Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • te sura 39 kur. 159-162
  • ‘Mbarikiwa ni Yeye Anayekuja kama Mfalme’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Mbarikiwa ni Yeye Anayekuja kama Mfalme’
  • Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Habari Zinazolingana
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini? Na Tunaonyeshaje Kwamba Tunautaka?
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Serikali ya Mungu ya Amani
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
te sura 39 kur. 159-162

Sura ya 39

‘Mbarikiwa ni Yeye Anayekuja kama Mfalme’

WEWE unaijua Sala ya Bwana?— Ebu sema nisikie.— lkiwa huikumbuki, tutaisoma pamoja katika Biblia katika Mathayo sura ya sita, mistari tisa mpaka kumi na tatu.

Sasa, katika sala hiyo inasema, “Ufalme wako uje.” Ufalme ni nini? Unajua?— Ufalme ni serikali. Na wewe unajua hiyo ni nini, sivyo? — Serikali ni kikundi cha watu wanaotawala nchi.

Katika serikali kuna mkuu au mtawala. Katika nchi nyingine mtu huyu anaitwa rais. Lakini unajua mtawala wa serikali ya Mungu anaitwa nini?— Yeye ni mfalme.

Kwa ufalme wa Mungu Yehova mwenyewe amechagua mfalme. Unajua mfalme huyo ni nani?— Ni Yesu Kristo. Yeye ni bora kuliko mtawala ye yote ambaye wanadamu wanachagua. Yesu ana uwezo zaidi kuliko ye yote wa watawala hawa. Na Yesu kweli anampenda Mungu, hivyo sikuzote anafanya mema.

Hapo zamani katika Israeli wafalme wapya walipanda kuingia katika Yerusalemu juu ya mwana-punda ili wajionyeshe wenyewe kwa watu. Hivi ndivyo Yesu alifanya.

Nje ya Yerusalemu kulikuwako kijiji. Wakati Yesu alipofika karibu nacho, alisema kwa wawili wa wanafunzi wake: ‘Nendeni katika kijiji kile, na mtaona mwana-punda. Mfungueni na kumleta kwangu mimi.’

Wanafunzi walifanya kama Yesu alivyosema. Na wakati walipomleta mwana-punda kwa Yesu, alikaa juu yake. Wakati alipofika karibu na Yerusalemu, kundi kubwa la watu lilikuja kumlaki.

Wakati Yesu alipokuwa akiendelea kupanda, karibu kundi lote lilianza kutanda mavazi yao katika njia mbele yake. Wengine walikata matawi kutoka kwa miti wakayaweka haya katika njia. Kwa hivi walionyesha kwamba walitaka Yesu awe mfalme.

Watu walifurahia kumshangilia Yesu. Walipaza sauti hivi: “Mbarikiwa ni Yeye anayekuja kama Mfalme katika jina la Yehova!”

Lakini si kila mtu alifurahi kwa vile Yesu alikuwa akipanda kama mfalme katika Yerusalemu. Wengine hata walisema hivi kwa Yesu, ‘Waambie wanafunzi wako wanyamaze.’—Luka 19:28-40, NW.

Wewe unaona namna gani juu ya kuwa na Kristo kama mfalme?— Ikiwa ungalikuwa ukii-shi wakati Yesu alipopanda katika Yerusalemu, je! ungalimshangilia kama yeye aliyetumwa na Yehova kwa watu wake?—

Basi, Yesu hayuko duniani leo, sivyo?— Yeye yuko mbinguni. Ni kutoka huko mbinguni ndiko anatawala kama mfalme. Hata ingawa hatuwezi kumwona, yeye anaweza kumwona kila mmoja wa sisi hapa duniani. Hatuwezi kumdanganya. Yeye anaona tunachofanya, na hata anajua tunayofikiria. Ikiwa kweli tunampenda Yehova, yeye anajua hilo. Na ikiwa tunajitahidi kufanya ambayo Biblia inasema, yeye atatusaidia. Je! wewe ungependa awe mfalme wako milele?—

Si kila mtu anataka Kristo awe mfalme. Labda watasema wanamwamini Mungu, lakini hawataki ufalme wake. Hawataki Mungu au Kristo awe akiwaambia jambo la kufanya. Wanataka serikali zao wenyewe apa hapa duniani. Basi unajua jambo litakalowapata?—

Biblia inatupa jibu katika Danieli sura ya pili, mstari wa 44. Na tuchukue Biblia zetu na kufungua hapo pamoja. Andiko hili linasema juu ya wakati wetu linaposema hivi: “Katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.”

Je! ulifahamu hilo?— Biblia inasema kwamba serikali ya Mungu itaharibu serikali hizi zote za kidunia. Sababu gani?— Kwa sababu hazimtii yeye ambaye Mungu amefanya kuwa mfalme.

Dunia nzima ni mali ya Mungu. Aliifanya tena akafanya ulimwengu mzima wote. Basi yeye ana haki kuamua ni serikali ya namna gani imepaswa kutawala. Na serikali yake ndiyo serikali bora. Hivi karibuni ufalme wa Mungu ndio utakuwa serikali peke yake.

Je! wewe unataka kuishi milele chini ya ufalme wa Mungu?— Mimi nataka. Lakini lazima tuonyeshe hilo kwa Mungu. Je! unajua namna ya kuonyesha?— Ni kwa kujifunza sheria za Mungu na kuzitii kila siku.

Sasa, Mungu anasema kwamba ufalme wake utaharibu serikali za wanadamu. Lakini je! yeye anatuambia kwamba imetupasa sisi tufanye hivyo? Hapana. Biblia inasema kwamba imetupasa tuzitii sheria za wanadamu, kwa kadiri Mungu anavyoruhusu serikali hizo kutawala.

Lakini ikiwa kweli tunamtaka Kristo kama mfalme, inatupasa tufanye zaidi ya hilo. Inatupasa tutii mambo yote ambayo Kristo alisema. Yeye alisema kwamba imetupasa tuwe “si wa ulimwengu.” Je! tungekuwa tukimtii yeye ikiwa tungejaribu kuwa sehemu ya serikali za ulimwengu? Yesu na mitume wake waliepuka mambo hayo.—Yohana 17:14.

Pahali pake walifanya nini?— Walisema kwa watu wengine juu ya ufalme wa Mungu. Hiyo ilikuwa kazi kubwa katika maisha zao. Je! na sisi tunaweza kufanya hivyo?— Ndiyo, na tutafanya ikiwa tunamaanisha tunachosema wakati tunapoombea ufalme wa Mungu uje.

(Sasa tumia dakika chache zaidi msome maandiko zaidi haya yanayoonyesha namna imetupasa tumwone yeye ambaye Mungu amefanya mfalme: Isaya 9:6, 7; Danieli 7:13, 14; Yohana 18:36; Mathayo 6:33.)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki