Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 3/10 uku. 10
  • Tunajifunza Nini Kutokana na Vitu vya Asili?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tunajifunza Nini Kutokana na Vitu vya Asili?
  • Amkeni!—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Zawadi Zinazotufanya Tuwe Viumbe wa Kipekee
    Amkeni!—2003
  • “Sifa Zake Ambazo Hazionekani, Zinaonekana Waziwazi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Vutiwa na Ubuni Jifunze Kumhusu Mbuni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2010
g 3/10 uku. 10

Tunajifunza Nini Kutokana na Vitu vya Asili?

“Jinsi kazi zako zilivyo nyingi, Ee Yehova! Zote umezifanya kwa hekima.”—Zaburi 104:24.

WATU wengi wanapotaja kuhusu “vitu vya asili” wao huwa wanaonyesha kwamba vitu vilivyo hai vilibuniwa kutoka chanzo fulani. Kwa mfano, katika toleo la Machi (Mwezi wa 3) 2003, jarida Scientific American lilisema hivi: “Kati ya vitu vyote vilivyobuniwa kufunika miili ya viumbe, manyoya ndiyo yenye unamna-namna na yenye kushangaza zaidi.” Ingawa huenda mwandishi huyo akafikiri kwamba vitu vya asili vilijitokeza, anasema kwamba manyoya ‘yalibuniwa.’ Je, vitu vya asili vinaweza kujitokeza vyenyewe?

“Kubuni” kunamaanisha “kupangia (kitu) ukiwa na kusudi au nia hususa akilini.” (The New Oxford Dictionary of English) Ni mtu tu anayeweza kubuni na kuvumbua. Kama vile wavumbuzi walivyo na majina, Muumba pia ana jina. Yehova ndiye Mbuni wa vitu vya asili. Yeye peke yake ndiye ‘Aliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote,’ na ndiye ‘aliyeumba vitu vyote.’—Zaburi 83:18; Ufunuo 4:11.

Tunajifunza nini kutokana na uumbaji? Mambo ya maana zaidi yanatufundisha kumhusu Yehova na sifa zake za ajabu, kutia ndani hekima yake. “Sifa zake ambazo hazionekani, zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinaeleweka kwa vitu vilivyofanywa, yaani, nguvu zake za milele na Uungu.” (Waroma 1:20) Vitu vya asili vinatufunza kwamba hekima ya Mungu ni ya hali ya juu kuliko yetu. Ikiwa anaweza kubuni vitu bora zaidi kuliko wavumbuzi, je, haipatani na akili kwamba anaweza kutupa mashauri bora zaidi kuliko mashauri ya wanadamu?

Mashauri ya Mungu hayaonekani tu katika “kitabu cha uumbaji,” lakini yanapatikana katika Neno lake, Biblia. Katika Biblia unaweza kupata ushauri mwingi wenye kutegemeka. Biblia inasema: “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida.”—2 Timotheo 3:16.

Ikiwa unapendezwa kujifunza kuwahusu wavumbuzi, bila shaka utapendezwa hata zaidi kujifunza kumhusu Muumba. Kwa mfano, huenda unataka kupata majibu ya maswali kama vile: Kwa nini tunateseka na kufa? Je, hilo ndilo kusudi la Mungu kwa wanadamu? Ikiwa sivyo, kwa nini Mungu anawaacha watu wateseke?

Iwe wanakubali au la, wanasayansi wamejifunza ubuni kutoka kwa Yehova. Wewe pia unaweza kujifunza mengi kutoka kwa Muumba wetu. Kwa mfano, unaweza kujifunza jinsi ya kuwa na ndoa imara, jinsi ya kulea watoto kwa mafanikio, kusudi la Mungu kwa dunia, na mambo mengi zaidi yanayoweza kufanya maisha yako yawe yenye kusudi. Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova, kinaweza kukusaidia unufaike kikamili kutokana na Neno la Mungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki