungufu wa maji, uchafuzi, umaskini, maradhi, na uhitaji unaoongezeka wa idadi za watu zenye kuongozeka. Vivyo hivyo ni wazi kwamba wanadamu hawawezi kutatua matatizo haya.

Msingi wa Kutazamia Mazuri

Hata hivyo, wakati ujao si wenye kuhuzunisha kama wengi watabirivyo. Kwa nini? Kwa sababu suluhisho la shida ya maji ya ulimwengu haliwezi kutolewa na mwanadamu; laweza kutolewa na Mungu. Ni yeye peke yake aliye na uwezo na vilevile nia ya kutatua matatizo yote ya maji.

Si jambo la kutiliwa shaka kwamba Yehova Mungu aweza kutatua matatizo haya. Yeye ndiye Mbuni na Muumba si wa dunia tu bali pia wa maji yaliyo ndani ya dunia. Ni yeye aliyeanzisha duru ya maji ya ajabu pamoja na duru nyinginezo zote za kiasili ambazo hufanya maisha duniani yawezekane. Ufunuo 14:7 humtambulisha Yehova kuwa “Yeye aliyezifanya mbingu na dunia na bahari na mabubujiko ya maji.”

Yehova ana uwezo wa kudhibiti maji ya ulimwengu. Ni “Yeye atoaye mvua inyeshe juu ya nchi, na kuyapeleka maji mashambani.” (Ayubu 5:10) Juu yake Biblia husema: “Amegeuza jangwa ikawa ziwa la maji, na nchi kavu ikawa chemchemi za maji.”—Zaburi 107:35.

Tena na tena amethibitisha uwezo wake wa kuandaa maji. Kwa mfano, yeye aliwaandalia Waisraeli maji wakati wa miaka 40 jangwani, nyakati fulani kimwujiza. “Akatokeza na vijito gengeni, akatelemsha maji kama mito,” husema Biblia. “Tazama, aliupiga mwamba; maji yakabubujika, ikafurika mito.”—Zaburi 78:16, 20.

Atakalofanya Mungu

Mungu hataruhusu shida ya maji iendelee milele. Biblia hutabiri kwamba wakati waja ambapo atatenda kwa niaba ya wale wote ulimwenguni pote ambao hutamani kuishi chini ya utawala wenye upendo wa serikali yake ya kimbingu, ambayo hivi karibuni itachukua uongozi wa dunia.—Mathayo 6:10.

Serikali hiyo, au Ufalme, itamaliza maradhi yasababishwayo na maji, pamoja na magonjwa mengineyo. Biblia huhakikishia waaminifu-washikamanifu wa Mungu hivi: ‘Mungu atakibarikia chakula chako, na maji yako; naye atakuondolea ugonjwa kati yako.’ (Kutoka 23:25) Isitoshe, wachafuzi wa maji ya dunia wataharibiwa ‘atakapoleta kwenye uangamizi wale wanaoiangamiza dunia.’—Ufunuo 11:18.

Dunia yote itasitawi chini ya utunzi wenye upendo wa Mungu. Watu hawatapata kung’ang’ana tena kamwe kutafuta maji safi yaliyo matamu. Mungu Mweza Yote, ambaye sikuzote husema kweli, alimpulizia nabii wake aandike hivi kuhusu wakati ujao: “Maana katika nyika maji yatabubujika; na vijito jangwani. Na mchanga ung’aao mfano wa maji utakuwa ziwa la maji, na nchi yenye kiu itakuwa chemchemi za maji.”—Isaya 35:6, 7; Waebrania 6:18.

[Picha katika ukurasa wa 10]

Mungu aahidi: “Katika nyika maji yatabubujika; . . . na nchi yenye kiu itakuwa chemchemi za maji.”—Isaya 35:6, 7

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki