Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g21 Na. 3 kur. 10-13
  • Biblia Inatufundisha Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia Inatufundisha Nini?
  • Amkeni!—2021
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mambo Ambayo Biblia Haifundishi
  • Mungu Alianza Lini Kuumba Ulimwengu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Je, Sayansi Inapingana na Masimulizi ya Mwanzo?
    Amkeni!—2006
  • Ukweli Kuhusu Simulizi la Uumbaji
    Amkeni!—2014
  • Sayansi na Kitabu cha Mwanzo
    Uhai—Ulitokana na Muumba?
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2021
g21 Na. 3 kur. 10-13

Biblia Inatufundisha Nini?

“Hii ndiyo historia ya mbingu na dunia wakati zilipoumbwa.” (Mwanzo 2:4) Kwa maneno hayo, Biblia inaeleza kwa ufupi jinsi sayari yetu ilivyotokea. Je, mambo ambayo Biblia inasema yanapatana na ukweli wa kisayansi? Fikiria mifano hii michache.

Mwanzo: Mbingu na dunia zinaumbwa

Je, ulimwengu umekuwepo sikuzote?

Mwanzo 1:1 inasema: “Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.”

Mpaka kufikia katikati ya karne ya 20, wanasayansi wengi mashuhuri waliamini kwamba ulimwengu umekuwepo sikuzote. Lakini kwa kutegemea uvumbuzi wa hivi karibuni, wanasayansi wengi sasa wanakubali kwamba ulimwengu una mwanzo.

Dunia ilikuwaje mwanzoni?

Mwanzo 1:2, 9 inasema mwanzoni dunia “haikuwa na umbo nayo ilikuwa tupu,” ikiwa imefunikwa na maji.

Maneno hayo yanapatana na utafiti wa hivi karibuni wa kisayansi. Mtaalamu wa biolojia, Patrick Shih, anasema kwamba sayari yetu ilianza ikiwa na “anga lisilo na hewa ya oksijeni . . . na ilikuwa na ardhi yenye mwonekano wa ajabu.” Gazeti la Astronomy linaripoti hivi: “Utafiti mpya unaonyesha kwamba zamani dunia yote ilikuwa imejaa maji na ilikuwa na sehemu ndogo sana ya ardhi iliyoonekana.”

Baada ya muda, angahewa lilibadilikaje?

Mwanzo 1:3-5 inaonyesha kwamba mwanga ulipoanza kupenya angahewa, chanzo chake hakingeweza kuonekana duniani. Ni baada ya muda fulani kupita, ndipo mwezi na jua vingeweza kuonekana kutoka duniani.—Mwanzo 1:14-18.

Biblia haisemi kwamba viumbe hai vyote duniani viliumbwa kwa siku sita zenye saa 24.

Kituo kimoja cha utafiti (Smithsonian Environmental Research Center) kinasema kwamba mwanzoni angahewa la sayari yetu liliruhusu kiwango kidogo sana cha mwanga kifike duniani. Watafiti hao wanasema: “Ukungu mzito wa gesi ya Methani uliifunika dunia nzima.” Baadaye, “ukungu huo wa gesi ya methani ukaondoka na anga likawa la bluu.”

Viumbe wa duniani waliumbwa kwa mpangilio gani?

1​—Siku ya Kwanza: Mwanga hafifu unapenya kwenye anga la dunia.​—Mwanzo 1:3-5

2​—Siku ya Pili: Dunia imefunikwa na maji na utando mzito wa mvuke. Vitu hivyo viwili vimetengenishwa na kuna nafasi kati ya vitu hivyo.​—Mwanzo 1:6-8

3​—Siku ya Tatu: Maji yaliyo duniani yanapungua na nchi kavu inatokea.​—Mwanzo 1:9-13

4​—Siku ya Nne: Jua na mwezi ungeweza kuonekana kutoka duniani. ​—Mwanzo 1:14-19

5​—Siku ya Tano: Mungu anaumba viumbe wa kwenye maji na wanaoruka angani wakiwa na uwezo wa kuzaliana kulingana na aina zao.​—Mwanzo 1:20-23

6​—Siku ya Sita: Wanyama wanaumbwa, wakubwa kwa wadogo. Siku ya sita inamalizika kwa kuumbwa kwa wanadamu wawili wa kwanza.​—Mwanzo 1:24-31

Mwanzo 1:20-27 inaeleza kwamba samaki walianza kuumbwa, wakafuata ndege, kisha wanyama na mwishowe wanadamu. Wanasayansi wanaamini kwamba samaki wa kwanza walitokea muda mrefu kabla ya wanyama wa kwanza, na kwamba wanadamu walitokea muda mrefu baadaye.

Biblia haisemi kwamba haiwezekani kwa viumbe hai kubadilika baada ya muda fulani kupita

“Ingawa simulizi la Biblia kwenye Mwanzo sura ya kwanza ni fupi, lakini inashangaza jinsi maneno hayo na muda unaotajwa unavyopatana na uvumbuzi wa kisasa wa kisayansi.”​—Gerald L. Schroeder, mtaalamu wa fizikia.

Mambo Ambayo Biblia Haifundishi

Baadhi ya watu wanadai kwamba Biblia haipatani na utafiti wa kisasa wa kisayansi. Hata hivyo, mara nyingi wanatoa madai hayo kwa sababu hawaelewi mambo ambayo Biblia inafundisha.

Biblia haisemi kwamba ulimwengu au dunia imekuwepo kwa miaka 6,000 tu. Badala yake, inasema kwamba dunia na ulimwengu uliumbwa “hapo mwanzo.” (Mwanzo 1:1) Biblia haielezi kihususa muda ambao dunia na ulimwengu umekuwepo.

Biblia haisemi kwamba viumbe hai vyote duniani viliumbwa kwa siku sita zenye saa 24. Badala yake inatumia neno “siku” kurejelea kipindi fulani cha wakati. Kwa mfano, inasema kwamba uumbaji wa sayari yetu na viumbe hai​—katika zile siku sita za uumbaji zinazotajwa kwenye Mwanzo sura ya kwanza—​ulitokea katika kipindi cha wakati kinachoitwa “siku ambayo Yehovaa Mungu aliumba dunia na mbingu.” (Mwanzo 2:4) Hivyo, kila siku moja kati ya zile siku sita ambazo Mungu alitumia kuandaa dunia na kuumba viumbe hai, inaweza kuwakilisha kipindi kirefu sana cha wakati.

Biblia haisemi kwamba haiwezekani kwa viumbe hai kubadilika baada ya muda fulani kupita. Kitabu cha Mwanzo kinasema kwamba wanyama waliumbwa “kulingana na aina zao.” (Mwanzo 1:24, 25) Neno “aina” linalotajwa katika Biblia si la kisayansi, lakini inaonekana linarejelea makundi mbalimbali makubwa ya viumbe hai. Hivyo, “aina” moja inaweza kutia ndani jamii nyingi, mbalimbali, za wanyama au mimea yenye tabia fulani zinazofanana. Ufafanuzi huu unaonyesha kwamba inawezekana mabadiliko yalitokea kati ya wanyama au mimea mbalimbali iliyo katika “aina” moja na iliyokuwa katika eneo lilelile.

Una maoni gani?

Kama tulivyoona, Biblia inafafanua kwa njia rahisi na iliyo sahihi mwanzo wa ulimwengu, jinsi dunia ilivyoonekana mwanzoni, na jinsi viumbe hai walivyotokea. Je, inawezekana pia Biblia imemtambulisha kwa usahihi Yule aliyeumba vitu hivyo vyote? Encyclopædia Britannica inasema: “Kwa ujumla, wazo la kwamba uhai ulitokana na chanzo fulani chenye nguvu zinazopita za wanadamu halipingani na uvumbuzi wa kisasa wa kisayansi.”b

Fikiria hili:

Soma Mwanzo 1:1–2:4. Mambo ambayo Biblia inasema kuhusu uumbaji ni tofauti sana na hekaya za watu wa kale kuhusu uumbaji. Kwa mfano, Wababiloni waliamini kwamba ulimwengu na wanadamu waliumbwa kutokana na maiti ya mungu wa kike na damu ya mungu wa kiume. Wamisri wa kale walifikiri kwamba wanadamu waliumbwa kutokana na machozi ya mungu Ra. Nchini China, baadhi ya watu waliamini kwamba maiti ya mtu fulani mkubwa sana ilibadilika na kuwa nguvu za asili za dunia na kwamba wanadamu walitokana na chawa waliotoka kwenye mwili wake. Je, unafikiri simulizi la kwenye kitabu cha Mwanzo ni mojawapo ya hekaya hizo? Au linapatana na sayansi?

Tazama video ya dakika nne yenye kichwa Je, Ulimwengu Uliumbwa? Tafuta video hiyo kwa kuandika kichwa chake kwenye tovuti ya jw.org/sw.

a Yehova ni jina la Mungu kama linavyoonyeshwa kwenye Biblia.

b Encyclopædia Britannica haisemi kwamba viumbe hai viliumbwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki