Sura ya 8
Kwa Nini Mungu Ameruusu Uovu Yetu ya Leo?
1. Ni mambo gani yanayowapata wanadamu kuhusu uovu?
KATIKA historia yote ya wanadamu kumekuwako uovu mwingi. Na leo, haidhuru ni wapi unatazama katika ulimwengu, kuna umwagaji wa damu, uvunjaji wa sheria, chuki na ufisadi. Mara nyingi sana ni watu wazuri, wasio na hatia ndio hupatwa na matendo maovu ya wengine. Huenda wao hupatwa na jeuri, labda kupoteza nyumba zao, wapenzi wao au hata maisha zao wenyewe. Labda wewe mwenyewe umepatwa au labda hukupatwa na mambo ya namna hiyo. Hata ijapokuwa hukupatwa, inaelekea umepatwa na mambo ambayo yameleta maumivu ya moyoni, kupatwa na mambo kama vile dhuluma, ukatili, kupunjwa au kudanganywa.
2. Sababu kwa nini Mungu ameuruhusu uovu zinashughulika na maswali ya maana sana yaliyotokezwa wakati gani?
2 Kwa nini Mungu ameruhusu uovu wa namna hiyo mpaka siku yetu ya leo? Ziko sababu nyingi, lakini kuelewa sababu hizo sawasawa ni lazima tuchunguze maswali ya maana sana yaliyotokezwa wakati wa uasi wa kwanza. Inaelekea umesoma habari ya jambo hili katika Biblia katika sura ya tatu ya Mwanzo. Basi, na tuangalie maana halisi ya matukio haya.
3. Simulia kwa ufupi yaliyotukia wakati wa kutenda dhambi kwa mwanadamu?
3 Kwa ufupi, hili ndilo jambo lililotukia: Yehova alimwambia mtu kwamba uhai wake ulitegemea juu ya utii kwa Muumba wake, na ya kwamba kutokutii kungetokea katika mauti. (Mwanzo 2:17) Adui wa Mungu, Shetani, alipinga usemi huu ulio wazi. Alimwambia mke wa Adamu kwamba binadamu wawili wangeweza kutokutii na hata hivyo “Hakika hamtakufa.” Tena alidai kwamba kutokutii kwa namna hiyo kwa hakika kungewaletea maendeleo ya mambo, kufumbulisha macho yao, na ya kwamba wangekuwa “kama Mungu, mkijua mema na mabaya.” (Mwanzo 3:4, 5) Basi, jambo gani liliingizwa katika tendo hili la uasi wa Shetani?
MASWALI YA MAANA SANA YALIYOTOKEZWA
4. Taja baadhi ya maswali ya maana sana yaliyotokezwa na
4 Hesabu ya maswali ya maana sana yalitokezwa. Kwanza, Shetani alitokeza shaka juu ya ukweli wa Mungu. Kweli maana yake alimwita Mungu mwongo, na hiyo kwa habari ya shauri la uzima na mauti. Pili, alitokeza wazo la kwamba wanadamu hawakutegemea juu ya Muumba wao kwa maisha yenye kuendelea na furaha. Yeye alidai kwamba wala uhai wa wanadamu wala uwezo wao kutawala mambo yao kwa kufaulu haukutegemea juu ya utii kwa Yehova. Yeye alibisha kwamba wanadamu wangeweza kutenda bila kumtegemea Muumba wao na kuwa kama Mungu, wakijiamulia wenyewe yaliyo kweli na yaliyo uongo, yaliyo mema au yaliyo mabaya. Tatu, kwa kubisha juu ya sheria ya Mungu iliyosemwa, yeye kwa kweli alidai kwamba njia ya Mungu ya kutawala ni mbaya na si kwa faida ya viumbe vyake na katika njia hii hata alitokeza mwito wa kuthibitisha haki ya Mungu ya kutawala.
5. Kama inavyoonyeshwa katika kitabu cha Biblia cha Ayubu, ni swali gani lingine la maana sana lililotokezwa na Shetani?
5 Lakini kitendo cha Shetani kilitokeza bado swali lingine la maana sana, kama ilivyoonyeshwa baadaye katika Biblia katika kitabu cha Ayubu, sura za 1 na 2. Mle, kuhusiana na mwanadamu aitwaye Ayubu, inaonyeshwa kwamba Shetani alitokeza shaka juu ya uaminifu wa viumbe vyote kwa Yehova Mungu. Kwa kweli, Shetani alifanya dai kwamba wale wamtumi-kiao Mungu hufanya hivyo, si kwa sababu wanampenda Mungu na utawala wake wa haki, bali kwa sababu za kichoyo tu, kama vile baraka za kimwili ambazo Mungu huwapa. Alidai kwamba, ikiwa sababu hizo zilinyang’anywa, ndipo hata mwanadamu kama Ayubu angemwepuka Mungu. (Ayubu 1:6-11; 2:4, 5) Naam, uasi wa Shetani katika Edeni ulitokeza shaka juu ya uaminifu wa viumbe vyote vya Mungu mbinguni na duniani. Wakiwekwa katika jaribu, je! wangethibitisha upendo wao kwa Baba yao wa mbinguni na kuonyesha kwamba walipendelea utawala wake zaidi kuliko mwingine wo wote?
NJIA YA MUNGU YA KUJIBU MASWALI YA MAANA SANA
6. Je! Shetani alitokeza shaka juu ya nguvu ya Mungu? Basi ni swali la aina gani la maana sana lililopaswa kujibiwa?
6 Angalia, tafadhali, kwamba Shetani hakutokeza shaka lo lote juu ya nguvu ya Mungu. Yeye hakumsai Yehova kutumia nguvu zake kumharibu yeye kama mpinzani. Bali alitokeza mwito wa kuthibitisha haki ya Mungu kutawala na ukweli wa njia yake ya kutawala. Pia, alitokeza wazo la kwamba viumbe vya Mungu visingekuwa na uaminifu. Kwa hiyo lilikuwa swali la maana sana lililohusu wema na ubaya lililopaswa kujibiwa.
7. Simulia mfano unaoonyesha jinsi swali la maana sana la namna hiyo la wema na ubaya lingeweza kujibiwa.
7 Mashtaka ya uongo ya Shetani juu ya Mungu yanaweza kufananishwa, kwa kiasi fulani, katika njia ya kibinadamu. Ikiwa mtu mwenye jamaa kubwa anashtakiwa na mmojawapo wa jirani zake mambo mengi ya uongo juu ya njia ambayo kwa hiyo huongoza jamaa yake. Ikiwa jirani anasema pia kwamba washiriki wa jamaa hawana upendo halisi kwa baba yao bali sababu peke yake wao hukaa naye ni kwamba wapate chakula na mambo ya kimwili ambayo yeye huwapa. Jinsi gani baba wa jamaa angejibu mashtaka ya namna hiyo? Ikiwa yeye alitumia jeuri juu ya mshtaki, hii haingejibu mashtaka. Badala, huenda ikaonyesha kwamba yalikuwa ya kweli. Lakini linge-kuwa jibu bora namna gani ikiwa aliiruhusu jamaa yake mwenyewe kuwa mashahidi wake kuonyesha kwamba baba yao kweli alikuwa kichwa cha jamaa cha haki na chenye upendo na ya kwamba walikuwa na furaha kuishi pamoja naye kwa sababu walimpenda! Ndivyo angethibitishwa haki kabisa.—Mithali 27: 11; Isaya 43:10.
8. Ni jambo gani limeonyeshwa kwa sababu ya Mungu kuruhusu wakati wa kutosha kwa swali la maana sana kujibiwa kupita
8 Jambo hili huonyesha katika njia fulani jambo ambalo Mungu amefanya. Tena, yeye ameruhusu wakati wa kutosha—sasa karibu miaka 6,000—kwa swali la maana sana kujibiwa kupita shaka lote. Yeye ameruhusu wakati huu, si kuviruhusu viumbe vyake vya uaminifu kuthibitisha upendo wavyo kwake na kwa utawala wake tu, bali pia kuonyesha kwamba aina nyingine yo yote ya utawala hutokea tu katika ubaya. (Mithali 1:30-33; Isaya 59:4, 8) Kwa kumwasi Yehova Mungu, Shetani alijiweka mwenyewe kama mtawala wa kushindana. Na, kwa kuchukua mwendo ulioshauriwa na Shetani, wanadamu wawili wa kwanza walijitangaza wenyewe kujitegemea pasipo utawala wa Yehova na wakaja chini ya utawala wa Shetani. (Mwanzo 3:6; Warumi 6:16) Mungu kwa kumwacha Shetani na pia wanadamu kufika kwenye upeo katika jitihada zao kutenda na kutawala pasipo kumtegemea Muumba wao, kushindwa kwao kabisa kufanyiza serikali njema, pamoja na faida halisi kwa wanadamu wote, kungekuwa dhahiri kupita kukana kote kwa wakati ujao. Wakati ule ule Yehova angewafanya wale waliomo duniani ambao wanampenda walitangaze jina lake na makusudi yake kwa kuelimishwa kwa wote wapendao na kutafuta yaliyo mema.
9. Mungu alisema jambo gani kwa Farao wa Misri linalofanana
9 Basi, hali iko kama ile inayohusu Farao wa Misri aliyefuata mwendo unaofanana na ule wa Shetani Ibilisi katika kumpinga Yehova Mungu na ambaye kwake Yehova alisema: “Kwa kuwa wakati huu ningekwisha kuunyosha mkono wangu, na kukupiga wewe na watu wako, kwa tauni, nawe ungekatiliwa mbali na kuondolewa katika nchi; lakini, nilikusimamisha wewe kwa sababu ii hii, ili nikuonyeshe uweza wangu, tena kwamba jina langu litangazwe katika dunia yote.”—Kutoka 9:15, 16.
MATOKEO YAMEONYESHA NINI?
10. Jinsi gani Shetani ametumia wakati ulioruhusiwa na Mungu kwa habari ya mbingu na dunia?
10 Biblia huonyesha kwamba Shetani ametumia wakati kujenga tengenezo mbinguni na duniani ambalo juu yake yeye hutawala. Kiasi cha utawala wake wa dunia kinaonyeshwa kwa jambo la kwamba yeye aliweza kutoa kwa Yesu falme zote za ulimwengu badala ya ibada ya Yesu. (Mathayo 4:8, 9) Ndiyo sababu Shetani huitwa “mtawala wa ulimwengu huu.” (Yohana 16:11, NW) Hii imemaanisha nini kwa wanadamu, na yamekuwa matokeo gani ya mwendo wa wanadamu wa kutokumtegemea Mungu na utawala wake?
11. Yamekuwa matokeo gani ya huzuni ya mwendo wa wanadamu wa kutokumtegemea Mungu na utawala wake?
11 Historia hushuhudia kwamba huu haujaleta amani, uradhi na uzima wa milele kwa wanadamu. Umeleta kinyume: maelfu ya miaka ya maumivu, mateso na mauti. Maandishi ya historia na hali ya mambo ya kuogofya katika ulimwengu leo ni uthibitisho wa kwamba wanadamu hawajafaulu katika kutawala pasipo Mungu. Wanadamu wamejaribu aina zote za serikali, lakini bado wanakosa usalama na furaha yenye kudumu. Kweli, kumekuwako maendeleo katika njia ya kimwili. Lakini je! kweli ni maendeleo wakati wanadamu hutuma maroketi kwenye mwezi, lakini hawawezi kuishi pamoja katika amani duniani? Ni faida gani kwao kujenga nyumba zenye kutayarishwa na kila kifaa, ila kuwa na jamaa zikifarakanywa na talaka na ukaidi? Je! vita, ghasia katika barabara, uharibifu wa uhai na mali na kuenea kwa mahali pote kwa uvunjaji wa sheria ndilo jambo fulani la kujivunia? Hata kidogo! Bali mambo hayo ni matokeo ya utawala usiomjali Mungu. Kweli, kama Mhubiri 8:9 asemavyo, “mtu mmoja anayo mamlaka juu ya mwenziwe kwa hasara yake.”
12. (a) Mwandikaji mashuhuri wa magazeti alisema nini juu ya chanzo cha huzuni duniani? (b) Kupatana na nabii Yeremia, je! mwanadamu aweza kwa usalama kuelekeza hatua zake mwenyewe?
12 Hivyo kuruhusiwa kwa uovu kwa muda mrefu na Mungu kumethibitishwa kupita shaka lote kwamba jitihada ya wanadamu kutawala pasipo Mungu ni jambo la bure kabisa. (Zaburi 127:1) Kama mtengenezaji mashuhuri wa magazeti alivyosema: “Kadiri tutafutavyo sababu nyingine, ndivyo tuvumbuavyo kwamba huzuni duniani ni ya kufanyizwa na wanadamu. Udhaifu wetu mkuu ni wa kwamba hatujatatua tatizo la serikali ya kujitawala.”a Mwandikaji wa Biblia aliyeongozwa na roho ya Mungu Yeremia alisema sawasawa: “Ee [Yehova] najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu. Ee [Yehova], unirudi.”—Yeremia 10:23, 24; tazama pia Mithali 16:25.
13. Kwa kuwa utawala wa Shetani umethibitishwa kushindwa, Mungu sasa ana haki kabisa kufanya nini?
13 Uongozi wa Shetani juu ya mambo ya dunia umeleta kukosa umoja, uovu na mauti, na utawala wake umekuwa kwa njia ya udanganyifu, nguvu na choyo. Yeye amejithibitisha mwenyewe kutofaa kuwa mtawala wa cho chote. Hivyo sasa Yehova ana haki kabisa katika kumwangamiza mwasi huyu mdhilifu pamoja na wote ambao wameshiriki katika matendo yake maovu. (Warumi 16:20) Lakini namna gani juu ya uaminifu wa viumbe vya Mungu kwa utawala wa upendo wa Yehova na dai la Shetani la kwamba wote wangemwepuka ikiwa wangejaribiwa?
14. (a) Ni kwa madhumuni gani mema baadhi ya wanadamu wamemtumikia Mungu kwa nia? (b) Kwa kushika kwa Ayubu ukamilifu wa moyo kwa Mungu ijapokuw mkazo kutoka kwa Shetani, Ayubu alimthibitisha Ibilisi kuwa nini?
14 Yehova Mungu alijua kwamba “upendo haushindwi kamwe” naye alijua ya kwamba wanadamu wengine wangemtumikia kwa nia, kwa upendo, na si kwa sababu walihongwa au kulazimishwa. (1 Wakorintho 13:8, NW) Maelfu nyingi wamefanya hivi katika karne zote. Ayubu alikuwa mmojawapo wa hawa. Hata ijapokuwa Shetani alileta mkazo mkubwa juu yake na akakumba mali zake zote; watoto na afya, Ayubu bado alitangaza: “Mpaka nitakapokufa mimi sitaondoa ukamilifu wa moyo wangu.” (Ayubu 27:5, NW) Ayubu alimthibitisha Shetani kuwa mwongo.
15. (a) Jinsi gani Yesu alijibu shtaka la uongo la Shetani? (b) Je! Adamu mkamilifu angaliweza kuthibitisha uaminifu kamili kwa Mungu?
15 Kama tulivyokwisha kuona, mwanadamu mkamilifu Yesu alipinga vishawishi vyote na mahongo ya Shetani. Tena, wakati alipopigwa mijeledi na askari walinzi na kupigiliwa misumari kwenye mti wa mateso ya ukatili kufa, Yesu alishikamana na uaminifu wake kwa Mungu. (1 Petro 2:23) Hii ilithibitisha kwamba Adamu mkamilifu angaliweza kufanya lilo hilo ikiwa alikuwa ametaka, na kwamba Mungu hakuwa dhalimu katika kutaka utii kamili kutoka kwa wanadamu. (2 Wathesalonike 1:4, 5) Kwa uaminifu wake kwa Mungu, Yesu alitoa jibu bora kwa shtaka la uongo la Shetani.
16. (a) Ijapokuwa kuthibitishwa kabisa kuwa mwongo, kwa nini Shetani bado anaendelea kuwatesa wampendao Mungu? (b) Uaminifu wa watumishi waaminifu wa Mungu ni ushuhuda wenye kusadikisha wa jambo gani?
16 Lakini Shetani, kwa kupotoka kwa akili zake kwa choyo na kiburi, amekataa kulegeza mwendo wake wa wazimu. Ijapokuwa imethibitishwa zamani kwamba yeye ni mwenye makosa na mwongo, yeye huendelea kuwatesa wampendao Mungu. (Ufunuo 12:17) Tangu mauti ya Yesu maelfu nyingi ya Wakristo wamemtumikia Yehova Mungu kwa sababu walimpenda na walitaka utawala wake wa upendo juu yao. Na sasa hivi, mamia ya maelfu hutangaza uaminifu wao kwa Yehova kama mtawala. (Ufunuo 7:9, 10) Kushika kwao kwa uaminifu kwa Neno la Yehova na heshima yao kwa sheria yake kumewawezesha kuishi katika uradhi, ijapokuwa upinzani wote kutoka kwa Shetani. Umoja, upendo na ukamilifu wa moyo ulioonyeshwa na watumishi wa Mungu katika karne zote hutoa ushuhuda mkubwa wa kwamba njia ya Yehova ya kutawala katika upendo ndiyo njia ya pekee ya kweli, kwamba wanadamu waweza kudumu kuwa waaminifu kwake chini ya jaribu kali zaidi sana, na kwamba Shetani ndiye mwongo mkubwa zaidi kuliko wote wa wakati wote.
MPAKA LINI JARIBU LITAENDELEA?
17. Je! Mungu atauruhusu uovu kuendelea milele, na jinsi gani kitabu cha Biblia cha Danieli hujibu swali hilo?
17 Yehova ameuruhusu uovu mpaka siku yetu ya leo ili ajibu maswali yote ya maana sana yaliyotokezwa na Shetani. Lakini hatauruhusu uovu kuendelea milele. Yeye ameweka wakati halisi wakati atakapoukomesha. Mwandikaji wa Biblia Danieli aliutaja huu zamani wakati alipoandika: “Mwisho utatokea wakati ulioamriwa.”—Danieli 11:27.
18. Ijapokuwa kipindi cha wakati cha karibu miaka 6,000 huonekana kirefu kwa wanadamu, je! kinaonekana kirefu kwa Mungu? Basi jinsi gani Mungu huona miaka elfu?
18 Karibu miaka elfu sita kutoka siku ya Adamu mpaka kwa siku yetu ya leo huenda uonekane kuwa muda mrefu ukionwa kwa maoni ya wanadamu ambao huishi yapata miaka sabini. Lakini kwa kuwa Mungu aliweka mpaka wa wakati, ni vema kuthamini maoni yake ya shauri. Nabii Musa, katika Zaburi 90:4, husema kwa habari yake: “Miaka elfu machoni pako ni kama siku ya jana ikiisha kupita.” Mwaka ni wakati mrefu kwa mtoto mchanga wa miaka mitano, lakini kwa mtu mwenye miaka sitini ni mfupi kwa kulinganisha. Vilevile, kwa Yehova, ambaye huishi kwa umilele, miaka elfu ni kama siku moja.—2 Petro 3:8.
19. Kwa nini ruhusa ya Mungu ya uovu haikuwa udhalimu kwetu?
19 Wakati huu uliowekwa ambao katika huo uovu umeruhusiwa haukuwa udhalimu kwetu. Kwani, ikiwa Mungu alikuwa ameuponda uhai kutoka katika waasi wote katika Edeni, sisi hata tusingalizaliwa kamwe! Tusingalikuwa tumepata kamwe nafasi kwa uzima wa milele katika taratibu yake mpya. Basi jambo la kwamba Yehova hakukomesha uvumilivu wake wakati fulani wa mapema zaidi limetupatia sisi nafasi ya kuishi sasa, na kwa milele katika wakati ujao. (2 Petro 3:9, 15) Pia, Mungu ametumia wakati huu kutayarisha ukombozi wa wanadamu kupitia kwa Kristo. —Wagalatia 4:4, 5.
20. Jinsi gani Biblia katika Warumi 9:22-24 hueleza sababu kwa nini Mungu ameruhusu uovu?
20 Kwa kuongeza, Mungu ameutumia wakati kuchagua na kutayarisha kutoka miongoni mwa wanadamu “vyombo vya rehema.” Hawa ndio wale watakaokuwamo katika serikali ya haki juu ya wale watakaoishi milele duniani katika taratibu mpya. Ni baraka namna gani ambazo ufalme huu wa mbinguni humaanisha kwa wanadamu! Katika wakati ambao Mungu amekuwa akivitayarisha “vyombo vya rehema,” ameonyesha uvumilivu mwingi. Yeye amewavumilia waovu, “vyombo vya ghadhabu.” Ameahirisha uharibifu wao. Kwa nini? Biblia hujibu waziwazi: “Ili audhihirishe wingi wa utukufu wake katika vile vyombo vya rehema.” (Warumi 9:22-24) Ufalme wa Mungu wa mbinguni utapewa utukufu wa kuthibitisha haki ya jina la Mungu na kuwaangamiza waovu, “vyombo vya ghadhabu.” Pia, kwa kuruhusu kwake uovu kuendelea kwa muda, sehemu za utu wa Mungu zimedhihirishwa ambazo kwa kawaida zisingeonekana: rehema yake na uvumilivu. Hizi hukuza thamani yetu ya Muumba na utu wetu wenyewe, kadiri tumwigavyo. —Waefeso 5:1.
21. Ni faida gani nyingine imetokea kwa sababu uovu umeruhusiwa na Mungu kutimiza wakati wake uliowekwa?
21 Pia kumekuwako faida nyingine ya kweli katika kuruhusu kwa Mungu kwa uovu kwa muda ambao amefanya. Ikiwa wakati wo wote katika wakati ujao ye yote itampasa kutokeza shaka juu ya njia ya Mungu ya kufanya mambo, isingekuwa lazima tena kwake kumruhusu mtu huyo wakati kujaribu njia fulani nyingine. Maandishi ya miaka elfu sita ya kushindwa kwa Shetani, mashetani wake, na wanadamu ambao wamejaribu kuongoza mambo pasipo kumtegemea Mungu yametoa jibu la kutosha. Hapana mtu awezaye kudai kwa haki: ‘Hawakupata nafasi,’ au kusema, ‘Laiti walikuwa na wakati zaidi.’ Wakati ulioruhusiwa umetosha kuthibitisha kwamba njia ya uasi juu ya Muumba imekuwa yenye msiba kabisa! Hivyo Mungu atakuwa na haki kabisa kwa kumwangamiza upesi mwasi ye yote ambaye anatisha amani ya wakati ujao ya ulimwengu wote.—Zaburi 145:20.
22. Mpaka lini Yehova ataruhusu uovu, na ni nafasi gani ambayo wakati ubakio hutupa sisi?
22. Kunabaki wakati mfupi tu kabla Yehova hajaiharibu taratibu hii mbovu ya mambo. Wakati huu ubakio hutupa sisi nafasi kusimama upande wake na ‘kumfurahisha moyo wake.’ (Mithali 27:11) Ikiwa tunanyenyekea kwa nia utawala wake, yeye atatubariki na uzima wa milele katika taratibu yake mpya. Uchaguzi wa kukubali au kukataa umewekwa mbele ya kila mmoja wetu.—Kumbukumbu la Torati 30:19, 20.
23. (a) Jinsi gani imetupasa kuuona utii kwa Mungu? (b) Watumishi waaminifu wa Mungu wakiisha kufanya kazi ya kulitangaza jina lake na makusudi yake katika dunia yote, Yehova atafanya nini?
23. Utii kwa Mungu kwa kweli si mgumu. Tukithamini kwamba hekima ya Yehova ni kubwa kuliko yetu, na ya kwamba lo lote alifanyalo ni kwa faida yetu ni kwa faida yetu kwa sababu yeye ni Mungu wa upendo, basi tutamtii yeye katika kila kitu. Mapenzi yawayo yote ya Yehova, tutaka kuyafanya, kwamba ni katika wakati wa hatari au katika mambo ya maisha ya kila siku. Ndiyo njia ambayo watumishi waaminifu wa Mungu wamejiona sikuzote. (Danieli 3:16-18; Zaburi 119:33-37) Katika karne ya kwanza baadhi ya hawa walisema kwa korti kuu: “Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.” (Matendo 5:29) Leo, Yehova anatumia watuimishi wake waaminifu kutangaza jina lake na makusudi yake katika dunia yote. (Mathayo 24:14) Wakati jambo hilo litakapofanyika kwa kutosheka kwake, ndipo atakapomwonyesha shetani uwezo wa nguvu zake zote kwa kumponda yeye na waasi wengine wote, akileta kikomo kwenye taratibu hii mbovu. Ndiyo, Yehova atakapoondoa uovu katika ulimwengu wote na kufanya njia kwa taratibu yake mpya ya haki.
[Maelezo ya Chini]
a David Lawrence, U.S. News & World Report, ya Septemba 25, 1967, ukur. wa 128.
uasi wa Ibilisi.
shaka lote?
na habari ya Shetani Ibilisi?