Sura ya 4
Sababu Kwanini Tunazeeka na Tunakufa
1. (a) Ni tamaa gani ya watu wa kawaida kuhusu afya na uzima? (b) Kwa sababu maradhi na mauti viko kila mahali, kunaulizwa maswali gani juu ya kusudi la Mungu kwa wanadamu?
KILA mtu wa kawaida hutamani uzima na afya njema. Tunatafuta kitulizo cha maumivu na mateso ambayo maradhi huleta na tunatamani njia fulani ya kuepukana na matokeo yenye kudhoofisha ambayo uzee huleta juu ya miili yetu. Hutuumiza sisi, pia, wakati tunapowaona wale tuwapendao wakiteswa na mambo haya. Kwa sababu ya hii, watu wengi huuliza, “Je! yote haya yalikuwa sehemu ya kusudi la Mungu la kwanza? Wakati Mungu alipoumba wanadamu je! lilikuwa kusudi lake kwamba ni lazima wanadamu wazeeke, na kuwa viziwi au vipofu? Je! yeye alitaka ngozi ya wanadamu iwe na makunyanzi ya uzee, moyo wake uwe wenye maradhi na viungo vyake vingine vivunjike? Kweli, je! Mungu aliwaumba wanadamu wapate kufa?”
2. (a) Je! Mungu aliumba wanadamu na hitilafu yo yote? (b) Basi, ni tumaini gani ambalo Mungu aliwapa Adamu na Hawa?
2 La, Yehova Mungu hakuumba wanadamu kwa wakati ujao wa namna hiyo wenye huzuni. Biblia hutuambia sisi kwamba Yehova alitayarisha maskani nzuri ya bustani kwa wanadamu wawili wa kwanza, naye akawabarikia. Kwa kuchunguza kazi yake ya kuumba, kwa haki Mungu aliitangaza kuwa “chema sana.” (Mwanzo 1:28, 31) Hii inamaanisha kwamba Adamu na Hawa waliumbwa wakamilifu, bila hitilafu katika akili au mwili. (Kumbukumbu la Torati 32: 4; Mithali 10:22) Walikuwa na tumaini la kuishi milele.
3. Wataalamu wa sayansi husema nini juu ya kuwezekana kwa uzima wa wanadamu?
3 Kwa kupendeza, wataalamu wa sayansi ya kisasa wanajua kwamba mwili wa binadamu hujifanya wenyewe upya sikuzote. Na wao husema kwamba, ukiwa chini ya hali sahihi, unaweza kuishi milele. Mshindi wa Zawadi ya Nobel, Dr. Linus Pauling, alieleza kwamba nyama za mwili wa mwanadamu hujirudisha zenyewe mahali pa zile zinazoharibika na, kwa kubahatisha, zapaswa ziendelee kufanya hivyo milele. Mtaalamu wa biochemistry William Beck alisema pia: “Siwezi kuona sababu kwa nini mauti, katika asili ya vitu, lazima iwe isiyoepukika.” Lakini, ijapokuwa kuumbwa hivyo, wanadamu huendelea kuzeeka na kufa. Kwa nini? Neno la Mungu Biblia hutupa sisi jibu lenye kutosheleza.
MATOKEO YA KUTOKUTII
4. Ni jaribu gani ambalo Mungu aliweka juu ya Adamu na Hawa, kutia mkazo wa uzito wa utii?
4 Wakati Yehova alipomwumba Adamu na Hawa, walikuwa sehemu ya kidunia ya jamaa kubwa ya Mungu ambayo ilikwisha kutia ndani yake hesabu kubwa ya viumbe vya kiroho katika mbingu. Mungu alikuwa ndiye Baba wa wanadamu wawili, kwa kuwa ndiye aliyekuwa amewapa uzima. Walakini, karama ya uzima, ilikuwa yenye masharti; yaani, ingeendelea kuwa yao kwa kadiri walivyotimiza masharti tu ya utii wa upendo kwa Baba yao wa mbinguni. Utii wa sheria ni wa lazima kwa amani na utaratibu mzuri wenye kuendelea, hivyo iliwabidi wamtambue Mungu kama Mtawala wao Mkuu kupita wote. Je! wao walijua jambo hili? Ndiyo, kwa sababu Yehova aliweka jaribu juu yao lililotia mkazo uzito wa utii. Yeye akasema kwa Adamu: “Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.” —Mwanzo 2:16, 17.
5. (a) Je! jaribu la utii wa Adamu na Hawa lingeweka shida juu yao? (b) Kwa nini ‘tunda lililokatazwa’ halikuwa ngono?
5 Jaribu hili la utii halikuwa gumu. Hawakunyimwa chakula kilichohitajiwa, wala hawakujaribiwa kupita uwezo wao. Walakini, utii wao ungeonyesha kwamba walithamini uhusiano wao na Mungu. (1 Yohana 5:3) Ijapokuwa watu wengine wana wazo la kwamba ‘tunda lililokatazwa’ lilishughulika na ngono baina ya mwanamume na mwanamke, hii haikuwa hivyo. Mungu mwenyewe alikuwa amekwisha kuwaambia “zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi.” (Mwanzo 1:28) Wakati Mungu alipowaamuru wasile tunda la mti fulani ilikuwa na maana tu kwamba Mungu alitenga mmojawapo wa miti mingi yenye matunda ya Edeni na akawaamuru wanadamu wawili wasile baadhi ya matunda yake.
6. (a) Kwa nini mti uliitwa “mti wa ujuzi wa mema na mabaya”? (b) Wakati Adamu na Hawa walipokula tunda, ni jambo gani baya ambalo walikuwa wakilifanya kuhusu Baba yao wa mbinguni?
6 Kwa nini mti uliitwa “mti wa ujuzi wa mema na mabaya”? Kwa sababu, kama matokeo ya amri ya Mungu, matunda yake yalifananisha haki ya Mungu kuamua kwa viumbe vyake yaliyo “mema” na yaliyo “mabaya” kwao. Basi, kwa wanadamu wawili kula baadhi ya matunda haya ingekuwa na maana kwamba wao walikuwa wakimpa Baba yao wa mbinguni visogo vyao na kuukataa uongozi wake wa kimungu na mapenzi makamilifu. Ijapokuwa ni rahisi, jaribu lilitia ndani mengi. Lilitia ndani tegemeo la wanadamu juu ya Muumba wao na utambuzi wa wanadamu wa mamlaka ya kimungu. Kumbuka, pia, kwamba Yesu Kristo alitumia kwa wanadamu wasiokamilika kanuni ya kwamba “aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.” (Luka 16:10) Jinsi hili lilivyohusu zaidi sana viumbe vikamilifu!
7. (a) Kiumbe kisichoonekana, kikisema kupitia kwa nyoka, kilimwambia Hawa nini juu ya tunda la mti? (b) Basi Hawa alifanya nini, na mumewe alipojua, alifanya nini?
7 Kwa nini Hawa alivunja sheria ya Mungu na aka-la baadhi ya matunda? Wazo halikuanzia na yeye bali lilitolewa kwake kwa njia ya kiumbe cha kiroho kikitumia nyoka wa vivi hivi ili kusema kupitia kwa yeye. Kiumbe hicho cha kiroho, kikitambulishwa katika Biblia kama Shetani Ibilisi, kwa hiyo huitwa “nyoka wa zamani.” (Ufunuo 12:9) Kiumbe kisichoonekana kikisema kupitia kwa nyoka kilikana waziwazi kweli amri ya Mungu ambayo Hawa alitumia maneno yake. Yeye alionyesha tunda la mti kuwa laweza kumfanya yeye kuwa kama Mungu, akijiamulia mwenyewe yaliyokuwa “mema” na yaliyokuwa “mabaya.” Ndipo Hawa alipoanza kulitazama tunda kama lenye kutamanika sana naye akamwasi Mungu kwa kula baadhi yake. Adamu, mumewe na kichwa chake, alipojua jambo ambalo alikuwa amelifanya, hakuupinga mwendo wake bali akajiunga naye katika huo.—Mwanzo 3:1-6; Yakobo 1:14, 15; 1 Wakorintho 11 : 3.
8. (a) Kwa tendo lao la uvunjaji wa sheria, Adamu na Hawa walikuwa na hatia ya nini? (b) Kwa nini haitupasi kuhukumu uzito wa jambo ambalo Adamu na Hawa walifanya kwa njia ambayo watu hutazama kutokutii na wivi leo?
8 Kwa tendo hili la uvunjaji wa sheria wakawa na hatia ya dhambi, na hivyo wakajiletea wenyewe adhabu ya dhambi. (1 Yohana 3:4) Katika kutafakari haki ya uamuzi wa Mungu tusifanye kosa la kuhukumu uzito wa jambo ambalo Adamu na Hawa walifanya kwa njia ambayo watu wengi hutazama mambo katika wakati wetu. Leo kutokutii wazazi kumeenea, mara nyingi kuachwa bila kuadhibiwa. Pia wivi umeenea, na wengi hufikiri ya kwamba, ikiwa kinachoibwa ni kidogo, si kitu sana kuiba. Uasi na kusema kinyume cha mamlaka vilevile hufanywa mara kwa mara leo. Lakini jambo hilo halifanyi mambo haya haki! Mengi ya matokeo maovu tuyaonayo leo katika aina ya ukaidi unaoongezeka na uvunjaji wa sheria ni kwa sababu ya wazazi na wengine katika mamlaka kutokusahihisha mambo mwanzoni.—Mithali 13:24; Mhubiri 8:11.
9. (a) Kutafakari jambo ambalo Adamu na Hawa wallfanya kweli, kwa nini Mungu alijiwia mwenyewe na jamaa yake ya ulimwengu wate kuthibitisha sheria? (b) Ni adhabu gani ambayo watu wawili wavunjaji wa sheria walipata kwa dhambi yao?
9 Mungu hakutaka kutia moyo kufanya makosa kwa kutokufikiliza sheria yake mwenyewe. Kwa kutokutii kwao Adamu na Hawa walionyesha ukosefu mkubwa wa upendo kwa Yeye aliyekuwa amewaruzuku sana kwa ajabu. Walikuwa na hatia ya wivi, kwa sababu walikichukua kile ambacho Muumba wao alisema hakikuwa chao. Hata kwa ubaya zaidi, walijiunga na adui wa Mungu na, kwa matendo yao, wakamwita Mungu mwongo. Yehova alijiwia mwenyewe na jamaa yake yote ya ulimwengu wote kuthibitisha sheria yake. Alifanya jambo hili. Kama matokeo ya dhambi yao ya makusudi watu wawili wavunja sheria walifukuzwa kutoka katika Edeni wapate kufa.—Mwanzo 3: 22-24.
10. Jinsi gani matokeo ya dhambi yawezavyo kufananishwa na kipande cha mashine, na dhambi iliwaongoza Adamu na Hawa kwenye matokeo gani?
10 Matokeo ya dhambi juu yao yaweza kufananishwa na jambo linalotokea kwa kipande cha mashine nzuri wakati haitumiwi vizuri, kupatana na maagizo ya fundi. Mashine itatokeza udhaifu na, wakati fulani, kuvunjika. Vivyo hivyo, kama matokeo ya kutojali maagizo ya Muumba wao, Adamu na Hawa walipoteza ukamilifu wao. Akili zao na miili yao ilianza kuvunjika, na hatimaye ikaacha kufanya kazi, katika mauti. Hivyo ndivyo kutokutii na kuondolewa kwenye kibali cha Mungu kulivyomaanisha kwao. (Mwanzo 3:16-19) Baada ya Adamu alipokuwa amekwisha kuitumia nguvu yote ya mwili wake ambao hapo kwanza ulikuwa mkamilifu, yeye akafa akiwa mwenye umri wa miaka 930. Hii ilikuwa kabla ya kumalizika kwa “siku” ya mfano yenye miaka elfu ambayo Mungu alikuwa ameweka.—Mwanzo 5:5; 2 Petro 3:8.
MATOKEO JUU YA WATOTO
11. Jinsi gani Biblia hueleza sababu kwa nini sisi leo tunakuwa wagonjwa na tunakufa?
11 Lakini, kwa kuwa sisi leo hatukuasi sheria hiyo katika Edeni, kwa nini nasi pia tunakuwa wagonjwa na tunakufa? Ni kwa sababu hii: Wote wa watoto wa Adamu walizaliwa baada ya kutokutii kwake. Hivyo watoto wake wakarithi dhambi na mauti kutoka kwake. Watu wote hurithi kutokukamilika, kwa sababu wote wanatoka kwa Adamu na Hawa. Kama vile kitabu cha Biblia cha Ayubu kituambiavyo: “Ni nani awezaye kutoa kitu kilicho safi kitoke katika kitu kichafu? hapana awezaye.” (Ayubu 14:4) Pia, katika Warumi 5:12 Biblia hueleza: “Kwa mtu mmoja [Adamu] dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi.” Kama vile kipande kikamilifu cha mashine hakiwezi kufanyizwa kwa kiolezo ambacho si kikamilifu, vivyo Adamu katika kutokukamilika kwake yeye asingeweza kuzaa watoto wakamilifu, wasio na dhambi.—Zaburi 51:5.
12. Jinsi gani matokeo ya dhambi ya Adamu na Hawa yaweza kulinganishwa na jambo linalotokea wakati watu wanaoishi maisha ya ufisadi wanapozaa watoto?
12 Matokeo ya dhambi ya Adamu na Hawa juu ya watoto wao yaweza kulinganishwa na jambo ambalo mara nyingi hutokea wakati watu hawaangalii sheria ya Mungu na kuishi kwa ufisadi huzaa watoto. Inawezekana kwa watu wa namna hiyo kupata maradhi katika viungo vya uzazi ambavyo Mungu aliwapa iii kuzaa watoto wao. Inawezekana kwa watoto wa wazazi ‘wachafu’ wa namna hiyo kuzaliwa wamelemaa kwa kimwili au kwa akili kwa sababu ya dhambi ya wazazi wao. Vivyo, pia, wazazi wetu wa kwanza wakawa ‘wachafu,’ wasiokamilika, wenye kupatwa na maradhi, na hatimaye wakafa. Wangeweza kupeleka kwa watoto wao kile ambacho wao wenyewe walikuwa nacho tu: kutokukamilika, na wakati ujao wenye maradhi na mauti. Ndiyo sababu kwa nini sisi sote tunazeeka na tunakufa, na kwa nini tunafanya makosa kwa urahisi sana.
13. Je! pana tofauti baina ya dhambi ya kukusudia na dhambi isiyo ya kukusudia? Jinsi gani hivyo?
13 Walakini, ni jambo moja kufanya makosa bila kukusudia kwa sababu ya dhambi iliyorithiwa, lakini ni jambo jingine kabisa kuzoea kwa kukusudia kile ambacho mtu anajua kuwa ni kosa. (1 Yohana 5:16) Ikiwa mtu ni mwenye kutubu kweli kweli kwa makosa ayafanyayo kwa sababu ya udhaifu uliorithiwa, aweza kutazamia msamaha wa rehema kutoka kwa Mungu. (Mithali 28:13) Lakini lazima awe mwangalifu kwamba, akiisha kujua yaliyo mema, asichague kwa makusudi kufuata mwendo ulio kinyume cha mapenzi ya Mungu. Kufanya hivyo kungemaanisha hasara ya kibali cha Mungu na uzima wenyewe. —Kumbukumbu la Torati 30:15-20; Waebrania 10: 26, 27.
14. Ni mpango gani ambao Mungu amefanya ili kuokoa wanadamu na dhambi na mauti?
14 Kwa furaha, Yehova amefanya mpango wa upendo kuwaokoa wenye kutubu na matokeo mabaya ya dhambi na mauti iliyorithiwa. Ondoleo hili la ajabu litakuja kwa dhabihu ya ukombozi wa Yesu Kristo. (1 Yohana 4:9) Hivyo, katika wakati uliowekwa na Mungu, chini ya utawala wa Ufalme wa Mwanawe, kutokukamilika kwa kibinadamu kulikorithiwa kutaondolewa polepole, na wanadamu hawatasikia tena matokeo ya dhambi ya Adamu. Kwani, hata mauti tuliyorithi kutoka kwa Adamu haitakuwa na nguvu tena juu yetu! (Ufunuo 21:3, 4) Unaweza kuwa ndiwe utakayejifurahisha baraka za namna hiyo. Jinsi gani? Kwa kutumia kwa faida mipango ambayo Yehova amefanya na kuthibitisha upendo wako kwake kwa kuzishika amri zake.—Mhubiri 12:13.
[Picha katika ukurasa wa 30]
Kwa makusudi Adamu akaihalifu sheria ya Mungu iliyosemwa waziwazi