Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 6/15 kur. 8-9
  • Jinsi ya Kuimarisha Uwajibikaji Katika Ndoa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kuimarisha Uwajibikaji Katika Ndoa
  • Amkeni!—2015
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KIKWAZO
  • 1 Ushikamanifu
    Amkeni!—2018
  • Jinsi ya Kuimarisha Ndoa Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Siri ya 2: Kuwajibika
    Amkeni!—2009
  • Wajibika Sikuzote Katika Ndoa Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2015
g 6/15 kur. 8-9
Wenzi wa ndoa wenye furaha wakitembea kwenye barafu

MSAADA KWA AJILI YA FAMILIA | NDOA

Jinsi ya Kuimarisha Uwajibikaji Katika Ndoa

KIKWAZO

Siku ulipofunga ndoa, uliweka nadhiri. Nadhiri hiyo ni uwajibikaji wa kudumu, yaani, kiapo cha kuendelea kushikamana na mwezi wako na kutatua matatizo yoyote yanayojitokeza.

Hata hivyo, kwa miaka mingi, huenda mizozano imeharibu uhusiano wenu. Je, bado unahisi unahitaji kuwajibika kikamili kwa mwezi wako?

MAMBO UNAYOPASWA KUJUA

Wenzi wa ndoa wakiwa wameketi ndani ya mtumbwi uliotia nanga kwenye ufuo

Uwajibikaji ni kama nanga inayoweza kuimarisha ndoa yako

Uwajibikaji ni suluhisho, na sio tatizo. Leo watu wengi hawapendi kuwajibika. Baadhi yao hufananisha uwajibikaji na mzigo mzito. Badala ya kuwa na maoni kama hayo, ona uwajibikaji kuwa nanga inayoweza kuimarisha ndoa yako. Megan, mwanamke aliyeolewa alisema hivi: “Wakati wa mzozano, jambo moja bora kuhusu uwajibikaji ni kujua kwamba wewe na mwenzi wako hamtaachana.”a Kuwa na uhakika kwamba ndoa yako ni salama licha ya kwamba mnakabili changamoto fulani, kunaweza kukupatia msingi wa kutatua matatizo yenu.—Ona sanduku “Uwajibikaji na Ushikamanifu.”

Jambo la hakika: Ikiwa unakabili hali ngumu katika ndoa yako, sasa ndio wakati wa kuimarisha uwajibikaji, wala si kuutilia shaka. Unaweza kufanya hivyo jinsi gani?

MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

Chunguza maoni yako. “Ndoa ya maisha.” Je, maneno hayo hukufanya uhisi umefungwa au uko salama? Matatizo yanapotokea, je, wewe huona kuachana kuwa suluhisho? Ili kuimarisha uwajibikaji, ni muhimu kuona kwamba ndoa ni muungano wa kudumu.—Kanuni ya Biblia: Mathayo 19:6.

Chunguza historia yako. Maoni yako kuhusu uwajibikaji huenda yameathiriwa na mambo uliyoona kwa wazazi wako. Lea, mwanamke aliyeolewa alisema hivi: “Wazazi wangu walitalikiana nilipokuwa mdogo. Nilikuwa na wasiwasi kwamba hali hiyo ingenifanya niwe na maoni yasiyofaa kuhusu uwajibikaji.” Uwe na uhakika kwamba unaweza kufanya mambo kwa njia tofauti kabisa katika ndoa yako. Si lazima urudie makosa ya wazazi wako!—Kanuni ya Biblia: Wagalatia 6:4, 5.

Chunguza usemi wako. Unapokuwa katika hali ya kutoelewana na mwenzi wako, jizuie kusema maneno ambayo baadaye utajutia, kama vile “Nitakuacha!” au, “Nitatafuta mwingine anayenithamini!” Maneno kama hayo huathiri uwajibikaji, na badala ya kutatua tatizo yanakuwa chanzo cha ugomvi wa maneno. Badala ya kutumia usemi wenye kuumiza, unaweza kusema hivi: “Kwa kweli, sote tumeudhika. Tunaweza kufanya nini ili kutatua tatizo hili?”—Kanuni ya Biblia: Methali 12:18.

Onyesha kwamba ‘unaheshimu uwajibikaji.’ Weka picha ya mwenzi wako katika meza ya ofisini mwako. Uwe na maoni yanayofaa kuhusu ndoa yenu unapozungumza na wengine. Weka lengo la kumpigia simu mwenzi wako kila siku unapokuwa mbali naye. Daima tumia usemi “sisi,” na utumie maneno kama “mimi na mke wangu” au “mimi na mume wangu.” Kwa kufanya hivyo, utakazia kwako na kwa wengine kwamba unawajibika kwa mwenzi wako.

Iga mifano mizuri. Iga mifano ya wenzi wa ndoa wenye umri mkubwa na ambao wametatua matatizo ya ndoa kwa mafanikio. Waulize hivi: “Uwajibikaji una umuhimu gani katika ndoa yenu, na umewasaidia jinsi gani katika ndoa?” Biblia inasema hivi: “Chuma hunolewa kwa chuma. Ndivyo mtu anavyounoa uso wa mwingine.” (Methali 27:17) Ukiwa na kanuni hiyo akilini, jitahidi ili unufaike kwa kufuata ushauri wa wale waliofanikiwa katika ndoa.

a Biblia inaruhusu wenzi wa ndoa kuachana ikiwa mwenzi mmoja amefanya uasherati. Ona makala “Maoni ya Biblia—Uzinzi” katika gazeti hili la Amkeni!

MAANDIKO MUHIMU

  • “Kile ambacho Mungu ameunganisha mtu yeyote asikitenganishe.” —Mathayo 19:6.

  • “Kwa maana kila mmoja ataubeba mzigo wake mwenyewe.” —Wagalatia 6:5.

  • “Kuna mtu anayesema bila kufikiri kama kwa upanga unaochoma, lakini ulimi wa mwenye hekima huponya.”—Methali 12:18.

UWAJIBIKAJI NA USHIKAMANIFU

“Ikiwa wewe na mwenzi wako ni washikamanifu, mnaweza kufurahia muungano wenye kudumu. Mnapofikiria miezi, miaka, na makumi ya miaka inayokuja, mnajiona mkiwa pamoja bado. Wazo la kwamba hamngekuwa mmeoana haliingii akilini hata kidogo, na mtazamo huo hufanya ndoa yenu iwe salama. Mke mmoja anasema: ‘Hata ninapomkasirikia [mume wangu] na kuudhiwa na jinsi mambo yalivyo kati yetu, mimi sihangaiki eti ndoa yetu itavunjika. Jambo linalonihangaisha ni jinsi tutakavyorudia uhusiano tuliokuwa nao kabla ya mambo kuharibika. Mimi huwa sina shaka hata kidogo kwamba tutatatua tatizo hilo, ingawa wakati huo sijui jinsi ya kufanya hivyo.’”—Kutoka katika makala ya gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 15, 2003.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki