Kitabu cha Kale Kinachotunufaisha Leo
Watu wengi wanaiheshimu Biblia kwa sababu ni kitabu kitakatifu. Na ingawa Biblia inatufundisha jinsi ya kumwabudu Mungu, ina manufaa mengi zaidi. Ina ushauri mzuri unaoweza kutusaidia maishani.
Kwa mfano, fikiria mambo ambayo baadhi ya watu wamesema kuhusu manufaa waliyopata kwa kusoma na kutumia ushauri wa Biblia katika maisha yao.
“Maisha yangu yamekuwa bora. Ninahisi nimetulia kiakili na kihisia. Sasa nina furaha zaidi.”—Fiona.
“Kujifunza Biblia kumenisaidia kujua kusudi la maisha.”—Gnitko.
“Maisha yangu yamebadilika na kuwa bora zaidi. Sasa ninatumia muda mwingi pamoja na familia yangu.”—Andrew.
Hiyo ni mifano michache tu. Ulimwenguni pote, watu wengi wametambua kwamba Biblia ina ushauri mwingi unaotusaidia katika maisha ya kila siku.
Acheni tuchunguze jinsi Biblia inavyoweza kuwasaidia watu kuboresha . . .
Afya
Hali ya kihisia
Uhusiano wa familia na marafiki
Matumizi ya pesa
Uhusiano na Mungu
Makala zinazofuata zitatusaidia kuona kwamba ingawa Biblia ni kitabu kitakatifu, kinaweza pia kutusaidia katika nyanja mbalimbali maishani.