Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 4/08 uku. 3
  • Siku za Mwisho—Za Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Siku za Mwisho—Za Nini?
  • Amkeni!—2008
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Amwahidi Danieli Thawabu ya Ajabu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Jinsi Kitabu Cha Danieli Kinavyokuhusu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Watiwa Nguvu na Mjumbe Kutoka Kwa Mungu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Danieli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2008
g 4/08 uku. 3

Siku za Mwisho—Za Nini?

UKIONA ishara “Siku za Mwisho” katika dirisha la duka fulani, huenda ujumbe wake ukaeleweka kwa urahisi. Unaweza kumaanisha kwamba kipindi cha kuuza bidhaa fulani kwa bei ya chini kinakaribia kwisha au kwamba duka hilo linakaribia kufungwa. Lakini vipi mtu akisema, “Tunaishi katika siku za mwisho”? Maneno hayo yanamaanisha nini?

Maneno “siku za mwisho” na “wakati wa mwisho” yametumiwa kwa muda mrefu sana. (2 Timotheo 3:1; Danieli 12:4) Zaidi ya miaka 2,500 iliyopita nabii Danieli alipewa maono kuhusu serikali kuu za ulimwengu na kuhusu mapambano ambayo yangetukia kati ya serikali hizo kufikia “wakati wa mwisho.” Danieli aliambiwa kwamba maana ya maono hayo ingefunuliwa wakati wa mwisho. (Danieli 8:17, 19; 11:35, 40; 12:9) Danieli aliandika hivi pia: “Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote, nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo.”—Danieli 2:44.

Yesu Kristo alirejelea “ule mwisho” alipokuwa akijibu swali kuhusu “ishara ya kuwapo [kwake] na ya umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 24:3-42) Inaelekea kwamba Danieli na Yesu walikuwa wakirejelea mwisho, yaani, badiliko kubwa ambalo litaathiri watu wanaoishi na waliowahi kuishi duniani. Danieli aliandika kuhusu mwisho wa serikali zote za kidunia. Yesu alizungumza kuhusu “umalizio wa mfumo wa mambo.”

Je, unapaswa kuhangaikia jambo hilo? Bila shaka. Wanadamu wote wanapaswa, kwa sababu wote wanahusika. Hata hivyo, watu wengi hawachukulii jambo hilo kwa uzito. Biblia ilitabiri hivi: “Katika siku za mwisho watakuja wadhihaki na dhihaka zao, wakiendelea kulingana na tamaa zao wenyewe na kusema: ‘Huku kuwapo kwake kulikoahidiwa kuko wapi? Kwani, tangu siku mababu zetu walipolala katika kifo, mambo yote yanaendelea sawasawa kama tangu mwanzo wa uumbaji.’” (2 Petro 3:3, 4) Naam, watu fulani leo wanahisi kwamba historia inajirudia, kwamba maisha hayatawahi kubadilika.

Je, kuna uthibitisho wowote unaoonyesha kwamba kwa kweli tunaishi katika kipindi ambacho Biblia inakiita siku za mwisho? Acheni tuone.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki