Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g21 Na. 3 kur. 8-9
  • Mambo Ambayo Wanasayansi Hawajui

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mambo Ambayo Wanasayansi Hawajui
  • Amkeni!—2021
  • Habari Zinazolingana
  • Mtaalamu wa Biolojia ya Viini-Tete Anaeleza kwa Nini Anamwamini Mungu
    Amkeni!—2016
  • Chanzo cha Ulimwengu na Uhai Ni Nini?
    Amkeni!—2002
  • Jinsi Sayansi Inavyoathiri Maisha Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Muumba Aweza Kufanya Maisha Yako Yawe na Maana Zaidi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2021
g21 Na. 3 kur. 8-9
Mwalimu wa sayansi akijadiliana na baadhi ya wanafunzi wake.

Mambo Ambayo Wanasayansi Hawajui

Inaonekana ni kana kwamba wanasayansi wamejifunza kila kitu kuhusu ulimwengu. Hata hivyo, bado kuna maswali mengi ambayo hawawezi kujibu.

Je, wanasayansi wanajua jinsi ulimwengu na uhai ulivyoanza? Jibu rahisi ni hapana. Baadhi ya watu husema kwamba wanasayansi wanaojifunza kuhusu ulimwengu wanaweza kufafanua chanzo cha ulimwengu. Hata hivyo, Marcelo Gleiser, profesa wa elimu ya nyota katika chuo cha Dartmouth, ambaye anaamini kwamba mambo ya Mungu hayawezi kujulikana, anasema hivi: “Hatujawahi kufafanua chanzo cha ulimwengu hata kidogo.”

Vivyo hivyo, makala moja kwenye gazeti la Science News inasema hivi kuhusu chanzo cha uhai: “Huenda haiwezekani kujua kihususa jinsi uhai ulivyoanza duniani: Miamba mingi na mabaki ya vitu vya kale ambavyo vingetusaidia kujua jinsi Dunia ilivyokuwa mwanzoni vimepotea muda mrefu uliopita.” Maelezo hayo yanaonyesha bado sayansi haijajibu swali hili, Ulimwengu na uhai ulianzaje?

Lakini huenda ukajiuliza, ‘Ikiwa viumbe hai vilivyomo duniani vilibuniwa, ni nani aliyevibuni?’ Inawezekana umejiuliza pia maswali yafuatayo: ‘Ikiwa kuna Muumba mwenye hekima na upendo, kwa nini anaruhusu wanadamu aliowaumba wateseke? Kwa nini anaruhusu kuwe na aina nyingi za ibada zinazopingana? Kwa nini anawaruhusu waabudu wake wafanye mambo mengi mabaya?’

Sayansi haiwezi kujibu maswali hayo. Lakini hilo halimaanishi kwamba huwezi kupata majibu yenye kuridhisha. Kwa kweli, watu wengi wamepata majibu yenye kuridhisha katika Biblia.

Ikiwa ungependa kujua kwa nini baadhi ya wanasayansi walioamua kujifunza Biblia wanaamini kwamba kuna Muumba, tembelea tovuti ya jw.org/sw. Tafuta kwenye “maoni kuhusu chanzo cha uhai.”

Walipata uthibitisho kutoka kwenye sayansi na Biblia

Georgiy N. Koidan, mkemia

“Kazi yangu inahusisha ‘kuchanganya’ kemikali mbalimbali ili kutengeneza molekuli. Unahitaji kupanga mapema hatua mbalimbali utakazopitia unapochanganya kemikali hizo. Ikiwa utasahau hatua moja tu, molekuli yote inaweza kuharibika. Ingawa kazi yangu ni ngumu na inahitaji umakini sana, ni rahisi sana unapoilinganisha na maelfu ya utendaji wa kemikali unaotokea ndani ya chembe za viumbe hai ili kutokeza molekuli tata. Hilo linanifanya niamini kwamba kuna Mkemia Mkuu, yaani, Muumba.

“Nilipojifunza Biblia, nilitambua kwamba hiki si kitabu cha kawaida. Uandikaji wa Biblia ulikamilika karibu miaka 2,000 iliyopita, lakini ninahisi kwamba ushauri wake una manufaa sana leo pia. Ushauri wake una matokeo mazuri tunapoutumia kutatua matatizo ndani ya familia, kazini, na pamoja na jirani zetu. Nilifikia mkataa kwamba ushauri wenye kuaminika kama huo lazima utoke kwa mtu mwenye hekima ya hali ya juu zaidi kuliko wanadamu.”

Yan-Der Hsuuw, mtaalamu wa viinitete

“Ili kiinitete kikue, chembe zote za mwili zinahitaji kushirikiana, na kubadili chembe fulani ziwe tishu za neva, misuli, mifupa, damu, na tishu nyingine na hatimaye kutokeza kiumbe kamili. Bado hatuelewi jinsi chembe zinavyobadilika kuwa kiinitete. Maoni yangu ni kwamba uhai umetokana na Muumba mwenye akili nyingi sana.

“Ninafikiri ukuaji wa kiinitete ndani ya tumbo la uzazi la mama, kama inavyoelezwa kwenye Biblia katika Zaburi 139:15, 16, unafanana na uvumbuzi wa kisayansi wa hivi karibuni. Maelezo hayo sahihi yangewezaje kuandikwa zamani hivyo ikiwa mwandishi hakufunuliwa na Muumba?”

Tazama video yenye kichwa Rocío Picado Herrero: A Chemistry Teacher Explains Her Faith katika Kiingereza. Tafuta video hiyo kwa kuandika kichwa chake kwenye tovuti ya jw.org.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki