Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g20 Na. 2 kur. 6-7
  • Je, Tunapaswa Kumlaumu Mungu Tunapoteseka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Tunapaswa Kumlaumu Mungu Tunapoteseka?
  • Amkeni!—2020
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini ni Muhimu Kupata Jibu la Swali Hilo?
  • Jambo la Kufikiria
  • Mambo Ambayo Biblia Inafundisha
  • Yaliyomo
    Amkeni!—2020
  • Biblia Inasema Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Swali la 3: Kwa Nini Mungu Anaruhusu Niteseke?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2020
g20 Na. 2 kur. 6-7
Kasisi ameinua Biblia anapoongoza ibada ya mazishi kanisani.

1. Je, Tunapaswa Kumlaumu Mungu Tunapoteseka?

Kwa Nini ni Muhimu Kupata Jibu la Swali Hilo?

Watu wengi wanakataa kumwabudu Mungu kwa sababu wanafikiri kwamba anasababisha kuteseka.

Jambo la Kufikiria

Iwe ni moja kwa moja au la, viongozi wengi wa dini wamefundisha kwamba Mungu husababisha wanadamu wateseke. Kwa mfano, baadhi yao husema hivi:

  • Majanga ya asili ni adhabu kutoka kwa Mungu.

  • Watoto wadogo hufa kwa sababu Mungu anahitaji kuongeza malaika mbinguni.

  • Mungu anaunga mkono upande fulani katika vita, na sikuzote vita husababisha watu wengi wateseke.

Lakini je, inawezekana kwamba viongozi wa dini hawafundishi ukweli kumhusu Mungu? Ikiwa Mungu hakubaliani na mambo wanayofundisha, je tunaweza kuwaamini?

JIFUNZE MENGI ZAIDI

Tazama video Kwa Nini Ujifunze Biblia? kwenye jw.org/sw.

Mambo Ambayo Biblia Inafundisha

Mungu hasababishi kuteseka.

Ikiwa anasababisha tuteseke, basi anatenda kinyume na sifa zake zinazotajwa kwenye Biblia. Kwa mfano:

“Njia zake zote ni haki. . . . Yeye [Mungu] ni mwadilifu na mnyoofu.”​—KUMBUKUMBU LA TORATI 32:4.

“Mungu wa kweli hawezi kamwe kuwazia kutenda uovu, na Mweza-Yote hawezi kamwe kutenda kosa!”​—AYUBU 34:10.

“Mweza-Yote hapotoshi haki.”​—AYUBU 34:12.

Mungu anazikataa dini zote zisizofundisha ukweli kumhusu.

Dini hizo zinatia ndani zile zinazofundisha kwamba Mungu anasababisha kuteseka, na pia zile zinazounga mkono vita au jeuri.

“Manabii wanatabiri uwongo katika jina langu. Sikuwatuma wala kuwaamuru wala kuzungumza nao. Wanawatabiria ninyi maono ya uwongo na . . . udanganyifu wa moyo wao wenyewe.”​—YEREMIA 14:14.

Yesu alishutumu unafiki wa dini.

“Si kila mtu anayeniambia, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, bali yule anayefanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni ndiye atakayeingia. Wengi wataniambia siku hiyo: ‘Bwana, Bwana, je, hatukutoa unabii katika jina lako, na kufukuza roho waovu katika jina lako, na kufanya matendo mengi yenye nguvu katika jina lako?’ Ndipo nitakapowaambia: ‘Sikuwajua ninyi kamwe! Ondokeni kwangu, ninyi mnaotenda uasi sheria!’”​—MATHAYO 7:21-23.

Je, tunapaswa kumlaumu Mungu tunapoteseka?

Wazia kwamba baba anawalea vizuri watoto wake na kuwapa mahitaji yao yote. Baada ya muda, mtoto wake mmoja anaasi, anaondoka nyumbani na kuamua kuishi maisha ya anasa. Je, baba anapaswa kuwajibika kwa sababu ya mwenendo wa mtoto wake? Ikiwa mtoto huyo atapatwa na mambo mabaya, je, anapaswa kumlaumu baba yake? Vivyo hivyo, hatupaswi kumlaumu Mungu kwa sababu ya mambo mabaya yanayotupata.

Je, hilo linamaanisha kwamba tunapaswa kujilaumu tunapoteseka?

Utapata jibu kwenye swali la 2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki