Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • fl sura 10 kur. 131-145
  • Ubora wa Kutia Adabu katika Upendo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ubora wa Kutia Adabu katika Upendo
  • Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • FIMBO YA ADHABU
  • KUWEKA MIPARA ILIYO IMARA
  • TAFRIJA ZIFANYWE KWA KIASI
  • UNAPOTOA ADHABU, PASHANENI HABARI!
  • NJIA MBALIMBALI ZA KUTOLEA ADABU
  • TOA ADABU KATIKA UPENDO
  • Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Nidhamu Inazaa Tunda Lenye Kuamanika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Nidhamu Inayofaa
    Amkeni!—2015
Pata Habari Zaidi
Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
fl sura 10 kur. 131-145

Sura ya 10

Ubora wa Kutia Adabu katika Upendo

1. Ili watoto wawe watiifu, mtu anatakiwa afanye nini?

WATOTO watiifu, wenye upendo na wenye adabu njema, hawatokei bure. Wanatengenezwa na kufanyizwa kupitia kwa mfano na kwa kutiwa adabu.

2. Maoni ya wachunguzi wengi wa akili za watoto yanapingana namna gani na shauri la Biblia?

2 Wachunguzi wengi wa akili za watoto wanashauri kwamba haifai kuwapiga watoto, kama mmoja wao alivyosema hivi: “Je! mnajua ninyi akina mama kwamba kila unapompiga mtoto wako unaonyesha kwamba unamchukia mtoto wako?” Lakini katika Neno lake, Mungu anasema hivi: “Yeye asiyetumia fimbo yake anachukia mwana wake: lakini yeye anayemupenda anamwazibu wakati kwa wakati.” (Mezali 13:24, Biblia ya Kiswahili ya Zaire) Makumi machache ya miaka iliyopita, sana sana katika mataifa ya Magharibi, vitabu vinavyoeleza habari za kulea watoto, vikiwa na mawazo ya kushauri kuwapa watoto uhuru mwingi, vilijaa sana masoko. Kutoa adabu kungemzuia mtoto na kumfanya asikue, ndivyo wachunguzi wa akili walivyosema; na kwa habari ya kupiga, wazo hilo lilikuwa lenye kuwachukiza sana. Mawazo yao yalipingana kabisa na shauri la Yehova Mungu. Neno lake linasema kwamba ‘unavuna ukipandacho.’ (Wagalatia 6:7) Je! makumi machache ya miaka ya kupanda mbegu ya kuachilia watoto wafanye wanavyotaka imeonyesha nini?

3, 4. Ni mambo gani ambayo yametokana na ukosefu wa adabu zinazofaa nyumbani, hivyo wengi wanapendekeza nini?

3 Mazao mengi ya uvunjaji wa sheria na makosa ya watoto yanajulikana sana. Katika mataifa mengi yenye utajiri, kati ya makosa mazito yanayofanywa, kadiri ya zaidi ya 50 kwa mia ni makosa yanayofanywa na watoto. Katika sehemu fulani za ulimwengu, wanja za shule na vyuo vikuu ndipo mahali penye kufanyiwa mafarakano kati ya wanafunzi na waalimu, mapigano, matusi na matukano, kuharibu mali za watu, kushambulia watu, unyang’anyi, matendo ya kuteketeza nyumba na mali za watu kwa kusudi, wivi wa kutumia nguvu, kulalwa kwa wanawake kwa nguvu, dawa za kulevya na mauaji. Msemaji wa chama cha waalimu katika nchi moja kubwa alichunguza akaona kwamba ukosefu huo wa adabu unatokea kwa sababu ya kushindwa kwa shule kuwafundisha watoto utii katika umri wa mapema. Tena, alilaumu jamaa zilizoharibika na wazazi kutotaka kuwekea watoto wao kanuni zinazofaa za mwenendo mwema, akionyesha kuwa sababu ya makosa hayo ya watoto. Katika kulichunguza ulizo la ‘sababu gani washiriki wengine wa jamaa fulani wanakuwa wavunjaji wa sheria na hali wengine wasiwe hivyo,’ kitabu The Encyclopcedia Britannica kinasema: “Labda maongozi ya jamaa ya kutia adabu hayana nguvu sana, ni ya ukali mno, ama hayapatani sana. Mchunguzi Mwamerika amedokeza kwamba labda adabu isiyofaa inahusiana na kadiri yapata 70 kwa mia ya wanaume wanaovunja sheria.”

4 Matokeo hayo ambayo yamepata watu yamefanya wengi wao wageuze maoni yao waanze tena kutoa adhabu.

FIMBO YA ADHABU

5. Biblia ina maoni gani juu ya kupiga mtoto?

5 Kupiga kunaweza kuokoa uhai wa mtoto, kwa maana Neno la Mungu linasema hivi: “Usimnyime mtoto wako mapigo; maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa. Utampiga kwa fimbo na kumwokoa nafsi yake na [Kaburi].” Tena, “Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.” (Mithali 23:13, 14; 22:15) Wazazi wakiona uhai wa watoto wao kuwa wenye thamani sana, hawatakosa kutoa adhabu kwa sababu ya ugoigoi au uzembe wao. Upendo utawaongoza wachukue hatua, kwa hekima na kwa kufaa, wakati inapohitajiwa.

6. Adabu ni pamoja na nini?

6 Kwa habari ya adabu yenyewe, haitolewi kwa kuadhibu peke yake. Kwanza adabu inamaanisha ‘mafundisho na mazoezi yanayoshikamana na agizo fulani au mpango fulani.’ Ndiyo sababu Mithali 8:33 inasema, “sikieni mafundisho, mpate hekima,” si ‘mwone mafundisho’ (adabu). Kulingana na 2 Timotheo 2:24, 25 ZSB, inampasa Mkristo “kuwa mupole kwa watu wote, anayeweza kufundisha, muvumilivu, akiwaonya kwa upole wenye kushindana naye.” Hapa neno hili “kufundisha,” limetafsiriwa kutokana na neno la Kigiriki lenye maana ya adabu. Neno lilo hilo limetafsiriwa katika Waebrania 12:9 hivi “Tuliwapa heshima inayostahili wale baba zetu wa kidunia waliotutia adabu; je! tusijiweke chini ya Baba yetu wa kiroho kwa vyepesi hata zaidi, na hivyo tupate uzima?”—New English Bible.

7. Ni faida gani zinazotokana na adhabu inayotolewa na wazazi?

7 Mzazi anayeshindwa kumpiga mtoto hataheshimiwa na mtoto, kama vile watawala wakati wanapoachilia makosa bila kutoa adhabu. Adhabu ikitolewa kwa kufaa, inaonyesha mtoto kwamba wazazi wake wanapendezwa naye. Inasaidia kufanya nyumba iwe na amani, kwa maana “baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.” (Waebrania 12:11) Watoto wasiotii, wasio na adabu ni wenye kutia uchungu katika nyumba yo yote, na watoto hao si wenye furaha wakati wo wote. “Azibu mwana wake naye atakupumzisha; ndiyo, atafurahisha nafsi yako.” (Mezali 29:17, ZSB) Baada ya adhabu ya upendo, mtoto anaweza kupata maoni mapya na mwanzo mpya, na mara nyingi ni rafiki mzuri zaidi. Kwa kweli, adhabu ‘inaleta matunda yenye amani.’

8. Wazazi wanawezaje kutoa adhabu katika upendo?

8 “Yeye ambaye Yehova anapenda, anamtia adabu.” (Waebrania 12:6, NW) Ndivyo na mzazi anayetaka sana mtoto wake awe na hali njema. Kutoa adhabu kunapaswa kufanywe katika upendo. Hasira ni jambo la kawaida wakati mtu anapokasirishwa na kosa la mtoto, lakini, kama Biblia inavyoonyesha, imempasa awe “mvumilivu.” (2 Timotheo 2:24) Mtu akiisha kupoa hasira yake, huenda dhambi ya kitoto isionekane kubwa mno: “Busara ya mwanadamu bila shaka inatuliza hasira yake, na ni uzuri wake kuachilia mbali makosa.” (Mithali 19:11, NW; tazama vilevile Mhubiri 7:8, 9.) Huenda zikawako sababu zenye kupunguza uzito wa kisa fulani: Labda mtoto huyo amechoka sana au anaumwa. Labda amesahau alivyokuwa ameambiwa; watu wazima wanasahau pia, sivyo? Lakini hata ikiwa kosa fulani halipaswi kuachiliwa mbali, ile adhabu haipaswi itolewe katika hasira isiyozuiwa au kwa pigo linaloamsha hasira nyingi za mzazi. Adhabu inatia ndani kufundisha, na kwa hasira nyingi mtoto anajifunza somo pasipo kujiweza. Mtoto haoni anapendwa kama anavyoona wakati adhabu inapotolewa vizuri. Basi, usawa ni wa lazima, nao unaleta amani.

KUWEKA MIPARA ILIYO IMARA

9. Imewapasa wazazi wawape watoto nini kupatana na Mithali 6:20, 23?

9 Inawapasa wazazi wawape watoto wao maongozi. “Mwanangu, ishike amri ya baba yako, wala usiiache sheria ya mama yako. Zifunge daima katika moyo wako; zifunge katika koo yako. Unapotembea huku na huku, itakuongoza; unapolala, itakulinda ; na wakati umeamka, yenyewe itakufanya uifikirie. Kwa maana amri ni taa, na nuru ni sheria, nayo makaripio ya kutia adabu ndiyo njia ya uzima.” Maagizo hayo ya wazazi ni ya kuongoza na kumlinda mtoto, nayo yanaonyesha kwamba wazazi wanataka watoto wao wawe na hali njema na furaha.—Mithali 6:20, 23 NW.

10. Jambo gani laweza kutokea wakati wazazi wanaposhindwa kutia watoto wao adabu?

10 Baba anayeshindwa kufanya hivyo, ana lawama. Eli, kuhani mkuu katika Israeli wa kale, aliachilia watoto wake wa kiume wasitawishe tamaa mbaya, kutokuheshimu na uasherati; aliwapinga kidogo lakini hakuchukua hatua ya kweli ili awaachishe kufanya makosa yao. Mungu alisema hivi: “Ninaihukumu nyumba yake kwa wakati usiojulikana kwa kosa ambalo amelijua, kwa sababu wanawe wanamtukana Mungu, naye hakuwakemea.” (1 Samweli 2:12-17, 22-25; 3:13, NW) Vivyo hivyo, mama akishindwa kutimiza wajibu wake, anapata aibu: “Fimbo na maonyo hutia hekima; bali [mvulana au msichana] aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.”—Mithali 29:15.

11. Sababu gani watoto wanahitaji kuwekewa mipaka?

11 Watoto wanahitaji kuwekewa mipaka. Hawajioni vizuri ikiwa hakuna mipaka. Kuwa nayo na kuifuata kunawafanya watoto wajione kuwa sehemu ya kikundi fulani; wanakuwa mali ya kikundi hicho, nao wanakubaliwa nacho kwa sababu wanafuata matakwa yake. Kuachilia watoto kunawafanya wawe katika hali yenye matatizo. Matokeo yanaonyesha kwamba watoto wanahitaji watu wazima ambao wana hakika sana na mipaka, na watakaowapa wengine mipaka hiyo. Watoto wanahitaji kufahamu kwamba kila mtu duniani anawekewa mipaka, na ya kwamba mipaka hiyo inamletea mtu furaha na faida. Uhuru unaweza kufurahiwa tu wakati wengine wanapokubali mpaka wa uhuru wetu nasi tunapokubali mpaka wao. Bila shaka kuvuka mipaka inayofaa, kunamaanisha kwamba mkosaji huyo anaelekea ‘kiasi cha kudhuru na kuingilia haki za ndugu yake.’—1 Wathesalonike 4:6, NW.

12. Sababu gani ni jambo la maana kujitia adabu, nao wazazi wanaweza kusaidiaje watoto wao wakusitawishe?

12 Watoto wanapojifunza kwamba kuvuka mipaka inayofaa kunaleta adhabu ya namna moja au namna nyingine, wanaikubali mipaka yao wenyewe, na kwa kuwa imara na kwa uongozi wa wazazi, watoto wanasitawisha hali ya kujitia adabu wenyewe, ambalo ni jambo la lazima ili waishi kwa furaha. Yatupasa sisi wenyewe tujitie adabu, ama sivyo, tutatiwa adabu na mwingine. (1 Wakorintho 9:25, 27) Tukijitia adabu sisi wenyewe na kusaidia watoto wetu wafanye ivyo hivyo, maisha zetu na zao zitakuwa zenye furaha zaidi, pasipo masumbufu na masikitiko.

13. Ni mambo gani ya maana ambayo wazazi wanapaswa wa-kumbuke wanapowekea watoto wao maongozi?

13 Watoto wanapaswa wafahamu vizuri maongozi na mipaka ambayo wanawekewa, iwe ya kadiri, na kukumbuka kuonyesha rehema. Usiwatazamie kufanya mengi mno wala machache mno. Kumbuka umri wao, maana watatenda kulingana na umri huo. Usiwatazamie kuwa kama watu wazima. Mtume alisema kwamba, alipokuwa mtoto mchanga, alitenda kama mtoto mchanga. (1 Wakorintho 13:11) Lakini kanuni za kiasi zikiisha kuwekwa, na watoto wako wanazifahamu, weka lazima ya kutii upesi na bila kugeuka-geuka. “Neno lenu Ndiyo na limaanishe Ndiyo, La yenu, iwe La.” (Mathayo 5:37, NW) Watoto wanawathamini sana wazazi wanaotimiza wanayosema, wasiogeuka-geuka na wanaoweza kutazamiwa kutimiza yale wanayowaambia watoto wao, maana wanajua nguvu inayowategemeza, nao wanajiona kwamba wanaweza kuitegemea wakati taabu zinapofika na wanapohitaji msaada. Wazazi wakiwa na kiasi, lakini imara katika kutoa adhabu ya kuondoa makosa, jambo hilo linawafanya watoto wajione salama na imara. Watoto wanataka kujua upande wao, nao wanaujua wakiwa na wazazi kama hao.

14. Sababu gani kuwa imara ni kwa maana wakati watoto hawaitikii uongozi wa wazazi wao?

14 Inawapasa wazazi wakaze nia ili waonyeshe imara yao wakati mtoto anapokataa kutii agizo lao. Hapo ndipo wazazi wengine wanapotumia njia za kumwogopesha mtoto kwa kusema kwamba watamchapa. Wanaanza kubishana naye bure au wakijaribu kumhonga (kumbembeleza kwa kumpa kitu fulani) ili afanye walilomwambia kufanya. Mara nyingi jambo linalotakiwa tu ni kuwa imara sana na kumwambia mtoto, kwa mkazo sana, kwamba ni lazima alifanye, tena alifanye sasa hivi. Ikiwa mtoto angetaka kwenda mbele ya motokaa inayokuja, wazazi wangemwambia waziwazi jambo la kufanya kwa hakika. Kama wachunguzi fulani wa jambo hilo wanavyoeleza: “Karibu wazazi wote wanawaambia watoto wao waende shuleni, . . . wapige mswaki, waondoke juu ya nyumba, waoge, na vivyo hivyo. Mara nyingi watoto wanapinga. Lakini wanakubali, kwa sababu wanajua kwamba wazazi wao hawafanyi mchezo.” Unaweza kutazamia watoto wako ‘kufunga daima maongozi na amri zako katika mioyo yao’ ikiwa unazitia nguvu tena bila kugeuka-geuka.—Mithali 6:21.

15. Wakati wazazi hawaweki lazima ya kutii maongozi kama inavyotakiwa, watoto wanaweza kuwaje?

15 Wazazi wanapoweka lazima ya kutii maongozi mara chache tu kwa sababu wanavutwa na wazo ama hali fulani ya muda, au wakati wanapokawia kuwachapa watoto wao wanapokataa kutii, watoto bila kuogopa, watajaribu kufanya makosa ili waone kama wanaweza kuadhibiwa. Adhabu inapokawia kutolewa, watoto ni kama watu wazima, wanafanya mioyo yao kuwa migumu ili wafanye mabaya. “Kwa sababu hukumu juu ya tendo baya haitekelezwi upesi, mioyo ya wanadamu huthibitishwa ndani yao ili kutenda mabaya.” (Mhubiri 8:11) Hivyo, sema unalokusudia kufanya, na kutimiza unalosema. Hapo ndipo mtoto wako atakapofahamu kwamba hivyo ndivyo ilivyo, naye atajua kwamba kumbe ni kazi bure kutokeza midomo kwa uchungu, wala kubishana, wala kutenda kana kwamba anadhani wewe ni mjeuri na asiye na upendo.

16. Imewapasa wazazi wafanye nini ili waepuke kutoa amri zisizo na kiasi?

16 Hilo linataka kufikiri kabla ya kusema. Sheria au amri zinazotungwa bila kufikiri, si za kiasi mara nyingi. Uwe “mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema: wala kukasirika.” (Yakobo 1:19) Ikiwa adhabu haitolewi kwa kiasi na kama inavyotakiwa, watoto watajua kwamba hiyo si haki, nao wataanza kusitawisha chuki.

TAFRIJA ZIFANYWE KWA KIASI

17. Watoto wamepaswa wathamini maoni gani ya kazi na michezo?

17 Kucheza ni sehemu ya kawaida ya maisha ya mtoto. (Zekaria 8:5) Inawapasa wazazi wafahamu hilo, lakini wawe wakitia polepole katika maisha ya mtoto hali ya kuona ubora wa kufanya kazi na hali ya kujiona kuwa na daraka. Kisha, kazi zo zote za nyumbani alizo nazo mtoto zinaweza kufanywa kwanza; kucheza ni jambo la pili.

18. Rafiki wanaweza kuleta matokeo gani kwa watoto?

18 Watoto wengine wanageuka kuwa wazururaji (watembeaji bila jambo wanalofanya) katika barabara za mjini, au wanakuwa wageni kabisa nyumbani kwao kwa sababu ya kutafuta tafrija mahali pengine. Ikiwa mashirika (urafiki) si mazuri, matokeo yatakuwa si mazuri vilevile. (1 Wakorintho 15:33) Bila shaka kuwa na ushirika kidogo nje ya nyumba ni kwa faida kwa mtoto ili apate kufahamu watu wengi. Lakini ushirika wa nje unapokuwa hauna kiasi au unapoa chwa pasipo kuongozwa, mpango wa jamaa unakosa nguvu au hata unavunjika.

19. Ni mambo gani ambayo wazazi wanaweza kuchunguza ili wajue kama wanaifanya nyumba iwe mahali penye kufurahisha kwa watoto wao?

19 Pamoja na adabu wanayotoa ili watengeneze hayo, wazazi wanaweza kujiuliza wenyewe jambo watakalofanya ili waifanye nyumba ifurahishe zaidi watoto; kwamba wanatumia wakati wa kutosha pamoja nao, si kuwafundisha au kuwatia adabu tu, bali vilevile wakiwa rafiki za kweli na wenzi wa watoto wao. Je! kwa kawaida wewe ni mtu “mwenye kazi nyingi mno” hata huwezi kutumia wakati wa kuwa pamoja na watoto wako, ucheze nao? Mara nafasi hizo za kucheza pamoja na watoto zisipotumiwa, hazitapatikani tena. Wakati ni wenye kuelekea upande mmoja, naye mtoto hakai pale pale tu, bali anaendelea kukua na kubadilika. Majira yanapita, na ijapokuwa mwana wako anaonekana kama alikuwa kitoto kichanga jana tu, akijifunza kutembea, unafahamu pasipo kutazamia kwamba anaendelea kuwa mwanamume kijana, naye msichana wako mdogo amekwisha kugeuka akawa mwanamke kijana. Ukiendeleza usawa mzuri na kujitia adabu mwenyewe katika kutumia kwako wakati, hapo tu ndipo unapoweza kuepuka kuzidharau nafasi zinazotolewa na kipindi hicho chenye maana sana—au uepuke kuona watoto wako wakijitenga na wewe wakati wangali wenye umri mchanga.—Mithali 3:27.

20, 21. Imewapasa wazazi wawe na daraka gani ikiwa nyumbani kuna television?

20 Ikiwa television inatumiwa sana kuleta tafrija, inaweza kuwa lazima kuweka mipaka ya kuitumia. Wazazi wengine wanatumia television kuwa kama yaya wa kutunza mtoto. Huenda ikafaa kufanya hivyo na haichukui fedha nyingi; lakini kwa kweli njia hiyo inaweza kuwa yenye gharama kubwa sana. Mara nyingi vipindi vya television vinajaa mambo ya ujeuri na uasherati. Maoni yanayotolewa ni ya kwamba ujeuri ni njia inayokubalika ili kuondolea magumu; uasherati unaonekana kuwa sehemu inayokubalika ya maisha ya kila siku. Uchunguzi mwingi umeonyesha kwamba jambo hilo laweza kumfanya mtu azoelee matendo hayo hata asione kuwa ni mabaya, sana sana vijana. Unatamani sana watoto wako wale chakula chenye kuleta afya wala si kile kichafu. Imekupasa upendezwe hata zaidi na kile kinachoingia katika akili zao. Kama Yesu alivyoonyesha, chakula hakiingii katika mioyo yetu, bali kile tunachoingiza katika akili zetu kinaweza kuingia katika mioyo yetu.—Marko 7:18-23.

21 Kutoa uongozi juu ya aina ya vipindi vinavyotazamwa na vilevile kadiri ya wakati unaotumiwa kutazama television, kunaweza kusaidia sana ukuzi wa mtoto. Television inaweza kutoa tafrija yenye kufurahisha na hata elimu fulani; lakini ikitumiwa pasipo kiasi inaweza kuwa mazoea mabaya yanayopoteza wakati mwingi sana. Wakati ni uhai, na sehemu ya wakati huo ingeweza kutumiwa bila shaka katika njia nyingine zenye faida zaidi. Ni kwa vile kutazama ‘television’ kunavyokuwa badala ya kufanya. Haichukui tu mahali pa kufanya kazi ya kutumia mwili, bali inachukua vilevile mahali pa kusoma na kuzungumza. Jamaa inahitaji mazungumzo na kuwa pamoja, na kukaa pamoja kimya tu katika chumba kimoja mkitazama television hakutatimiza uhitaji huo. Ikiwa kutazama television kupita kiasi limekuwa tatizo, badala ya kutazama television, wazazi wana.weza kusitawisha katika watoto wao kuona faida ya kufanya kazi nyingine, kama vile mchezo wenye kuleta afya, kusoma, kazi za jamaa, sana sana ikiwa wazazi wenyewe wanaongoza na kuweka mfano.

UNAPOTOA ADHABU, PASHANENI HABARI!

22. Sababu gani ni jambo la maana watoto wafahamu maneno yanayotumiwa na wazazi wao?

22 Mzazi mmoja anaeleza jambo hili aliloona:

“Mwana wangu alipokuwa mwenye umri wa miaka mitatu tu, nilimwonya sana juu ya kusema uongo, namna Mungu anavyowachukia waongo, nikitumia Mithali 6:16-19 na maandiko mengine. Alisikiliza, tena akaonekana akiitikia vizuri. Lakini kwa maoni yangu hakuwa amefahamu maana yake. Basi nikamwuliza hivi, ‘Mwanangu, je! unajua uongo ni nini?’ Akasema, ‘Sijui.’ Tangu hapo nilihakikisha kwamba amefahamu maana ya maneno hayo na kwa nini alikuwa akiadhibiwa.”

23. Kusaidia watoto waone jinsi mwendo fulani unavyofaa kunaweza kutaka nini?

23 Watoto wanapokuwa bado vitoto vichanga, huenda wazazi wakaonyesha vitu vya kuepuka ambavyo ni hatari, kama vile kushika jiko lenye moto. Lakini sababu za maonyo hayo ya kwanza ambayo ni mepesi, zinaweza kutolewa. Huenda ikawa ni kusema tu kwamba jiko “lina moto!” na kuligusa “kutakuumiza!” Walakini, tangu mwanzo, mjulishe mtoto wako kanuni ya kwamba hayo yanafanywa kwa faida yake; kisha ukazie namna sifa kama vile fadhili, huruma na upendo, zinavyotakiwa sana. Msaidie mtoto afahamu kwamba sifa hizo ndio msingi wa matakwa mema au vizuizi vyote. Kazia vilevile sababu kwa nini tendo fulani linaonyesha tabia hizo zinazotakiwa au sivyo. Wakati hilo linapofanywa kwa kulingana, unaweza kuufikia moyo wa mtoto, si akili zake tu.—Mathayo 7:12; Warumi 13:10.

24. Sababu gani ni jambo la maana mtoto aheshimu mamlaka?

24 Vilevile, lazima ya kutii na kuheshimu mamlaka imepaswa ikaziwe hatua kwa hatua. Wakati wa mwaka wa kwanza wa maisha, nia au kukosa nia ya mtoto kutii matakwa ya mtu mzima kutaanza kuonekana. Mara mtoto anapokuwa na akili, kazia kwake hali ya kuthamini daraka ambalo wazazi wanalo mbele za Mungu. Hilo linaweza kumsaidia sana mtoto apate kutii matakwa. Pasipo hilo, huenda mtoto akadhani kwamba utii ni jambo ambalo wanaamriwa waonyeshe kwa sababu tu wazazi wao ni wakubwa na wenye nguvu kuwapita. Badala yake, ikiwa mtoto anasaidiwa afahamu kwamba wazazi hawatoi mawazo yao wenyewe bali wanampa mtoto huyo mambo ambayo Muumba anasema, mambo ambayo Neno lake linasema, hilo litatia nguvu shauri na uongozi wa wazazi ambao hakuna kingine kinachoweza kufanya hivyo. Hilo laweza kumpa mtoto nguvu inayohitajiwa wakati mambo mabaya yanapoanza kutokea katika maisha yake ya uchanga, anapoanza kuona ugumu wa kufuata kanuni za haki akishawishwa au kukazwa na hali.—Zaburi 119: 109-111; Mithali 6:20-22.

25. Shauri lililo katika Mithali 17:9 linaweza kusaidiaje wazazi wawatie watoto wao adabu katika njia inayofaa

25 “Mwenye kufunika kosa anatafuta upendo, na yeye anayeendelea kusema juu ya jambo lile lile anatenga wale wanaojuana sana.” (Mithali 17:9, NW) Hivyo ndivyo ulivyo uhusiano wa watoto na wazazi. Mtoto akiisha kujulishwa kosa lake naye anafahamu kwa nini anahitaji kuchapwa, naye amechapwa, upendo umepaswa umwongoze mzazi aepuke kuendelea kusema kosa lile lile. Hata ikiwa jambo gani lilifanywa, hakikisha kuonyesha wazi kwamba unachukia lile kosa si mtoto. (Yuda 23) Huenda mtoto huyo akadhani kwamba kwa vile amekubali kutii shauri, kutajwa kwa jambo hilo mara nyingi ni kutaka kumwaibisha bure. Jambo hilo laweza kuwa na matokeo ya kumfanya mtoto ajitenge na wazazi au watoto wengine katika jamaa. Wazazi wakiwa na mashaka juu ya mfano fulani mbaya unaotokea, basi jambo hilo laweza kutajwa wakati mwingine katika mazungumzo ya jamaa. Usirudie kutaja matendo ya zamani tu, lakini badala yake zichunguze kanuni zinazohusika, namna zinavyotumika na kwa nini ni zenye maana sana kuzifuata ili kuwe na furaha yenye kuendelea.

NJIA MBALIMBALI ZA KUTOLEA ADABU

26. Sababu gani watoto wote hawaltikii vizuri adhabu ile ile?

26 “Lawama hupenya moyoni mwa mwenye ufahamu, kuliko mapigo mia moyoni mwa mpumbavu.” (Mithali 17:10) Huenda watoto mbalimbali wakahitaji kutiwa adabu katika njia tofauti. Ni lazima kufikiria tabia na nia ya mtoto mmoja mmoja. Huenda mtoto mmoja akawa mwenye kushtuka, nayo adhabu, kama vile kupiga, huenda isiwe ya lazima sikuzote. Kwa habari ya mtoto mwingine, huenda kupiga kusilete matokeo yo yote. Au huenda mtoto akawa kama yule mtumishi anayesimuliwa katika Mithali 29:19, asiyetaka “kuonywa kwa maneno; maana ajapoyafahamu hataitika.” Ikiwa hivyo, mtoto huyo angehitaji kupigwa viboko (fimbo).

27. Baba mmoja alisaidiaje mtoto wake mdogo wa kiume aache kuandika ukutani?

27 Mama mmoja anaripoti hivi:

“Mwana wangu alikuwa na umri wa miaka miwili tu wakati alipoandika ukutani alama ndogo nyekundu karibu na sakafu. Baba yake alimwonyesha alama hizo na kumwuliza habari zake. Badala ya kusema Ndiyo au La, baba alikodolewa [alikaziwa] tu macho makubwa. Mwishowe baba yake akasema, ‘Fahamu, mwanangu, mimi nilipokuwa mwenye umri kama wako, niliandika ukutani. Inafurahisha kufanya hivyo, sivyo?’ Basi, kivulana huyo sasa akatulizwa wasiwasi, uso wake ulionyesha furaha, kisha akaanza kuzungumza kwa shauku namna alivyoona furaha sana kuandika alama. Alijua baba alifahamu hayo! Walakini, alielezwa kwamba hata ijapokuwa ilifurahisha kuandika ukutani, kuta hazikuwa mahali pa kuandikia. Mazungumzo yalianzishwa, naye mtoto huyo alitaka tu kupewa sababu zaidi.”

28. Mzazi anawezaje kuepuka kubishana na mtoto?

28 Ni vizuri kutoa sababu ili kufundisha na kutoa maagizo wakati wa kutia adabu, lakini kwa kawaida si jambo linalofaa kubishana na mtoto. Mtoto wake alipobisha juu ya kufanya kazi fulani, mama mmoja alisema hivi: “Ukiisha kuifanya, tutakwenda kutembelea shamba la starehe,” jambo hilo lilikuwa lenye kumfurahisha sana kijana siku hiyo. Mtoto alikuwa akinyimwa jambo fulani lenye kufurahisha au matembezi fulani mpaka wakati angefanya kazi aliyopewa. Ikiwa mama angekuja kuangalia na kukuta kazi haijafanywa, alikuwa akisema hivi, “Kumbe, haijafanywa bado? Basi tutakwenda utakapomaliza kufanya kazi.” Hakubishana na mtoto, bali alipata matokeo fulani.

29. Jambo gani lingeweza kufanywa ill mtoto aone matokeo yasiyofaa ya kosa lake?

29 Kuona matokeo yasiyofaa ya matendo mabaya kunaweza kusaidia watoto wajifunze kufaa kwa kanuni za haki. Je! mtoto amechafua vitu? Labda kumwambia yeye mwenyewe avisafishe kutakuwa na mkazo wenye nguvu zaidi sana. Je! ametendea wengine isivyo haki au kwa ukali? Kujifunza kuomba radhi (msamaha) kunaweza kufaa sana kuondoa maelekeo hayo mabaya. Labda amevunja kitu fulani wakati wa hasira. Akiwa mwenye umri wa kutosha, labda anaweza kutakiwa afanye kazi ili apate fedha za kununua kingine badala ya hicho. Watoto wengine wanafundishwa somo la lazima kwa kunyimwa mapendeleo fulani kwa muda. Katika kundi la Kikristo, kutoshirikiana na wakosaji fulani kwa urafiki ni njia inayotumiwa kuwafanya waone aibu. (2 Wathesalonike 3:6, 14, 15) Kwa habari ya watoto wadogo, kukatazwa kwa muda ushirika wa jamaa kunaweza kuleta matokeo mengi kuliko kupigwa. Walakini, matendo ya kupita kiasi kama vile kufungia mtoto nje ya nyumba, ni tofauti na upendo unavyotaka atendewe. Njia yo yote inayotumiwa, inawapasa watoto waonyeshwe kwamba ni lazima wapate matokeo ya mwenendo wao. Hilo linawafundisha wajue kwamba wana daraka.

TOA ADABU KATIKA UPENDO

30. Sababu gani ni jambo la maana wazazi wawe na usawa wanapowekea watoto wao maongozi?

30 “Hakikisheni mambo yaliyo ya maana zaidi,” ukikumbuka kwamba “hekima inayotoka juu ni . . . ya kiasi.” (Wafilipi 1:10; Yakobo 3:17 NW) Kumbuka kwamba watoto wadogo ni nguvu inayotaka itolewe, nao wanatamani sana kujifunza na kuchunguza mambo na kujaribu kuona namna mambo mapya yanavyofanya kazi. Onyesha busara nzuri na kuwa mwenye kuchagua wakati wa kuweka mipaka na maongozi. Kunatakiwa usawa kati ya jambo la lazima na lisilo la lazima. Ukiisha kujulisha namna mipaka hiyo ilivyo, basi, badala ya kujaribu kuongoza kila jambo lililo dogo, mruhusu mtoto afurahie kutenda kwa uhuru na kwa kutumaini, akiwa katika mipaka hiyo. (Mithali 4:11, 12) Bila hivyo, watoto wako wanaweza ‘kuchokozwa’ na ‘kukata tamaa,’ nawe utachoka kwa sababu ya kufanya mambo madogo kuwa makubwa.—Wakolosai 3:21.

31. Ni mfano gani wa kutoa adhabu ambao Yehova Mungu ameweka?

31 Basi, wazazi, “azibu mwana [wenu au binti yenu wakati] tumaini liko,” lakini fanyeni hivyo katika njia ya Mungu, katika upendo. Fuateni mfano wake: “Yule ambaye Yehova anapenda anamkaripia, hata kama vile baba anavyomkaripia mwanawe ambaye anapendezwa naye.” Ifanyeni adhabu iwe bora na yenye upendo, kama ile ya Muumba wenu, kwa maana hayo “makaripio ya kutia adabu ndiyo njia ya uzima.”—Mezali 19:18, ZSB; 3:12; 6:23, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki