Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g16 Na. 4 uku. 6
  • 3 Usikate Tamaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 3 Usikate Tamaa
  • Amkeni!—2016
  • Habari Zinazolingana
  • Unaweza Kutimiza Malengo Yako ya Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Kukinza ili Mazoea Mabaya Yasirudi
    Amkeni!—1992
  • Acha Mazoea Yakunufaishe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Jinsi ya Kusitawisha Mazoea Mazuri
    Amkeni!—2016
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2016
g16 Na. 4 uku. 6
Mwanamke akiweka alama kwenye kalenda

HABARI KUU | JINSI YA KUSITAWISHA MAZOEA MAZURI

3 Usikate Tamaa

Kalenda iliyowekwa alama

Inasemekana kwamba mtu anaweza kuzoea tabia mpya kwa siku 21. Hata hivyo, utafiti unaonyesha kwamba huenda baadhi ya watu wakatumia muda mfupi kuzoea jambo fulani ilhali wengine wakatumia muda mrefu. Je, hilo linapaswa kukuvunja moyo?

Hebu fikiria hali hii: Tuseme kwamba unataka kusitawisha mazoea ya kufanya mazoezi mara tatu kwa juma.

  • Juma la kwanza, unafaulu kufikia lengo lako.

  • Juma la pili, unakosa kufanya mazoezi kwa siku moja.

  • Juma la tatu, unafaulu tena.

  • Juma la nne, unashindwa kufanya mazoezi hata kwa siku moja.

  • Juma la tano, unafaulu tena, na kuanzia hapo unatimiza lengo lako kila juma.

Imechukua majuma matano kuzoea hali hiyo mpya. Huenda huo ukaonekana kuwa muda mrefu, hata hivyo, mara tu unapofikia lengo lako unafurahi kwamba ulisitawisha zoea zuri.

KANUNI YA BIBLIA: “Huenda mwadilifu akaanguka hata mara saba, naye hakika atasimama.”—Methali 24:16.

Biblia inatutia moyo tusikate tamaa. Haijalishi tutashindwa mara ngapi lakini jambo la maana ni kufikia malengo yetu.

Haijalishi tutashindwa mara ngapi lakini jambo la maana ni kufikia malengo yetu

MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

  • Kumbuka kwamba kuteleza si kuanguka. Tarajia kupata vizuizi unapojitahidi kufikia malengo yako.

  • Kumbuka wakati ulipofikia malengo yako. Kwa mfano, ikiwa unajaribu kuboresha njia ya kuwasiliana na watoto wako, jiulize hivi: ‘Ni wakati gani nilipotaka kuwafokea watoto wangu lakini nikajizuia kufanya hivyo? Nilifanya nini? Ninawezaje kufanya hivyo tena?’ Maswali kama hayo yanaweza kukusaidia uimarishe azimio lako la kutaka kufanikiwa badala ya kukazia fikira makosa.

Je, ungependa kujua jinsi ambavyo kanuni za Biblia zinaweza kukusaidia kushughulikia mambo mengine maishani kama vile, mahangaiko, kuwa na maisha ya familia yenye furaha na jinsi ya kuwa na furaha ya kweli? Zungumza na Mashahidi wa Yehova, au tembelea tovuti yetu ya jw.org/sw.

KANUNI ZA BIBLIA ZINAZOHUSIKA

“Macho yako yenye kung’aa yanapaswa kutazama mbele yako moja kwa moja.”—Methali 4:25.

“Nayasahau mambo ya nyuma na kujinyoosha kwenda mbele kuelekea mambo yaliyo mbele, ninafuatilia kuelekea ule mradi.” —Wafilipi 3:13, 14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki