Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g99 9/22 kur. 7-9
  • Kukoma kwa Vita

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kukoma kwa Vita
  • Amkeni!—1999
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tumaini Hakika la Amani ya Ulimwenguni Pote
  • Jinsi Gani na kwa Nini Uamini Ahadi za Mungu?
  • Amani Duniani—Itapatikanaje?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Serikali ltakayoleta Amani Duniani Pote
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Ufalme wa Mungu Watawala
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1999
g99 9/22 kur. 7-9

Kukoma kwa Vita

KILA mahali watu wametamani kwa muda mrefu ulimwengu usio na vita. Ni tamaa ambayo haijatimizwa bado. Kama tulivyoona kwenye makala iliyotangulia, wengi huitikadi kwamba amani ya ulimwenguni pote inaweza kuletwa tu na serikali ya ulimwengu, serikali inayoweza kuwakilisha watu wote duniani bila ubaguzi wowote. Ingawa hivyo, wengi hung’amua kwamba watawala wa kibinadamu hawawezi kuacha kwa hiari serikali inayowakilisha kila mtu duniani itawale badala yao. Je, hili lamaanisha kwamba serikali ya ulimwengu haiwezi kuwapo?

Huenda ikaonekana hivyo. Lakini, unabii wa Biblia unaonyesha kwamba serikali ya ulimwengu yenye kutawala dunia yote karibuni italeta amani duniani. Amani hii haitaletwa kupitia kwa mashauri ya amani ya wanadamu wala kupitia kwa miafaka ya kimataifa. Nabii Danieli alipuliziwa kuandika hivi: “Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele.”—Danieli 2:44, italiki ni zetu.

Ni Ufalme huu ambao Yesu aliwaambia wafuasi wake wasali juu yake katika ile sala inayojulikana na mamilioni ya watu kuwa Sala ya Bwana, au Baba Yetu. Labda unajua sala hiyo, ipatikanayo katika Mathayo 6:9, 10 kwenye Biblia. Sehemu ya sala hiyo inamsihi Mungu hivi: “Acha ufalme wako uje. Mapenzi yako na yatendeke, kama ilivyo katika mbingu, pia juu ya dunia.” Mungu atajibu sala hiyo. Karibuni Ufalme huo ‘utakuja’ kutimiza mapenzi ya Mungu kwa ajili ya dunia. Mapenzi ya Mungu yanahusisha kugeuza umbo la dunia yote kuwa paradiso ya amani.

Tumaini Hakika la Amani ya Ulimwenguni Pote

Je, kuna sababu yoyote ya kuamini kwamba Ufalme wa Mungu utatokeza hali bora kuliko serikali za wanadamu? Fikiria sehemu nane za Ufalme wa Mungu ambazo zitahakikisha kuwapo kwa amani ya kudumu kwa wote walio chini ya miliki yake.

1. Ufalme huo utaongozwa na kiongozi aliyeteuliwa na Mungu, Yesu Kristo aliyetukuzwa, ‘Mfalme wa Amani.’ (Isaya 9:6) Yesu alipokuwa duniani, alionyesha kwamba watumishi wake hawabebi silaha za kupigana vita halisi. Alimwambia Petro: “Rudisha upanga wako mahali pao, kwa maana wale wote wauchukuao upanga wataangamia kwa upanga.”—Mathayo 26:52.

2. Kwa kweli Ufalme huo utakuwa serikali ya ulimwengu. Kuhusu mamlaka aliyopewa Yesu, Danieli alitabiri: “Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie.”—Danieli 7:14.

3. Ufalme huo utawakilisha watu wote. Yesu atakuwa na watawala-wenzi “kutoka kila kabila na ulimi na watu na taifa” nao “watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia.”—Ufunuo 5:9, 10.

4. Ufalme wa Mungu utaangamiza serikali zote za kibinadamu, ambazo zinapinga mamlaka yake. ‘Ufalme huo . . . utavunja falme hizi zote [za wanadamu] vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.’—Danieli 2:44.

5. Wakazi wa dunia wataongozwa na sheria ya kimataifa. Isaya alitabiri hivi kuhusu wakati huo: “Maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la BWANA katika Yerusalemu. Naye atafanya hukumu katika mataifa mengi, atawakemea watu wa kabila nyingi.”—Isaya 2:3, 4.

6. Raia wa Ufalme huo watajifunza njia za amani. Isaya akaendelea kusema: “Nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.”—Isaya 2:4.

7. Wanaopenda jeuri watafagiliwa mbali. ‘BWANA humjaribu mwenye haki; bali nafsi yake humchukia asiye haki, na mwenye kupenda udhalimu. Atawanyeshea wasio haki mitego, moto na kiberiti na upepo wa hari, na viwe fungu la kikombe chao.’—Zaburi 11:5, 6.

8. Silaha zitaondolewa kabisa. “Njoni myatazame matendo ya BWANA, jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi. Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari.”—Zaburi 46:8, 9.

Jinsi Gani na kwa Nini Uamini Ahadi za Mungu?

Biblia hueleza mambo mengi zaidi juu ya Ufalme wa Mungu. Kwa mfano, inaonyesha ni nani watakaoshirikiana na Yesu Kristo katika kuongoza mambo ya dunia. Na zaidi inasema jinsi wanavyoteuliwa na sifa zinazowastahilisha. Biblia huonyesha pia jinsi Ufalme huo utakavyotumia rasilimali za dunia kuletea wakazi wote wa dunia ufanisi na furaha, utaondoa wivu na pupa ambazo mara nyingi zimeleta migogoro.

Je, unabii huu unaweza kuaminiwa? Yehova mwenyewe amesema: “Neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.” (Isaya 55:11) Taarifa hii ni uhakikisho thabiti kwamba Mungu hutimiza ahadi zake. Yehova ni Mweza Yote, kwa hiyo ana uwezo wa kuleta amani ulimwenguni pote. Hakuna jambo asiloweza kuelewa; kwa hiyo, ana hekima ya kudumisha amani. (Isaya 40:13, 14) Isitoshe, Yehova ni wonyesho halisi wa upendo, hivyo hakuna mtu awaye yote katika ulimwengu wote mzima aliye na tamaa kubwa zaidi ya kuleta amani ulimwenguni.—1 Yohana 4:8.

Bila shaka, imani inahitajika ili kuweza kuamini ahadi za Mungu. Imani hutegemea ujuzi na huo hukuzwa kupitia funzo la Neno la Mungu, Biblia. (Wafilipi 1:9, 10) Uhalisi wa Ufalme wa Mungu unadhihirika tunapojifunza juu ya utu wa Mungu na makusudi yake. Naam, vita vitakomeshwa kabisa, si kupitia jitihada za wanadamu, bali kupitia serikali tukufu ya ulimwengu inayoongozwa na Mungu, Ufalme wa Mungu.

[Picha katika ukurasa wa 8, 9]

Chini ya Ufalme wa Mungu, raia watajifunza amani, na silaha zitaondolewa kabisa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki