Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 1/14 kur. 2-6
  • Tovuti ya Kipekee

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tovuti ya Kipekee
  • Amkeni!—2014
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Ajili Ya Wenzi Wa Ndoa
  • Kwa Ajili Ya Wazazi
  • Kwa Ajili Ya Matineja
  • KWA AJILI YA WALE WANAOTAKA KUJIFUNZA BIBLIA
  • Yaliyomo
    Amkeni!—2015
  • Kupata Msaada wa Kuielewa Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Tumia Trakti Mpya ya Tovuti
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Yaliyomo
    Amkeni!—2016
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2014
g 1/14 kur. 2-6
Mwanamke kijana akitembelea jw.org

HABARI KUU

Tovuti ya Kipekee

  • SOMA Biblia katika lugha 50 hivi na habari zinazotegemea Biblia katika lugha zaidi ya 500.

  • TAZAMA habari katika lugha 70 hivi za ishara.

  • FUNGUA tovuti hii katika mamia ya lugha.

  • SIKILIZA drama zilizorekodiwa zinazohusu matukio ya Biblia yenye kusisimua.

  • ONA matukio ya Biblia kwenye hadithi zenye michoro.

  • TAZAMA drama na video za Biblia zitakazokusaidia kukabiliana na matatizo ya maisha.

  • PAKUA faili za kielektroniki za magazeti, vitabu, na makala zilizorekodiwa bila malipo.

  • FANYA UTAFITI kuhusu habari mbalimbali ukitumia Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO—sehemu yenye habari chungu nzima, inayopatikana katika lugha zaidi ya 100.

Kwa Ajili Ya Wenzi Wa Ndoa

“Ninataka familia yangu ifanikiwe. Mimi na mke wangu tumekabili matatizo mengi, hasa baada ya kupata watoto. Tunahitaji msaada”

BIBLIA INASEMA:

“Nyumba hujengwa kwa hekima, na kwa utambuzi itasimamishwa imara.”—Methali 24:3.

SEHEMU MUHIMU ZA TOVUTI HII

Mume na mke wakitembelea sehemu ya Wenzi wa Ndoa na Wazazi kwenye jw.org

Sehemu ya “Wenzi wa Ndoa na Wazazi” inaweza kukusaidia ujue:

  • Jinsi ya kuepuka maneno yenye kuumiza

  • Jinsi ya kukomesha tabia ya kunyamaziana

  • Jinsi ya kuwatia watoto nidhamu

  • Jinsi ya kuacha kugombana

  • Jinsi ya kusamehe

(Tafuta chini ya MAFUNDISHO YA BIBLIA > WENZI WA NDOA NA WAZAZI)

Siri ya Kupata Furaha ya Familia ni kitabu kinachozungumzia mambo mengi kuhusu familia, kutia ndani kujitayarisha kwa ajili ya ndoa ukiwa mseja na pia jinsi ya kuwatunza wazazi waliozeeka.

(Pia, unaweza kukipakua kwenye Tovuti ya www.jw.org/sw. Tafuta chini ya MACHAPISHO > VITABU NA BROSHUA)

Kwa Ajili Ya Wazazi

“Watoto wangu ndio watu muhimu zaidi kwangu. Ninataka wawe watu wazima nitakaojivunia”

BIBLIA INASEMA:

“Mlee mvulana kulingana na njia inayomfaa; hata atakapozeeka hatageuka kando na kuiacha.”—Methali 22:6.

SEHEMU MUHIMU ZA TOVUTI HII

Baba na kijana wake mdogo wakitembelea sehemu ya Watoto kwenye jw.org

Sehemu ya “Watoto” ina hadithi za Biblia zenye michoro, mazoezi ya picha, video, na masomo ya Biblia yanayoweza kukusaidia kuwafundisha watoto wako mambo kama vile . . .

  • kuwa watiifu

  • kuonyesha fadhili

  • kuishi vizuri na wengine

  • kujifunza kusema “asante”

(Tafuta chini ya MAFUNDISHO YA BIBLIA > WATOTO)

Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia na Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu ni vitabu vyenye picha maridadi unavyoweza kusoma pamoja na watoto wako.

(Pia vinapatikana kwenye Tovuti ya www.jw.org/sw. Tafuta chini ya MACHAPISHO > VITABU NA BROSHUA)

Kwa Ajili Ya Matineja

“Ningependa kupata madokezo ya jinsi ya kushughulika na shule, wazazi wangu, marafiki, na watu wa jinsia tofauti. Mimi si mtoto, hivyo sitaki kuamrishwa kila mara”

BIBLIA INASEMA:

“Moyo wako ukufanyie mema siku za ujana wako.”—Mhubiri 11:9.

SEHEMU MUHIMU ZA TOVUTI HII

Kijana akitazama sehemu ya Matineja kwenye jw.org

Sehemu ya “Matineja” ina makala na video zinazoweza kukusaidia . . .

  • unapohisi upweke

  • unapokuwa na matatizo shuleni

  • unapovunja sheria ya wazazi wako

  • unapoonewa na vijana wenzako au kusumbuliwa kingono

(Tafuta chini ya MAFUNDISHO YA BIBLIA > MATINEJA)

Kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, buku la 1 na 2 huzungumzia maswali muhimu 77 yanayoulizwa mara nyingi.

(Vitabu hivyo vinapatikana pia kwenye Tovuti ya www.jw.org/sw. Tafuta chini ya MACHAPISHO > VITABU NA BROSHUA)

KWA AJILI YA WALE WANAOTAKA KUJIFUNZA BIBLIA

“Ningependa kuielewa Biblia. Nifanyeje?”

BIBLIA INASEMA:

“Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida kwa kufundisha.” —2 Timotheo 3:16.

SEHEMU MUHIMU ZA TOVUTI HII

Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ni tafsiri sahihi inayotumia lugha rahisi.

(Tafuta chini ya MACHAPISHO > BIBLIA)

Sehemu ya “Majibu ya Maswali ya Biblia” inajibu waziwazi maswali kama vile “Je, Biblia ni kitabu cha wazungu?” na “Je, Mungu ndiye wa kulaumiwa kwa sababu ya kuteseka kwetu?”

(Tafuta chini ya MAFUNDISHO YA BIBLIA > MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA)

Sehemu ya “Jifunze Biblia Bila Malipo” inakupa nafasi ya kupata mafunzo ya Biblia bila malipo.

(Bonyeza “Omba Ufundishwe Biblia” kwenye sehemu ya chini ya ukurasa wa kwanza wa Tovuti yetu)

“Niliacha kusoma Biblia kwa sababu sikuielewa. Lakini nilipoisoma kwa kutumia kitabu ‘Biblia Inafundisha Nini Hasa?’ nilishangaa kuona jinsi Biblia inavyoeleweka kwa urahisi.”—Christina.

JE, UNA MASWALI KUHUSU MASHAHIDI WA YEHOVA?

Sehemu ya “Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi” hujibu maswali yanayoulizwa kuhusu Mashahidi wa Yehova, kama vile, “Mbona mnawatembelea watu walio na dini zao?” na “Kazi yenu inagharimiwaje?”

(Tafuta chini ya KUTUHUSU > MASWALI YANAYOULIZWA MARA NYINGI)

Kila siku, watu 700,000 hivi hutembelea Tovuti ya jw.org. Wewe pia unakaribishwa uitembelee.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki