Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 4/14 uku. 7
  • Kwa Sababu Mambo Hubadilika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Sababu Mambo Hubadilika
  • Amkeni!—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Afadhali Nijiue?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
  • 4 | Linda Tumaini Lako
    Amkeni!—2022
  • Ninataka Kufa—Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Ikiwa Nina Mawazo ya Kujiua?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Jinsi ya Kukabiliana na Mabadiliko
    Amkeni!—2016
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2014
g 4/14 uku. 7

HABARI KUU | USIKATE TAMAA!

1 Kwa Sababu Mambo Hubadilika

“Tunakazwa katika kila njia, lakini hatubanwi kupita kiasi cha kuweza kusonga; tunafadhaishwa, lakini si bila njia ya kutokea kabisa.”—2 WAKORINTHO 4:8.

Kujiua kumeitwa “suluhisho la kudumu la tatizo la muda mfupi.” Ingawa huenda ikawa vigumu kuamini, hali yenye kufadhaisha hata ile unayohisi imepita uwezo wako ni ya muda tu. Kwa kweli inaweza kubadilika na kuwa bora kwa njia isiyotazamiwa.—Ona sanduku “Hali Zao Zilibadilika.”

Hata hali isipobadilika, ni vizuri kushughulikia tatizo moja baada ya lingine. Yesu alisema, “Msihangaike kamwe juu ya kesho, kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe. Unatosha kila siku ubaya wake.”​—Mathayo 6:34.

Utafanya nini ikiwa hali yako haiwezi kubadilika? Kwa mfano, labda una ugonjwa wa kudumu. Au labda umekata tamaa kwa sababu ya kuvunjika kwa ndoa au umefiwa na mtu unayempenda.

Hata katika hali kama hizo, bado kuna jambo unaloweza kubadili: maoni yako kuhusu hali hiyo. Unapokubali kwamba kuna mambo usiyoweza kubadili, inakuwa rahisi zaidi kuwa na maoni yanayofaa. (Methali 15:15) Pia, itakuwa rahisi zaidi kwako kuvumilia hali ngumu badala ya kuona kifo kama suluhisho. Matokeo ni nini? Utaanza kudhibiti maoni yako kuhusu hali ambayo inaonekana kwamba imepita uwezo wako.​—Ayubu 2:10.

KUMBUKA: Huwezi kupanda mlima kwa hatua moja tu, lakini unaweza kuupanda hatua kwa hatua. Ndivyo unavyoweza kukabiliana na matatizo, hata yakiwa makubwa kama mlima.

UNACHOWEZA KUFANYA SASA: Zungumza na mtu fulani, labda rafiki au mtu wa familia kuhusu hali yako. Huenda mtu huyo akakusaidia kuwa na maoni yaliyosawazika kuhusu hali yako.​—Methali 11:14.

HALI ZAO ZILIBADILIKA

Wafikirie watu wanne waaminifu katika Biblia waliokata tamaa hivi kwamba wakatamani kufa.

  • Rebeka: “Ikiwa hivi ndivyo ilivyo, hasa kwa nini niko hai?”—Mwanzo​—25:22.

  • Musa: “Tafadhali niue kabisa. . . . Wala usiache niutazame msiba wangu.”—Hesabu​—11:15.

  • Eliya: “Iondoe nafsi yangu, kwa maana mimi si bora kuliko mababu zangu.”—1 Wafalme​—19:4.

  • Ayubu: “Kwa nini sikufa tokea tumbo la uzazi?”​—Ayubu 3:11.

Ukisoma masimulizi ya Biblia kuhusu watu hao utaona kwamba hali zao zilibadilika zikawa bora katika njia ambazo hawakuwazia. Inaweza kuwa hivyo kwako pia. (Mhubiri 11:6) Usikate tamaa!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki