Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g17 Na. 3 uku. 16
  • Manyoya ya Fisi Maji wa Baharini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Manyoya ya Fisi Maji wa Baharini
  • Amkeni!—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Yaliyomo
    Amkeni!—2017
  • Nyumba Zenye “Makoti ya Manyoya”
    Amkeni!—2005
  • Ulimi wa Paka
    Je, Ni Kazi ya Ubuni?
  • Bahari Isiyo na Kifani—Lakini Imekufa!
    Amkeni!—2008
Amkeni!—2017
g17 Na. 3 uku. 16
Fisi maji wa baharini

JE, NI KAZI YA UBUNI?

Manyoya ya Fisi Maji wa Baharini

WANYAMA wengi wanaoishi katika maji ya baridi wana tabaka jembamba la mafuta lililo ndani ya ngozi linalowasaidia kudumisha joto. Lakini fisi maji wa baharini hutumia mbinu nyingine. Yeye hutegemea manyoya yake yaliyobanana.

Fikiria jambo hili: Manyoya ya fisi wa baharini yamebanana zaidi kuliko ya mnyama mwingine yeyote. Ana manyoya karibu milioni moja katika kila inchi ya mraba (155,000 kwa kila sentimita ya mraba). Anapoogelea, manyoya yake huungana na kufanyiza tabaka la hewa katikati ya manyoya na ngozi yake. Hivyo, tabaka hilo la hewa huwa kama koti linalomkinga, kwa kuzuia maji ya baridi kugusa moja kwa moja ngozi yake na hivyo kuathiri joto la mwili.

Wanasayansi wanaamini kwamba kuna jambo tunaloweza kujifunza kutokana na manyoya ya fisi maji wa baharini. Wamejaribu kuiga kwa kutengeneza makoti yaliyo na manyoya yenye urefu mbalimbali, na manyoya yaliyobanana au kuachiana nafasi. Watafiti wamefikia mkataa wa kwamba, “kadiri manyoya yanavyobanana na kuwa marefu, ndivyo inavyokuwa vigumu zaidi kwa maji kupita.” Hilo ni sawa na kusema kwamba, fisi maji wa baharini ana koti bora sana.

Watafiti wanatumaini kwamba utafiti wao utasaidia kuboresha teknolojia ya kubuni na kutokeza vitambaa visivyoweza kupenya maji. Huenda hili likachochea watu fulani wafikirie kwamba ni bora wale wanaopiga mbizi kwenye maji ya baridi wavae mavazi yenye manyoya, kama vile fisi maji wa baharini!

Una maoni gani? Je, mfumo wa kutunza hewa ndani ya manyoya ya fisi maji ulijitokeza wenyewe? Au ulibuniwa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki